Matokeo ya Uchaguzi Mbeya

Date::1/31/2009
Profesa Lipumba amtaka Jaji Makame ajiuzulu
Kizitto Noya

SIKU chache baada ya Chama cha Wananchi (CUF), kushindwa katika uchaguzi wa Mbeya Vijijini, mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, ameibua shutuma nzito dhidi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) na kumtaka mwenyekiti wake, Jaji Lewis Makame, ajiuzulu.


Profesa Lipumba aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, akiwa Mtendaji wa tume,Jaji Makame, anapaswa kujiuzulu na tume hiyo kuvunjwa na kuundwa upya, kwa sababu imeshindwa

kusimamia chaguzi huru na haki.


Alisema kushindwa kwa chama chake katika uchaguzi wa Mbeya Vijijini na wapigakura wengi kutojitokeza kupiga kura, kumetokana na udhaifu wa tume hiyo, katika kusimamia uhuru na haki katika chaguzi.


"Kampeni zilitawaliwa na vituko vya mashabiki kupigwa, bendera za CUF kuchanwa, masunduku ya kura kukutwa kwa watendaji wa CCM, FFU kuwatisha wananchi na kasoro nyingine nyingi ambazo CUF imeziripoti kwa msimamizi wa uchaguzi na polisi," alisema Profesa Lipumba.


Akitoa mfano wa tukio moja baada ya jingine, Profesa Lipumba alisema, katika kata ya Ikukwa, CCM iliingilia kampeni za CUF, kubandua mabango ya mgombea wa chama hicho na kuchana bendera zake huku baadhi ya makada wake, wakinunua kadi za wapigakura kwa fedha taslimu.


Kwa mujibu wa Profesa Lipumba, Daftari la wapigakura lilikuwa na udhaifu mkubwa uliojitokeza kwa majina ya watu waliofariki dunia kuendelea kuwepo na wengine kujiandikisha zaidi ya mara moja.


Akizungumzia suala hilo, Jaji Makame alimpuuza Profesa Lipumba akisema, anongea asichokijua.


Jaji Makame aliliambia gazeti hili jana kuwa tume yake haihusiki na matukio yote aliyoyaeleza Profesa Lipumba na kwamba uchaguzi huo ulifanyika chini ya msimamizi maalum.


"Hivi ni kweli Lipumba hajui kama kama tume imeshatoa masanduku, anayepaswa kuyatunza ni msamamizi wa uchaguzi," alihoji na kuendelea " Hata kama masanduku yalikutwa kwa balozi, baada ya kuyakagua polisi walikuta nini ndani yake."


Kwa mujibu wa Jaji Makame, Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ilijitahidi kadiri ilivyoweza kufanya uchaguzi wa Mbeya Vijijini, kuwa huru na wa haki, lakini kilichovuruga ni kuondolewa kwa mgombea wa Chadema katika suala la kisheria.


"Sababu za matatizo hayo sio tume kwani imefanya kila liwezalo ikiwamo kutoa elimu ya uchaguzi katika vijiji vyote vya Mbeya ambako huenda Lipumba hakufika. Hapa kuna sababu nyingine, na sisi tunaungana na watu wanaosema kuwa uchache wa wapigakura umetokana na Chadema kuenguliwa kwenye uchaguzi huo," alisema.


Alisema ingawa hiyo ndiyo sababu ya msingi, halalamiki kwani Chadema iliondolewa kwa mujibu wa sheria za uchaguzi na wala isingekuwa vyema tume kukiuka sheria hiyo kwa sababu ya kuuhamasisha uchaguzi huo.


Uchaguzi mdogo wa ubunge Mbeya Vijijini ulifanyika Januari 25 mwaka huu ambapo watu waliopiga kura walikuwa 44,855 kati ya 127780 waliojiandikisha.


Kura halali zilikuwa 4394, na kura zilizokataliwa zilikuwa 914.


Mgombea wa CCM Mchungaji Lackson Mwanjali alishinda kwa kura 32867 sawa na asilimia 73, CUF ilipata kura 10,578 ambazo ni asilimia 23 na Chama Cha Sauti ya Umma (Sau) kiliambulia kura 496 sawa na asilimia moja hivyo kura zote zilizopigwa ni sawa na asilimia 35.


Siku moja baada ya Tume ya Uchaguzi kutangaza matokeo hayo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimejigamba kwamba asilimia 65 ya watu ambao hawakujitokeza kupiga kura, ni watu waliotaka kikipigia kura chama hicho.


Naibu katibu Mkuu wa Chadema Zitto Kabwe aliliambia gazeti hili jana kuwa watu hao ni wapenzi na wanachama wake ambao wameamua kutojitokeza kwa sababu ya chama hicho kuenguliwa.


Kabwe alitoa kauli hiyo baada ya Mwananchi kumtaka asema endapo anadhani kuwa idadi ya wapigakura ambao hawakujitokeza, ni wapenzi na wanachama wa Chadema.


"Unachosema ni kweli ni hii ni kwa sababu Tume imemwengua mgombea wetu ambaye alikuwa chaguo la wengi," alijibu kwa ufupi Kabwe na kuongeza:


Alisema wapiga kura hao waligoma kupiga kura kwa sababu walimkosa yule waliyetarajia kumchagua ambaye ni mgombea wa chama hicho alienguliwa katika kinyang'anyiro hicho Sambwee Shitambala.

Chanzo: Mwananchi
 
Okay Watanzania wenzangu uchaguzi umekwisha Mbeya japo jamaa WaCUF wameachwa kwenye mataa kama walivyozoeleshwa hilo ni lao au vipi ?
Sasa kwa vile tuanajadili demokrasia ya vyama vingi nchini kuna umuhimu wa kuweka tofauti zetu za kichama kama walivyosema kule Bungeni kuwa bado ushirikiano wao katika shughuli za Bunge upo na una nguvu zisizoyumbika au kuyumbishwa kutokana na migongano inayotokea katika kutafuta tonge zao.

Kwa vyama vyote vya siasa upande wa upinzani wasikae na kushangilia au kuchekelea jinsi vyama vilivyoshiriki vilivyoanguka ,muhimu ni kutazama utaratibu mzima wa uchaguzi ulivyoendeshwa aidha ni kuungana na vyama vilivyoshiriki kuona kama taratibu zilikiukwa na zilikiukwa kwa kiasi gani ,hili ni lazima liwe suala la pamoja sio la kuwacha kwa kuwa tu hatukushiriki hivyo halituhusu.

Safari tuendayo ni ndefu sana na itatuchukua muda mrefu ikiwa hatukuhisabisha matukio ya uchaguzi hasa kufuatwa kwa taratibu za uendeshaji uchaguzi kwani huku ndio kujifunza na kueka mikakati ya ujenzi wa uchaguzi ulio huru na wa haki, haitakiwi kwa vyama vya upinzani kujitenga ni lazima mkishamaliza mechi mnarudi mezani na kuona kwa kina wapi Chama Tawala wamepiga na kubomoa sheria,kwa nini litokee jambo hili,na kufuatilia utaratibu mzima ili yale matatizo yaliosababishwa na serikali yaanikwe kiumoja na kwa faida ya wotehapo baadae.Vyama kushiriki kimoja kimoja au kwa ushirikiano sio jambo baya ila ni muhimu katika nafasi nyeti kama ile ya Uraisi,kwani ikiwa huku tunakotokea mambo yameshaekwa sawa basi yeyote atakae ukwaa uraisi nguvu yake haitofanana na hawa maraisi wa sasa tulio nao. Hivyo napendelea nguvu za kuungana zipelekwe kwenye kiti cha Uraisi huku kwenye ubunge kunaweza kuachwa tu,wananchi wachague wanaempenda hapo mtaani pao.

Sasa maoni yangu ni kuukagua uchaguzi mdogo huu wa Mbeya na hata kule Tarime na kwengineko ili mambo haya yafyatiliwe kisheria ,sio uchaguzi umekwisha CUF kakataa ,serikali imekubali na mwengine yeye hayumo na kuwa yameisha ,kwa kuiwacha hali hii ipite na kuwa ndio yamekwisha basi ni hasara kwa vyama vya upinzani,tena ni hasara kubwa maana chance za kuwafikisha wale wote walioburuga na kuuchafua Uchaguzi katika vyombo vya sheria wapo ushahidi upo,sasa kusema ni kazi ya CUF pekee itakuwa ni makosa naamini vyama vyote vina haki ya kusimamia utekelezaji wa kufanyika kwa uchaguzi usio kuwa na mizengwe na hivyo ni kuungana na kuwa kitu kimoja katika kuyadai mambo haya yafuatiliwe na wahusika wapelekwe kwenye mkondo wa sheria.
Mkuu wa Tume kasema yeye hahusiki kabisa alikwishamuachia mkuu alieteuliwa kuendesha uchaguzi huo kwa maana kama ni kesi au mashitaka basi yaelekezeni kwa huyo na sio yeye bila ya shaka yeye amekwishajitua mzigo na kumbebesha mwengine,sasa huyo mwengine asiachiwe aendelee kula fedha ya rushwa ni lazima imtokee puani kwa kukosa kutunza amana alioachiwa ya kuendesha uchaguzi kihalali.Naomba kuwakilisha hoja.
 
Hii kauli tata hebu nipe shule kidogo...Mbeya was so obvious wanapiga kura hawakuwa na chaguo, imenikumbusha ile enzi za Jembe na nyundo ama picha na kivuli ama nyumba na something, nadhani wakumbuka hizo changuzi enzi za mwalimu. Kilichotokea Jamhuri ya watu wa Mbeya ni wananchi kutoona umuhimu wa kwenda kupiga kura kwa mgombea wasiye mpenda.....ndo maana turn out ilikuwa ndogo vile. Tusikimbilie historia kusimulate mambo ya Tz

respect

Ushi

- Mkuu wangu Ushi, heshima mbele sana nina swali moja tu kwako, ulipofanyika uchaguzi wa mbunge huko Mbeya mwaka 2005, huyu mgombe awa Chadema hakuwepo? Au Chadema haikushiriki?

- Ninajaribu kuielewa hii habari kwamba wananchi hawakutaka kupiga kura kwa kuwa chaguo lao lilkuwa Chadema, sasa 2005 ilikuwaje? Maana machagua ya Chadema si yanafahamika kama vile majimbo ya kinaa Zitto, Dr. Slaa, Ndesamburo, sasa huku Mbeya kuna siri gani mnayoijua hebu tumegeeni kidogo.

By the way, nimeimiss beep yako lakini nitaku-beeep kesho.
 
- Mkuu wangu Ushi, heshima mbele sana nina swali moja tu kwako, ulipofanyika uchaguzi wa mbunge huko Mbeya mwaka 2005, huyu mgombe awa Chadema hakuwepo? Au Chadema haikushiriki?

- Ninajaribu kuielewa hii habari kwamba wananchi hawakutaka kupiga kura kwa kuwa chaguo lao lilkuwa Chadema, sasa 2005 ilikuwaje? Maana machagua ya Chadema si yanafahamika kama vile majimbo ya kinaa Zitto, Dr. Slaa, Ndesamburo, sasa huku Mbeya kuna siri gani mnayoijua hebu tumegeeni kidogo.

By the way, nimeimiss beep yako lakini nitaku-beeep kesho.


Ulipofanyika uchaguzi mwaka 2005 Shitambala hakuwepo huko, si umesoma mwenyewe kwenye hotuba yake huko?

Wakati huo CCM ilipata zaidi ya kura 64,000. Kwenye uchaguzi wa mwaka huu 2009, CCM imepata kura nusu ya kura ilizopata mwaka 2005. Kwa maneno mengine pamoja na kuwa wapiga kura wameongezeka kutokana na wengine kuandikishwa upya, CCM haijaweza kufikisha hata nusu ya kura ambazo ilipata mwaka 2005. Kwa hiyo kura za CCM zimeshuka by 50%. Kura za CUF zimeongezeka kidogo kutoka elfu 8 mpaka elfu 10. Wengine waliobaki wameacha kupiga kura.

Basi itakuwa huko Mbeya mambo yamebadilika sana toka mwaka 2005 ambapo Kikwete alikuwa 'chaguo la Mungu' mpaka mwaka 2009 ambapo ametajwa kwenye orodha ya mafisadi.(machaguo ya shetani) Hata hali ya CHADEMA itakuwa imebadilika sana huko toka mwaka 2005 wakati Mbowe anashindana na 'Chaguo la Mungu' mpaka mwaka 2009 wakati wakina Zitto Kabwe wamekwenda huko kufanya Operesheni Sangara wakina na Mgombea bora zaidi Kijana Shitambala.

Asha
 
Kumbe jibu alilikuwa nalo Jaji Makame, anapokiri kwamba uchache wa waliojitokeza kupiga kura Mbeya Vijijini ulichangiwa na kuenguliwa kwa mgombea wa Chadema!

Inaonekana alielewa tangu awali!!!
 
Ulipofanyika uchaguzi mwaka 2005 Shitambala hakuwepo huko, si umesoma mwenyewe kwenye hotuba yake huko?

Wakati huo CCM ilipata zaidi ya kura 64,000. Kwenye uchaguzi wa mwaka huu 2009, CCM imepata kura nusu ya kura ilizopata mwaka 2005. Kwa maneno mengine pamoja na kuwa wapiga kura wameongezeka kutokana na wengine kuandikishwa upya, CCM haijaweza kufikisha hata nusu ya kura ambazo ilipata mwaka 2005. Kwa hiyo kura za CCM zimeshuka by 50%. Kura za CUF zimeongezeka kidogo kutoka elfu 8 mpaka elfu 10. Wengine waliobaki wameacha kupiga kura.

Basi itakuwa huko Mbeya mambo yamebadilika sana toka mwaka 2005 ambapo Kikwete alikuwa 'chaguo la Mungu' mpaka mwaka 2009 ambapo ametajwa kwenye orodha ya mafisadi.(machaguo ya shetani) Hata hali ya CHADEMA itakuwa imebadilika sana huko toka mwaka 2005 wakati Mbowe anashindana na 'Chaguo la Mungu' mpaka mwaka 2009 wakati wakina Zitto Kabwe wamekwenda huko kufanya Operesheni Sangara wakina na Mgombea bora zaidi Kijana Shitambala.

Asha

Uchambuzi makini huu...chaguo la shetani...duuu!! kuna wenzetu hawapendi kusikia ama kujua ukweli. Nina uhakika mgombea wa Chama Makini CHADEMA angekuwepo kwenye uchaguzi picha ingekuwa tofauti sana....
 
Ulipofanyika uchaguzi mwaka 2005 Shitambala hakuwepo huko, si umesoma mwenyewe kwenye hotuba yake huko?

- Now I see, kumbe ndio maana ameshidwa kujua sheria za uchaguzi maana si mkazi wa kule Mbeya, au kuna ya zaidi?
 
Uchambuzi makini huu...chaguo la shetani...duuu!! kuna wenzetu hawapendi kusikia ama kujua ukweli. Nina uhakika mgombea wa Chama Makini CHADEMA angekuwepo kwenye uchaguzi picha ingekuwa tofauti sana....

Nakwambia! Kama ukifanya mahesabu ya kura walizopata CCM Mbeya vijijini kwa kuzingatia idadi ya wapiga kura wote waliojiandikisha, yaani laki 1 na elfu 20. Basi CCM imepata asilimia 26 ya Kura zote zilizopaswa kupigwa, CUF asilimia 8; Kwa hiyo hapa kulikuwa na asilimia zingine kama 60 hivi za wapiga kura ambao inaonekana hawakutaka CUF wala CCM ndio maana hawakwenda kupiga kura kama tutasema kuwa asilimia 5 ya watu hao wasingepiga kura kwa kuwa ama walikuwa wagonjwa au wamepoteza kadi zao. Swali ni je, hao 60% walikuwa wanamtaka nani ili wasikie hamu ya kwenda kupiga kura?

Asha
 
- Now I see, kumbe ndio maana ameshidwa kujua sheria za uchaguzi maana si mkazi wa kule Mbeya, au kuna ya zaidi?

Sasa unaleta ubazazi, hebu soma hotuba yake hapa si iliwekwa humu, hebu tafuta link. Amejieleza vizuri kuwa ni mkazi wa Mbeya na alifungua kampuni yake ya uwakili huko. Nimesema hakuwepo kule nina maana ya kuwa hakuwepo kati ya waliogombea mwaka 2005. Waligombea wengine wakati huo, kwa historia yake aliyoieleza kwenye hotuba yake inaonyesha wakati huo alikuwa Kapteni wa JWTZ, asingeweza kugombea. Hebu mtu atupe link ya ile hotuba yake mi nimeshindwa kuiona.

Asha
 
1.

- Mwaka huu wamepiga kura wananchi wangapi mkuu?

2.

- Again naomba kujua wananchi wanagapi walipoiga kura kwenye hii by-election?

Umechoka. Nenda kampumzike. Urudi kujadili akili zikiwa zimetulia. Hili limeshaandikwa sana hapa tena hata wewe mwenyewe umeandika kuwa ni wapiga kura laki moja na elfu ishirini.

Asha
 
Back
Top Bottom