Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 57,248
- 90,318
1. Malengo yasiyo na uhalisia
Nimemsikiliza Rostam Aziz anasema tume ya kutengeneza dira walikuwa wanalenga Tanzania iwe na ukubwa wa uchumi(GDP) kati ya $bilion 500-700, wao sekta binafsi wakina Rostam wakapendekeza malengo iwe GDP $Trilion 1 ! Haya ni malengo yasiyo na uhalisia, kwa miaka 25 ijayo uchumi wa Tanzania kukua mara 12 zaidi ya sasa unahitaji miujiza au akili kama za Wazungu na Tiger economies. Uchumi wa $Trilioni 1 unazungumzia uchumi kama wa Saudi Arabia na Netherlands.
2. Kutoweka kipaumbele katika kupunguza masikini
Inaonekana walioitengeneza hii dira ni wale watu walioganda na wanaoamini zaidi katika "trickle down economics" , mkakati wa uchumi unaoamini zaidi kwamba ukuaji mkubwa wa uchumi siku zote utajitafsiri katika maisha mazuri kwa raia wengi. Huu ni mkakati ambao kwa sasa unaonekana kufeli vibaya sana katika nchi kadhaa zenye uchumi mkubwa . Ukuaji mkubwa wa uchumi hauna maana sana kama sio jumuishi na wenye kuleta nafuu ya maisha kwa raia wengi. Nchi nyingi duniani zenye uchumi mkubwa hadi za ulimwengu wa kwanza kwa sasa nyingi raia wanapoteza imani juu ya serikali zao kwa sababu uchumi unamilikiwa na watu wachache sana huku mamilioni wakiishi maisha ya kuteseka.
3. Utengenezaji wa Dira kuongozwa na mwalimu wa saikolojia na elimu.
Dira ya Taifa ilitakiwa iongozwe na mwanauchumi nguli, hili halitakiwi kuwa suala la mjadala au kubishaniwa.
Nimemsikiliza Rostam Aziz anasema tume ya kutengeneza dira walikuwa wanalenga Tanzania iwe na ukubwa wa uchumi(GDP) kati ya $bilion 500-700, wao sekta binafsi wakina Rostam wakapendekeza malengo iwe GDP $Trilion 1 ! Haya ni malengo yasiyo na uhalisia, kwa miaka 25 ijayo uchumi wa Tanzania kukua mara 12 zaidi ya sasa unahitaji miujiza au akili kama za Wazungu na Tiger economies. Uchumi wa $Trilioni 1 unazungumzia uchumi kama wa Saudi Arabia na Netherlands.
2. Kutoweka kipaumbele katika kupunguza masikini
Inaonekana walioitengeneza hii dira ni wale watu walioganda na wanaoamini zaidi katika "trickle down economics" , mkakati wa uchumi unaoamini zaidi kwamba ukuaji mkubwa wa uchumi siku zote utajitafsiri katika maisha mazuri kwa raia wengi. Huu ni mkakati ambao kwa sasa unaonekana kufeli vibaya sana katika nchi kadhaa zenye uchumi mkubwa . Ukuaji mkubwa wa uchumi hauna maana sana kama sio jumuishi na wenye kuleta nafuu ya maisha kwa raia wengi. Nchi nyingi duniani zenye uchumi mkubwa hadi za ulimwengu wa kwanza kwa sasa nyingi raia wanapoteza imani juu ya serikali zao kwa sababu uchumi unamilikiwa na watu wachache sana huku mamilioni wakiishi maisha ya kuteseka.
3. Utengenezaji wa Dira kuongozwa na mwalimu wa saikolojia na elimu.
Dira ya Taifa ilitakiwa iongozwe na mwanauchumi nguli, hili halitakiwi kuwa suala la mjadala au kubishaniwa.