Julius Nyerere tangu aazimie kuhamia Dodoma 1966 na kupitisha Azimio la Bunge 1973 mpaka anaondoka Madarakani 1985 hakuweza kuhamisha hata Wizara moja. Aliwahi kujaribu kuhamisha Wizara ya Mambo ya Nje lakini alipopelekewa Mchanganuo wa Bajeti yake aliufyata.
Kigezo pekee cha kupanga Dodoma kuwa Makao Makuu ilikuwa ukati kati wake pekee hawakutazama Ujangwa wala kupitiwa kwake na Bonde la Ufa ambacho ni kikwazo kikuu kwa ujenzi Mkubwa mkubwa.
Kwa Hili Magu kaharakisha kama alivyokurupuka MwlNyerere.
Angalau Mzee Mwinyi alijaribu kuukuza Mji wa Dodoma kwa kuifanya kuwa Tax havens ambapo ukiwekeza na kuzalisha Dodoma unalipa nusu ya kodi na hata utility ya Umeme na maji iliazimiwa ilipwe nusu bei japo utekelezaji wake nao haukufanikiwa.
Haikuandikwa Mbinguni kuwa Dodoma ni Makao Makuu ya Tanzania, ni utashi tu wa Mtu mmoja kwa tamaa zake za kumfurahisha Mgogo wake leo inaligharimu Taifa na watu wake!
Mkapa alithubutu kibusara kwa kulipeleka Bunge nako hapakuchangamka.
Jakaya alijaribu kupeleka Udom nako hapakuchangamka.
Dodoma ipo kuzalisha Omba omba tu na Wagonjwa wa Macho Nyerere kwa utashi wake kaigeuza Washington ya Tanzania ikamshinda