Frank Wanjiru
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 25,423
- 46,140
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Kigoma, leo Alhamisi Julai 16, 2026, imeifuta kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Jimbo la Kigoma Mjini yaliyompa ushindi Mbunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, Levocatus Chipando maarufu Baba Levo.
Akitoa uamuzi huo, Jaji Victoria Nongwa anayesikiliza shauri hilo amesema ushahidi uliowasilishwa na walalamikaji haukufikia kiwango cha kuwalazimisha wajibu maombi kuanza kujitetea mbele ya Mahakama.
Kesi hiyo ya uchaguzi namba 28949 ya mwaka 2025, iliyotokana na Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, ilifunguliwa na wananchi wanne waliodai kuwa ni wapiga kura wa Jimbo la Kigoma Mjini ambao ni Johary Kabourou, Luma Akilimali, Pendo Kombolela na Lumu Mwitu.
Walalamikaji walikuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi huo wakidai kuwepo kwa ukiukwaji wa sheria za uchaguzi na kuiomba Mahakama ibatilishe ushindi wa Baba Levo.
Hata hivyo, baada ya kupitia ushahidi uliowasilishwa, Mahakama imeamua kuifuta kesi hiyo hatua inayomaanisha kuwa ushindi wa Levocatus Chipando unaendelea kusimama.
Akitoa uamuzi huo, Jaji Victoria Nongwa anayesikiliza shauri hilo amesema ushahidi uliowasilishwa na walalamikaji haukufikia kiwango cha kuwalazimisha wajibu maombi kuanza kujitetea mbele ya Mahakama.
Kesi hiyo ya uchaguzi namba 28949 ya mwaka 2025, iliyotokana na Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, ilifunguliwa na wananchi wanne waliodai kuwa ni wapiga kura wa Jimbo la Kigoma Mjini ambao ni Johary Kabourou, Luma Akilimali, Pendo Kombolela na Lumu Mwitu.
Walalamikaji walikuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi huo wakidai kuwepo kwa ukiukwaji wa sheria za uchaguzi na kuiomba Mahakama ibatilishe ushindi wa Baba Levo.
Hata hivyo, baada ya kupitia ushahidi uliowasilishwa, Mahakama imeamua kuifuta kesi hiyo hatua inayomaanisha kuwa ushindi wa Levocatus Chipando unaendelea kusimama.