Matokeo ya Uchaguzi Mbeya

Wapinzani hawatapata mafanikio yoyote katika chaguzi za Tanzania bila ya kuungana. Watanzania tumewapigia kelele juu ya umuhimu wa kuungana ili kuunda chama kimoja chenye nguvu. Hata Waziri Mkuu wa Kenya Odinga alipitembelea Tanzania ili wapate mafanikio ya kuing'oa CCM madarakani inabidi waungane, lakini wapi.

Kama wameshindwa huku Mbeya vijijini hakuna wa kulaumiwa bali ni wao wenyewe wapinzani. Hii danganya toto ya vyama vya upinzani 'vina ushirikiano' haitawafikisha kokote bila kuvunja vyama vilivyopo na kuunda chama kimoja chenye nguvu.

2010 inakaribia na dalili si nzuri maana bado kuna mgawanyiko mkubwa miongoni mwa Wapinzani. CCM haistahili kuendelea kuwa madarakani kutokana na matatizo mbali mbali yakiwemo ya mafisadi, lakini Wapinzani kwa kutotaka kuungana wanaisadia sana CCM kuendelea kubaki mdarakani kwa kuyaweka mbele maslahi yao badala ya yale ya Taifa. Enyi wapinzani sikilizeni vilio na ushauri wa Watanzania ili muungane kabla ya uchaguzi wa 2010 kwani bado kuna muda wa kutosha kabisa kuweza kufanya hivyo.
BAK,
Zaidi ya nusu ya tunaochangia humu tunaonekana ni WAPINZANI. Viongozi wa upinzani huko waliko wanatusikiliza na kutusoma sana.Tumewasaidiaje/Tunawasaidiaje ili WAUNGANE/WAELEWANE?
 
Wapinzani watanyosheana vidole, watainyoshea tume ya uchaguzi, watanyoosha vidole kwa CCM, lakini itakuwa kila baada ya uchaguzi ni kilio cha samaki. Bila kuungana na kudai kwa nguvu zote tume ya uchaguzi iwe huru ni kupoteza muda. Lakini muhimu ya yote ni kuungana (Umoja ni nguvu....). Waangalie mfano wa Kenya walipokwa nawashindwa, walipoweka maslahi binafsi kando, KANU ikaondoka.

Hivi kweli hadi lini wapinzani wataukubali mfumo wa kugawanywa ili CCM iendelee kuongoza?.
 
Lakini wafu hawapigi kura. Hata kama majina yao yamo kwenye orodha ya wapiga kura.

Inasikitisha kuona mpaka kufikia karne hii tuliyo nayo bado WATANZANIA tupo naive kiasi hichi leo hii huyu kiumbe ajitae jasusi anasema eti hata kama kuna majina ya watu ambao wamesha fariki anadai hawapigi hakuweza hata kujiuliza kwanini sasa yawachwe hayomajina jibu lipo jepesi na imani analielewa na pia ukiangalia yule mzee william aliejiandikisha mara mbili hivi kitambulisho cha kupiga kura kimepotea nje ya nchi hapa tujiulize jamani tusiwe naive than eti herufi moja iliandikwa kimakosa poleni ndugu zangu tuna safari refu halafu yake tunakwenda kwamiguu
 
Hili suala la kuungana linakuzwa sana kama ndio njia pekee ya kushinda. Muungano ni kitu kizuri kama kinawezekana kama hakiwezekani ni mzigo tu wa kurudisha nyuma. Kwani kule Pemba CUF imeshinda kwa kuungana na nani? Au kule Tarime CHADEMA ilishinda hivi karibuni kwa nguvu ya chama kipi? Si ilishinda pamoja na vyama vingine vyote kuwa dhidi ya CHADEMA? Tunapoteza muda mwingi zaidi kuwataka wapinzani waungane na kuwasema vibaya kwa kutoungana badala ya kutumia muda mwingi zaidi na akili zetu za uchambuzi kujenga hoja za kuchochea Tume huru ya uchaguzi katika taifa letu, ama kuhakikisha kuna sheria nzuri za uchaguzi. Au potelea mbali basi tutumie muda huu kueneza vyama vya siasa tunavyovijua ili viwe na muundo wenye nguvu huko chini kabisa. Tukifanya hivyo, wallah nawaambia Tanzania itabaki na vyama vitatu tu; CCM, CHADEMA na CUF hapo hata kuungana au kushirikiana itakuwa rahisi sana. Hebu mlioko ughaibuni tupeni uzoefu wa nchi mbalimbali, je muungano wa vyama ndio njia kuu ya kufanya vyama vya upinzani vishinde? Mi nadhani tuchukulie tu hii kama njia mojawapo badala ya kila siku, wapinzani waungane waungane! Wapinzani bila kuungana hawaashindi CCM. Hapa kwetu Zanzibar CUF huwa inashinda pamoja na kuwa baadhi ya vyama vya upinzani huwa vinaipinga. Tusitengeneze Simba wa karatasi anayeitwa muungano wa vyama vya upinzani halafu kila siku tunaanza kumwogopa wenyewe

Asha
 
Wapinzani hawatapata mafanikio yoyote katika chaguzi za Tanzania bila ya kuungana. Watanzania tumewapigia kelele juu ya umuhimu wa kuungana ili kuunda chama kimoja chenye nguvu. Hata Waziri Mkuu wa Kenya Odinga alipitembelea Tanzania ili wapate mafanikio ya kuing'oa CCM madarakani inabidi waungane, lakini wapi.

Kama wameshindwa huku Mbeya vijijini hakuna wa kulaumiwa bali ni wao wenyewe wapinzani. Hii danganya toto ya vyama vya upinzani 'vina ushirikiano' haitawafikisha kokote bila kuvunja vyama vilivyopo na kuunda chama kimoja chenye nguvu.

2010 inakaribia na dalili si nzuri maana bado kuna mgawanyiko mkubwa miongoni mwa Wapinzani. CCM haistahili kuendelea kuwa madarakani kutokana na matatizo mbali mbali yakiwemo ya mafisadi, lakini Wapinzani kwa kutotaka kuungana wanaisadia sana CCM kuendelea kubaki mdarakani kwa kuyaweka mbele maslahi yao badala ya yale ya Taifa. Enyi wapinzani sikilizeni vilio na ushauri wa Watanzania ili muungane kabla ya uchaguzi wa 2010 kwani bado kuna muda wa kutosha kabisa kuweza kufanya hivyo.

Mkuu hili sio suluhisho; mie naamini 2010 wapinzani watapata wabunge wengi zaidi; na sio kwa sababu ya kuungana bali ni ikwa sababu ya nguvu binafsi za chama; utaona Chadema kwa bara itakavyowakimbiza ( hata wakiwa na vyama vitano ktk jimbo no matter), utaona CUF zanzibar mambo yatakuwa magumu zaidi kwa CCM; Kuungana ni kukaribisha unafiki ktk vyama; kila chama kina falsafa na vision yake; mtaungana vipi?; l abda mtengeneze chama kipya nacho sio muungano ni chama kipya; so mie naona cham safi kitaonekana mbele ya safari; tena wasiungane maana tayari tumeshaonja joto ya jiwe ktk kuungana watu wanataka kubebwa; that not the case
 
Mbona vyama vinaungana tu lakini haviiwezi CCM. Kwani hapa Mbeya Vijijini si vyama vya upinzani vya TLP, NCCR na PPT vyote viliungana kuisaidia CUF lakini vimeshindwa. Imagine vyama vinne vya upinzani vimeungana dhidi ya chama kimoja CCM na bado wameshindwa. Kwani ili muungano wa vyama uwepo ni mpaka CHADEMA nayo iwepo? CHADEMA haikuwepo kwenye muungano huo wa Mbeya Vijijini lakini muungano ulikuwepo na umeshindwa vibaya. CHADEMA ingefanya vizuri zaidi kuliko huo muungano, nakumbuka vyombo vya habari viliandika kuwa kule Tarime palikuwa na muungano wa TLP, CUF na NCCR dhidi ya CCM ambao ulielezwa kwamba ungetoa upinzani mkali. Lakini matokeo yake CHADEMA ndio ikashinda kwa uzembe wa kina Makamba. Huo muungano wa NCCR na wenzake na kile chama cha DP si walipata chini ya asilimia 5 za kura?

CCM imeushinda muungano wa vyama mbeya vijijini, tena hata kinara wa ushirikiano Mrema naye alikuwepo kumnadi mgombea wa CUF lakini bado wakashindwa.


........ndiyohiyo
 
Kuungana hapa sio kwamba CHADEMA, NCCR, CUF, CHAUSTA, SAU, UDP nk waungane wawe na chama kimoja, hapo itakuwa ngumu, japo kama ingewezekana ingekuwa bora. Lakini muungano uwe kama Kenya wakati wa "Rainbow Coalition" ama juzujuzi "Pentagon", vyama vinakuwa chini ya mwamvuli mmoja wa makubaliano. Ina maana vyama vibaki kama vyama, lakini vikubaliane kuweka mgombea mmoja wa uRais na wabunge, madiwani nk. Ila kwa Tanzania ni wakati kuweka nguvu ya kuachiana majimbo ya ubunge na udiwani, wakiweza kupata madiwani na wabunge wengi haitakuja kushindikana kuachiana hata nafasi ya Rais.

Umoja ni muhimu, kama vyama vyote vikiamua kudai tume huru, hata kususia chaguzi, nina imani hiyo pressure na pia itakayopatikana toka kwa nchi wahisani tutapata tume huru. Wakati wa mjadala wa Zanziba (muafaka), vyama vingine viliomba kushiriki, kusema ukweli pale ndio ilikuwa wakati muafaka vyama vyote vingeshiriki na kuweka nguvu pamoja, kama ingepatikana tume huru Zanziba na mengineyo, basi ingebidi na Bara ifanyike hayo hayo kama ya Zanziba.
 
TANU wakati ule wa kupata uhuru ilishinda bila KUUNGANA na chama kingine chochote. Naamini ule ndio ulikuwa uchaguzi HURU na wa HAKI wa MWISHO nchi hii. Chaguzi zilizofuata baada ya hapo ni MAIGIZO na VICHEKESHO vitupu hadi leo! Tatizo sio kuungana, tatizo ni jinsi tunavyoziendesha chaguzi hizi, wapiga kura wetu wengi vijijini ni MASIKINI sana, elimu ndogo sana ya URAIA, hatujapata bado KIONGOZI mwenye MVUTO na HAIBA, mwenye kipaji cha UONGOZI upande wa upinzani.
 
Kuungana hapa sio kwamba CHADEMA, NCCR, CUF, CHAUSTA, SAU, UDP nk waungane wawe na chama kimoja, hapo itakuwa ngumu, japo kama ingewezekana ingekuwa bora. Lakini muungano uwe kama Kenya wakati wa "Rainbow Coalition" ama juzujuzi "Pentagon", vyama vinakuwa chini ya mwamvuli mmoja wa makubaliano. Ina maana vyama vibaki kama vyama, lakini vikubaliane kuweka mgombea mmoja wa uRais na wabunge, madiwani nk. Ila kwa Tanzania ni wakati kuweka nguvu ya kuachiana majimbo ya ubunge na udiwani, wakiweza kupata madiwani na wabunge wengi haitakuja kushindikana kuachiana hata nafasi ya Rais.

Umoja ni muhimu, kama vyama vyote vikiamua kudai tume huru, hata kususia chaguzi, nina imani hiyo pressure na pia itakayopatikana toka kwa nchi wahisani tutapata tume huru. Wakati wa mjadala wa Zanziba (muafaka), vyama vingine viliomba kushiriki, kusema ukweli pale ndio ilikuwa wakati muafaka vyama vyote vingeshiriki na kuweka nguvu pamoja, kama ingepatikana tume huru Zanziba na mengineyo, basi ingebidi na Bara ifanyike hayo hayo kama ya Zanziba.

Kenya unadhani yalikuwa makundi mawili tu ya PNU na ODM kwenye uchaguzi wa urais, ubunge na udiwani? Yalishiriki mavyama kibao tu mengine kivyao vyao. Suala sio kuungana tu au kushirikiana. Mfano wa Kenya ni mfano mbovu sana kwa kuwa Kenya hakuna vyama kamali vya siasa, ni vikundi tu vinavyoongozwa na personalities za watu. ODM ilikuwa ni muunganiko wa personalities za watu hao unawaoita Pentagon. Ni kama leo CHADEMA iamue, kule Kigoma kuwe na Zitto, Kagera Baregu, Kilimanjaro Ndesambaro halafu imchukue Prof Lipumba Tabora ndio itengeneze pentagon ili kupata kura katika maeneo yao. Tanzania ni tofauti kidogo.

Kuhusu vyama kushirikiana mjadala wa muafaka hapa Zanzibar, haina maana yoyote kwa kuwa mjadala ulikuwa kati ya vyama vya CUF na CCM. Ingekuwa na maana kama mjadala ungekuwa kati ya CUF na Serikali iliyoiba kura na ambayo ndio iko madarakani.

Soma tena post yangu hapo juu, muungano au ushirikiano wa vyama ni kitu kinachoweza kuongeza nguvu ya kushinda lakini si njia pekee ya kushinda, na si lazima kwamba mkiungana tu mnashinda.

Nataka watu waondokane na huu utumwa wa kufikiri kwamba bila muungano wa vyama hakuna mabadiliko Tanzania

CCM imeshajua kuwa wananchi wanahuu utumwa ndio maana inapenyeza mamluki katika muungano wa vyama. Lakini pia kwa kujua hili, mtakumbuka pia CCM iliunda muungano wake wa vyama vidogo vya upinzani ulikokuwa na vyama vingi zaidi kuliko huu muungano wa vyama vinne, ulikuwa chini ya DP na SAU nao waliuzindua kwa kishindo ukawa unakabiliana na muungano wa vyama vya CHADEMA, TLP, CUF na NCCR. Kwa hiyo tukitegemea muungano tu, tutakatishwa tamaa na kujikatisha tamaa.


Asha
 
Mbona vyama vinaungana tu lakini haviiwezi CCM. Kwani hapa Mbeya Vijijini si vyama vya upinzani vya TLP, NCCR na PPT vyote viliungana kuisaidia CUF lakini vimeshindwa. Imagine vyama vinne vya upinzani vimeungana dhidi ya chama kimoja CCM na bado wameshindwa. Kwani ili muungano wa vyama uwepo ni mpaka CHADEMA nayo iwepo? CHADEMA haikuwepo kwenye muungano huo wa Mbeya Vijijini lakini muungano ulikuwepo na umeshindwa vibaya. CHADEMA ingefanya vizuri zaidi kuliko huo muungano, nakumbuka vyombo vya habari viliandika kuwa kule Tarime palikuwa na muungano wa TLP, CUF na NCCR dhidi ya CCM ambao ulielezwa kwamba ungetoa upinzani mkali. Lakini matokeo yake CHADEMA ndio ikashinda kwa uzembe wa kina Makamba. Huo muungano wa NCCR na wenzake na kile chama cha DP si walipata chini ya asilimia 5 za kura?

CCM imeushinda muungano wa vyama mbeya vijijini, tena hata kinara wa ushirikiano Mrema naye alikuwepo kumnadi mgombea wa CUF lakini bado wakashindwa.


........ndiyohiyo

hapo ndio ugundue kuwa huo unaoitwa muungano ni kama mchezo wa kuigiza au kiini macho.
 
CCM imeshinda uchaguzi wa Mbeya Vijijini. Kutokana na matokeo ambayo nimeyaona hapa kwenye kata mbalimbali mpaka sasa CCM inaongoza. Hata hivyo, idadi ya wapiga kura imekuwa ndogo sana. Katika kata za mjini kama utengule usongwe ambayo ina mji wa Mbalizi, wapiga kura waliojitokeza katika vituo vingi hawafiki hata asilimia 10. Wakati kwenye kata ya Ilembo waliojitokeza ni asilimia 15 tu ya wapiga kura wote. Kwenye kata nyingi zilizobaki wapiga kura waliojitokeza ni wastani wa asilimia 25, kati kata za Santilya, Iwiji, Iyunga Mapinduzi, Iwindi, Ikukwa nk. Mpaka ilipofika mchana hapakuwa na foleni za wapiga kura, watu wengi walikuwa makanisani, wengine majumbani na baadhi mashambani. Watu wengi walieleza dhamira ya kutokupiga kura kutokana na kampeni kupoteza mvuto baada ya mgombea wa CHADEMA kuenguliwa. Wananchi hao walikuwa wakielezea kwamba wanasubiri kupiga kura mwaka 2010 kukiwa na ushindani kati ya Shitambala na mgombea wa CCM. Nawapongeza timu yetu, hususani Mzee Malecela, kwani mbinu iliyotumika mchana ya kutuma mabalozi kwenye kila kaya kuhimiza watu kwenda kupiga kura ilifanya jioni ya kati ya saa 9 na 11 wapiga kura kujitokeza kiasi ambao kwa kweli wamechangia ushindi wa CCM. Nitawaletea matokeo kamili lakini katika vituo vingi CCM imeshinda kati ya asilimia 70 na 80 ya kura zilizopigwa. Nasubiri ya kata chache zilizobaki ili kupata matokeo kamili. Bado naendelea kujiuliza sababu ya watu kujitokeza chini ya asilimia 20 kupiga kura kama ni hiyo inayosemwa tu ya watu kususa baada ya CHADEMA kuondolewa au kuna sababu nyingine ya siri. CUF imeanza kulalamika kwamba imeshindwa kwa sababu ya hujuma za CCM na CHADEMA. Kwamba CCM imechukua kadi za kura kwa kubadilishana na mbolea na kwamba CHADEMA imechochea wananchi wasione umuhimu wa kupiga kura kwa kuwa wagombea wa CCM na CUF wameshirikiana kumwondoa mgombea aliyekuwa chaguo la wananchi wengi. Mrema naye ametoa lawama kwa CHADEMA kwamba ndio chanzo cha kuvurugika kwa uchaguzi huo.

…….ndiyohiyo

Watu wanasubiria 2010 wachague mbunge wao sio sasa; thats Good for chadema kumbe wamefanikiwa kushawishi asilimia almost 65 hawakupiga kura; mzee wa kabila wa miaka karibu 80 aliseama kuwa sie tutamsubiria SHITAMBALA 2010 Mkampa kila neno baya
 
TANU wakati ule wa kupata uhuru ilishinda bila KUUNGANA na chama kingine chochote. Naamini ule ndio ulikuwa uchaguzi HURU na wa HAKI wa MWISHO nchi hii. Chaguzi zilizofuata baada ya hapo ni MAIGIZO na VICHEKESHO vitupu hadi leo! Tatizo sio kuungana, tatizo ni jinsi tunavyoziendesha chaguzi hizi, wapiga kura wetu wengi vijijini ni MASIKINI sana, elimu ndogo sana ya URAIA, hatujapata bado KIONGOZI mwenye MVUTO na HAIBA, mwenye kipaji cha UONGOZI upande wa upinzani.

Nimependa hoja yako, wakati ule TANU ilikuwa inapambana na vyama vipi? ANC, AMNUT na mkoloni. Halafu kulikuwa na mapandikizi pia ya mkoloni kwenye baadhi ya hivyo vyama vya upinzani kama sasa ambapo CCM ina mapandikizi yake kwenye baadhi ya vyama. Hapa kwetu Zanzibar, ASP nayo ilishinda peke yake ingawa ASP nayo asili yake ni muungano wa makundi kama ambayo TANU nayo ilikuwa mabadiliko ya TAA. Huku wapinzani wa ASP nao walibadilika huko Pemba na waliungana pia. Hata hivyo, bado katika uchaguzi, ushindi ulipatikana kwa vyama kusimama vyenyewe.

TANU ilishinda kwa kuwa Nyerere alikwenda kujenga chama vijijini, CHADEMA nayo si inajenga chama hicho kwenye Operesheni Sangara? Naambiwa hii ndio sababu ya chama hicho kuwa na nguvu Mbeya Vijijini. Halafu TANU ilishirikiana na makundi ya kijamii kama Vyama vya wananyakazi. Haikupoteza muda mwingi kutaka ushirikiano na ANC, AMNUT nk. Sasa vipi leo tunatumia muda mwingi kutaka vyama kuungana badala ya kutumia muda mwingi kujenga vyama vyenye nguvu?

Asha
 
Je, ni ukweli kama uamuzi wa Tume kumwondoa Shitambala baada ya kuwasilisha hii rufaa yake Mbeya vijijini: Kampeni, uchaguzi na yatokanayo - Page 40 - JamiiForums.com

umechangia kufanya watu wasusie kwenda kupiga kura?

Kama ndivyo, kwanini Tume haikutumia mamlaka iliyokuwa nayo kwenye kifungu cha 38(4) ya kupokea fomu kwa namna yoyote na kuruhusu ushindani zaidi ambao ungekuwepo kama huyu mgombea angeshiriki?

Bado mpaka sasa matokeo hayajatangazwa, unajua jimbo hili lina kata 17, na inapakana na wilaya zingine nyingi za Mbeya kuna matokeo yalichelewa sana kuletwa, bado majumuisho yanamaliziwa lakini ni wazi CCM imeshashinda

....ndiyohiyo
 
Kenya unadhani yalikuwa makundi mawili tu ya PNU na ODM kwenye uchaguzi wa urais, ubunge na udiwani? Yalishiriki mavyama kibao tu mengine kivyao vyao. Suala sio kuungana tu au kushirikiana. Mfano wa Kenya ni mfano mbovu sana kwa kuwa Kenya hakuna vyama kamali vya siasa, ni vikundi tu vinavyoongozwa na personalities za watu. ODM ilikuwa ni muunganiko wa personalities za watu hao unawaoita Pentagon. Ni kama leo CHADEMA iamue, kule Kigoma kuwe na Zitto, Kagera Baregu, Kilimanjaro Ndesambaro halafu imchukue Prof Lipumba Tabora ndio itengeneze pentagon ili kupata kura katika maeneo yao. Tanzania ni tofauti kidogo.

Kuhusu vyama kushirikiana mjadala wa muafaka hapa Zanzibar, haina maana yoyote kwa kuwa mjadala ulikuwa kati ya vyama vya CUF na CCM. Ingekuwa na maana kama mjadala ungekuwa kati ya CUF na Serikali iliyoiba kura na ambayo ndio iko madarakani.

Soma tena post yangu hapo juu, muungano au ushirikiano wa vyama ni kitu kinachoweza kuongeza nguvu ya kushinda lakini si njia pekee ya kushinda, na si lazima kwamba mkiungana tu mnashinda.

Nataka watu waondokane na huu utumwa wa kufikiri kwamba bila muungano wa vyama hakuna mabadiliko Tanzania

CCM imeshajua kuwa wananchi wanahuu utumwa ndio maana inapenyeza mamluki katika muungano wa vyama. Lakini pia kwa kujua hili, mtakumbuka pia CCM iliunda muungano wake wa vyama vidogo vya upinzani ulikokuwa na vyama vingi zaidi kuliko huu muungano wa vyama vinne, ulikuwa chini ya DP na SAU nao waliuzindua kwa kishindo ukawa unakabiliana na muungano wa vyama vya CHADEMA, TLP, CUF na NCCR. Kwa hiyo tukitegemea muungano tu, tutakatishwa tamaa na kujikatisha tamaa.


Asha

Asha, nilizungumzia Kenya, sikusema kuna makundi wawili, soma post yangu utaona nimeonesha walikuwa na ushirikiano (rainbow coalition mwanzo, pentagon). Vile vile nisemapo kuungana sina maana ndio mwanzo wa ushindi wa wapinzani, lakini ni mojawapo ya njia kuelekea kutengeneza mazingira ya ushindi. Mfano, wakati Zanziba ulipofanyika uchaguzi, na wagombea wa CUF wakawa wana pingamizi, CUF ilipiga kura iitwayo ya “Maruhani” wakati kulikuwa na vyama vya upinzani vilisimamisha wagombea. Kama vyama vya upinzani vinataka kuiondoa CCM madarakani, ilikuwa ni kuwaunga mkono wale wagombea na kuachana na maruhani.

Unapozungumzia Zanziba (Pemba) na Tarime ni tofauti na maeneo mengine, kuna maeneo watu wameshaamka, hata uibe, utumie hila ni ngumu kubadili matokeo. Lakini kuna sehemu watu wanamwamko mdogo, hupiga kura tu, baada ya hapo basi. Ila Tarime na Pemba wakipiga kura husubiri na matokeo mpaka kieleweke.

Sasa ninapozungumzia muungano sio katika uchaguzi tu, bali ni katika kudai mambo muhimu yatakayozifanya japo chaguzi zetu ziwe huru. Mfano hawa jamaa wanatakiwa kushirikiana (kuungana) kudai katiba ili kuanzia hapo tupate tume huru. Haiwezekani tume iliyochaguliwa na chama kilichopo madarakani ikatenda haki kwa vyama vingine.

CUF kufanya mjadala na CCM kuna haki vyama vingine kushiriki, manake na vyama vingine vilishiriki huo uchaguzi sema tu vilipata kura chache za ubunge. Maamuzi ya CUF na CCM kwanini yawe ni maamuzi ya wote (Chadema, jahazi asilia, SAU, UDP nk). Hivyo vyama vingine vyenye nguvu hasa vilivyosimamisha wagombea Zanziba vilipaswa kushiriki. Na hili CUF ndio ilitakiwa ilipigie debe, lakini haikukubali. Umoja siku zote ni nguvu.
 
Utakufa nacho kijiba cha roho

Wewe sikushangai sana kwa sababu najua wewe ni mtu mwenye akili nyingi sana na mjanja halafu ni baridi (ufisiadi kwako wewe poa tu si ndiyo ulimuinua baba yako kule mbeya at least umefaidika nao). Ninae mshangaa sana ni huyo aliyekupa thanks, naomba umpe ujumbe huu. Anatakiwa achague kuwa moto au baridi lakini akiendelea kutaka vyote na kuwa vuvguvugu kama alivyo sasa siku moja atatapikwa.
 
Mama Asha,
Operesheni Sangara ifuatiwe na kuipanga upya safu ya VIONGOZI wenu WAKUU. Kuna watu mle wanaweza kuleta mabadiliko ya Uongozi wa Nchi hii.
 
Je, ni ukweli kama uamuzi wa Tume kumwondoa Shitambala baada ya kuwasilisha hii rufaa yake Mbeya vijijini: Kampeni, uchaguzi na yatokanayo - Page 40 - JamiiForums.com

umechangia kufanya watu wasusie kwenda kupiga kura?

- Ukishindwa kubali ili urudi nyuma na kusoma instructions upya uweze kushinda next time, hapa CCM imeshinda hands down hakuna sababu ya visingizio visivyo na kichwa wala miguu na hili jimbo lilikuwa la CCM anyways sasa hii sizitaki mbichi hizi zinatoka wapi?

- Unataka kusema nini mkuu, kuwa Nyaulawa RIP, aliposhinda wananchi walisusia uchgauzi uliopita? Sasa cheki hapa chini vipi na huku Arusha, wananchi walisusia uchaguzi?


CHADEMA yashindwa vibaya

--------------------------------------------------------------------------------

Chama cha demokrasia na maendeleo kimeshindwa vibaya katika uchaguzi wa udiwani kati ya kati mjini Arusha.
Katika uchaguzi huo CCm ilipata ushindi mkubwa wa zaidi ya 68% uku CHADEMA ikiambulia 22%.CHADEMA ilitumia nguvu kubwa katika uchaguzi huo,mwenyekiti wa CHADEMA F Mbowe alitumia siku tatu za mwisho kumpigia debe mgombea wake Bwana Simba kitu ambacho kiliwashangaza wakazi wa jiji la Arusha hasa ikizingatiwa uchaguzi ulikuwa ni kata tu
.
 
Mama Asha,
Operesheni Sangara ifuatiwe na kuipanga upya safu ya VIONGOZI wenu WAKUU. Kuna watu mle wanaweza kuleta mabadiliko ya Uongozi wa Nchi hii.

Si walisema mwaka huu wanafanya uchaguzi?!? Lets wait and see watafanya nini katika uchaguzi huo
 
Mama Asha,
Operesheni Sangara ifuatiwe na kuipanga upya safu ya VIONGOZI wenu WAKUU. Kuna watu mle wanaweza kuleta mabadiliko ya Uongozi wa Nchi hii.

Baba KadiMwitu

Sangara inaweka safu mpya za uongozi kwenye matawi, inajenga chama ngazi ya chini kabisa vijijini na mitaani.

Safu mpya ya kitaifa itapatikana kwenye mkutano mkuu ambao tumeambiwa unafanyika mwezi Juni.

Karibu ugombee, mi mwenzio nitagombea ujumbe wa mkutano mkuu kutoka Zanzibar

Asha
 
Back
Top Bottom