nandembako
JF-Expert Member
- Jun 16, 2013
- 654
- 523
Upo kimya hutaki makelele anatokea mtu anakuuliza mbona upo kimya?....mjibu hapana sipo kimya nipo hapa hapa....
Umekaa na mtu ukajamba alafu anakuuliza, umejamba? unamjibu hapana, hiyo ni chorus tu...
Maswali ya kijinga na majibu ya hasira;
1. Mtu anakuona umejilaza na macho umefunga anakuuliza umelala?..... Hapana najaribu kufa.
2. Mvua inanyesha halafu unatoka nje kisha mtu anakuuliza unakwenda na hii mvua?..... Hapana nitakwenda na inayofuata.
3. Rafiki yako anapokupigia simu yako ya mezani afu anakuuliza uko wapi?..... Niko kanisani naombewa.
4. Wanakuona umelowa ukitokea bafuni wanakuuliza umetoka kuoga?... . Hapana nimeanguka kwenye bakuli la choo.
5. Umesimama nje ya lift kwenye jengo la sakafu ya chini kisha unaulizwa unapanda juu?..... Hapana ninasubiri chumba changu kije kinichukue hapa chini.
6. Unamnunulia mkeo maua anakuuliza hayo ni maua?..... Hapana mke wangu, ni karoti.
7. Uko kwenye foleni ya kulipa tiketi ya kuingia uwanjani kucheki mpira, rafiki yako anakuuliza na wewe unaenda kuangalia mpira?..... Nimekuja kulipa ada ya shule.
8. Ongezea na yako
mmekaa nje kwenye mkeka saa 12 jion mnafuturu mtu anapita anawauliza mnafuturu? mjibu hapana tunalegeza swaumu.
Upo kwenye folen ya kupata kitambulisho cha mpiga kura toka asubuhi hujafikiwa tuu anakuja mtu anakuuliza hujapata kitambulisho tuu....
Nimepata hapa kwenye folen nauza sura
Nitakutandika bakora hata kama ni mtu mzima!....LolMmepewa assignment ya group,siku ya Presentation umesogea mbele ili uliwakilishe group Lecturer anauliza Umekuja kupresent?....Hapana nimekuja kucheza mziki wa Awilo
Nitakutandika bakora hata kama ni mtu mzima!....Lol
Mweeee!!!Ni usiku wa manane mtu anapiga simu alafu anakuuliza umelala?.... jibu hapana niko nje naota jua.