William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,375
- Mkuu Asha ahsante kwa majibu yako, nilifkiri na nyinyi mnahusika na hizi nyepesi nyepesi za CUF huko, lakini nimekusikia mkuu.
Heading yako inatuambia matokea ya uchaguzi Mbeya, hayo matokeo yako wapi?
........................................After all vitambulisho vyote vinapicha kama mtu atatumia kitambulisho cha mtu mwingine atajulukana.Wasiwasi wa CUF ........QUOTE]
Message ya kwanza toka kwa mama imeingia JF kama 'fragment' natafuta chanzo sikioni lakini hata hivyo;
SaidSabke, suala la kuhakiki vitambulisho vyenye picha na kulinganisha na sura halisi huwa lina uzito sawa na lile la kujua kusoma na kuandika.
Kuna illiteracy ya kusoma picha. Enzi hizi tunaruhusiwa kutumia picha zilizoziba masikio na nywele na kuacha uso tu, hapo ndo kabisa!
FMES,
Kama CUF walitegemea kushinda Mbeya vijijini wana wazimu, na hata Chadema kufikiria kwamba mgombea wao angeweza kuuzika Mbeya vijijini ni hadithi za Alinacha!..Walichouza kwa wananchi ni kuonyesha nani anayefaa kupokea ruzuku kati ya CUF na Chadema kwani yalikuwa majungu matupu!
Hivi vyama vyote vinatakiwa kuondoa different zao na kuunda umoja wa nguvu na sio kukimbilia ruzuku inapohitajika.. Chadema kabla ya Uchaguzi wa mwaka 2005, hakuna hata mmoja wetu aliyefikira wangeondoka na wabunge watano tu hasa nikitazama mikutano ya Mbowe..
Uchaguzi wa mwaka 2005 utumike kama fundisho na kama wataendelea kujenga matumaini ya uwezo wao pekee chini ya tawala ya dola CCM basi hizi ni njozi mpya kabisa!...
Namshukuru sana Mbowe kwa hotuba yake aliyoitoa Arusha na hakika matokeo ya Kiteto, Tukuyu na Mbeya vijijini yatumike kama funzo la kutazama wapi wamekosea...wajipange upya waondoe tofauti zao hasa ktk kugombea ruzuku badala ya maslahi ya Taifa..
Tulia... nani anakudanganya kama kuishi Tz ni sawa na kuishi jehanamu?Nyie vijana mnaojifanya sijui mko marekani sijui wapi mnatumika vibaya sana. Laiti kama mngekuwapo hapa na kuonja hii joto ya jiwe msinge kuwa mnaropoka hayo maneno ya kukatisha tamaa kila kukicha. Mshindwe na mlegee kwa........................
Tulia... nani anakudanganya kama kuishi Tz ni sawa na kuishi jehanamu?
Utakufa nacho kijiba cha rohoDie slowly .................
1. Wapinzani hawatapata mafanikio yoyote katika chaguzi za Tanzania bila ya kuungana.
2. Watanzania tumewapigia kelele juu ya umuhimu wa kuungana ili kuunda chama kimoja chenye nguvu.
3. Hata Waziri Mkuu wa Kenya Odinga alipitembelea Tanzania ili wapate mafanikio ya kuing'oa CCM madarakani inabidi waungane, lakini wapi.
4. Kama wameshindwa huku Mbeya vijijini hakuna wa kulaumiwa bali ni wao wenyewe wapinzani.
5. Hii danganya toto ya vyama vya upinzani 'vina ushirikiano' haitawafikisha kokote bila kuvunja vyama vilivyopo na kuunda chama kimoja chenye nguvu.
6. 2010 inakaribia na dalili si nzuri maana bado kuna mgawanyiko mkubwa miongoni mwa Wapinzani.