Maswahibu yanayomkuta Halima Mdee yalinikuta na Mimi, tofauti tu yeye ni Senior Mimi nilikuwa Junior

Hitimisho:

Tulitembea hadi ofisi ya Finance Mananger huku yeye akiwa katangulia - alikuwa mzee wa hekima wa age kama 55 - 60 hivi, tuliingia tukaketi pia baada ya muda Operation Manager na yeye akaingia ndani, hatukuwa na wasiwasi tena maana kama msahama tulishapata toka CEO haya yanayofuata si ya hatari tena.

Finance akaanza - Kama mlivyosikia kwa CEO wetu, leo asubuhi kabla hamjafika tulikuwa na kikao cha uongozi kwa hiyo haya yote ntakayoyasema tulishayafanyia maamuzi tayari ila tulisubiri mfike ili tuyabariki.. sasa sitaki kurudia hayo yote yaliyotokea kwenu tangu mwanzo hapana, waungwana na wasomi huwa wana focus yaliyo mbele yao na hii ndiyo kazi yangu mimi na mwenzangu hapa.

Kwanza kabisa PONGEZI nyingi sana nazitoa kwenu toka kwa kampuni yetu kwa kutuletea mteja ambaye kwa tetesi tulizopata alikuwa afunge mkataba na kampuni nyingine siku chache kabla ya ninyi kufanya mazungumzo na yeye, ila kwa weredi wenu mmeweza kumshawishi na mmetuletea project kubwa kama hii Big Up kwenu. Muda huo nilikuwa naendeea kuchekea tumboni...

Akaendelea Pili kampuni yetu pamoja na hayo yote imeamuwa kuwazawaidia ajira MPYA...... kwa muda mrefu tulikuwa tuna mpango wa kufungua tawi letu Arusha, ila tulikuwa tunakwamba kidogo kwa hiyo tukawa tunaendelea kuwatumia mawakala - sasa napenda kuwajulisha kwamba mmechaguliwa ninyi wawili kwenda kufungua tawi hilo ambalo kwa kuanza litashughulika na kazi za Sales / Marketing pamoja na Technical na viongozi mtakuwa ni ninyi.

Akanitaja mimi ( nitakuwa Head wa Marketing / Sales) na mwenzangu atakuwa upande wa Technical. Kwa sababu position hizi ni kubwa na ninyi hamna uzoefu mkubwa basi mtafanya orientation kwa wiki mbili na mabosi wenu wa zamani yaani Operation Manager na Sales Manager na mkiwa huko Arusha mtatimiza majukumu yenu na kuriport moja kwa moja kwa CEO. Kwa hiyo kwa wiki mbili hizi mtafanya kazi hapa bega kwa bega na hawa watu ili mjue nini majukumu yenu mapya... Sambamba na hilo kikao cha leo kimeamua kuwapa 5% ya thamani ya projet nzima kama asante kwenu.

Muda huo nilibakia nimeduwaa siamini kinachoendelea pale, jamaa yangu ndiyo kabisaa alikuwa mbali, nilishtuka wakati anasema " I think your comfortable with these positions in front of you right? nikashtuka kidogo nikasema Yes, na mwenzangu Yes.

Operation Manager naye akasema kuwa kwa wiki hizi mbili zijazo tutafanya kazi naye pamoja na yule wa Sales (Building capacity) kabla hatujasafiri kwenda kwenye majukumu mapya.. Pia pamoja ya yeye tutasimalia hii Project nzima kuhakikisha inafanya kazi kama ilivyotazamiawa. Walisimama wote wakatupa hage la nguvu la Hongera na kututakia mafanikio mema... Tulisimama na kuondoka, ili kesho yake tuanze rasmi majukumu hayo mapya ya orientation.

Tulitoka, wakati natoka nilihisi miguu nyepesi sana, yaani siamini kama kweli yametukuta haya, tulifika reception tukaaga - dada aka smie na kutumbia Hongera... tulitabasabu sababu tunamjua. Tulifika nje ya office pale wawili wote tuliangaliana na kukumbatiana wa furaha kubwa, tukaagana ili tukapumzike baada ya kazi ngumu ya siku tatu mfululizo. Nilifika nyumbani nilipiga magoti kumshukuru Mungu wangu kama kawaida yangu kwa yote mema aliyonitendea kwa kutujaza Hekima mpaka kumelimaliza jambo letu salama.

Tulianza orientaion yetu vizuri, tukawa tunaingia kwenye Management meeting..., kule tukaanza kujua na kujadili future focus ya kampuni, financial, Sales na Technical strategies etc... Baada ya wiki mbili tulipata ile 5% yetu - pesa nyingii sana... tuliaga na kwenda Arusha kuanza kazi. Tulifanya kazi yetu vizuri kule Arusha huku tukireport moja kwa moja kwa CEO, na huko ndipo nikakomaa kwenye idara zote za mauzo na ufundi - pamoja na mwenzangu tukajifunza kufuata MISINGI ya kazi - Taratibu zilizopo na kutii mamlaka na kufuata itifaki.

Poleni kina Mdee, mimi nilivuka kwa style hii - ninyi nafikiri bado mna nafasi kubwa ya kusamehewa kama kweli mlikuwa na dhamira ya kweli ya KUJENGA badala ya KUBOMOA, Sisi mlango ulifungwa ila ukafunguliwa tena kwa stle hii ya kipekee - bado naamini mna NAFASI.


-------------------------------- END ---------------------------------
Congrats mkuu na usimuliaji mzuri sana.
Be blessed.
 
Maswahibu yanayomkuta Halima Mdee yalinikuta na mimi, tofauti tu yeye ni Senior na mimi nilikuwa Junior. (Soma kisa changu hiki cha ukweli kwa ufupi kabisa)

Sehemu ya Kwanza.

Baada tu ya kuhitimu chuo nje ya nchi miaka hiyo ya juzi kati nilirudi nchini na kupata kazi bila kuchelewa katika kampuni binafsi ya Tehama (Information Technology) katika idara ya Ufundi ( Technical Department)

Baada tu ya kukamilisha miezi sita ya uangalizi kazini na kupata barua rasmi ya kuajiriwa kuna siku katika kutimiza majukumu yangu nikakutana na mteja (CEO wa kampuni moja) akapenda sana teknolojia yetu na kutaka kuitumia kwenye kampuni yake, akanipa miadi niende ofisini kwake ili nimweleze vizuri namna Teknolojia yetu inavyofanya kazi.

Nilirudi ofisini kwetu nilimshirikisha mwenzangu tulie ajiriwa naye siku moja ili tuwe wawili tukasaidiane kumdadavulia nondo CEO huyo wa kampuni kubwa ( Ipo hadi leo); Mwenzangu akakubali. Kesho yake asubuhi tulifika ofisini kwa CEO huyo tukapokelewa vizuri na kupelekwa kwa Katibu muhtasi wake ambaye naye akatupeleka hadi ofisini kwa bosi wake. Ofisi kubwa nzuri ambayo sikuwahi kufikiri naweza kuingia, basi tukamweleza vizuri mno namna Teknolojia yetu inavvyofanya kazi na namna anaweza kuitumia, maana alikuwa na office Tanzania, Rwanda, Kenya, Uganda na Burundi. Akatuambia amepanga kutumia kama dola laki mbili kufanikisha hilo ambapo ni kama mil 460 na ushee kwa hivi kwa sasa, akatuambia tukacheki na CEO wetu ama muhusika yeyote ofisini kwetu ili aje kupanga hilo deal.

Tuliagana, akatutoa ofisini kwake hadi kwa katibu muhtasi wake na kumwambia atuangalie.... nanukuuu " Laura , Please take care of these young boys.." akafunga mlango wake akatuacha sisi na dada Laura... huku tukitaka kutoka dada Laura akafungua fridge akatupatia soda moja moja kila mtu kwa chaguo lake na tulivyomaliza akatupatia barua, kila moja ya kwake... tukashukuru tukaondoka..huku atuamini kama haya yanayotokea ni yetu sisi ama tunaota.

Tulipofika nje tuliangaliana na kuangusha kutabasamu kali kwa pamoja, nilifungua barua yangu aisee nikakuta wekundu kadhaa wamejipanga halikadhalika na rafiki yangu na yeye hivyo hivyo.... nikajua fikakwamba sasa maisha yanakwenda kutunyookea, tunapeleka dili la dola laki mbili ofisini? kweli?.... Mungu si athumani aisee.


Sehemu ya Pili

Tulipofika ofisini moja kwa moja kwa CEO wa kampuni yetu uzuri tulimkuta- ilikuwa huwezi kuingia hovyo hovyo ila tuliweza kwa sababu CEO huyo alikuwa mtu wa kujichanganya na staff hasa vijana - tulimwomba masijala bayana wake na akaturuhusu, tukagonga tukaingia tukamwambia kuhusu deal hilo - alifurahi saana na kutuambia muda wowote tumlete mteja huyo.

Tulimpigia mteja wetu na kumwambia CEO kashakubali hivyo kesho saa tatu afike ofisini kwa ajili ya mazungumzo - kweli Kesho yake asubuhi akafika ofisini kwetu akiwa pale reception akanipigia simu, nikiwa na rafiki yangu tukashuka chini tukampokea mteja wetu na kwenda moja kwa moja ofisini kwa CEO.

Tulifika ofisi ya Masijala Bayana alituashiria kwamba twende moja kwa moja maana bosi kubwa alikuwa anatusubiria....nikiwa nimetangulia nilifungua mlango na kukutanisha macho na CEO huku nikiachia tabasabu kubwa na yeye pia.... akatupokea wote watatu tukaketi - nilifanya utambulisho mfupi kwake na baadaye mteja wetu naye alitushukuru mimi na mwenzangu kwa ufafanuzi mzuri wa namna Techologia yetu inavyofanya kazi, CEO wetu alitushukuru sisi yaani mimi na mwenzangu, akatuomba tuondoke ili sasa yeye aongee vizuri na mwenyeji wake, tulisimama tukatabasamu na kutoka ofisini kwake.

Waliongea humo kwa takibani dk 20 hivi baadaye tukamwona mgeni wetu akitoka wakiwa na CEO na kutupungia sign na dole gumba ( ofisi ya CEO ipo pembeni mwa department ya Ufundi) baada ya kama dakika tatu nikapata message toka wa mteja wetu akisema " Mr X deal done) huku X akitaja jina langu.

Nilifurahi mno mno, nikamuonyesha message rafiki yangu, aisee nikajua sasa natoka kimaisha nikiwa ningali kijana mdogo ( wakati huo nilikuwa na miaka 26 tu) maana nilijua watu wa sales huwa wakileta wateja huwa wanapata 10% ya deal zima. Nikapiga hesabu za haraka haraka nikajua tuna kama 46m commission mbele yetu ... Mungu akupe nini...

ilipofika saa 11 kasoro siku hiyo hiyo kabla tu sijatoka ofisini nikapata email toka kwa Operation Manager kwamba ananiomba kuwa na mkutano naye kesho yake saa tatu kabla ya kwenda site. Nilikubali mwaliko huo kwa njia ya email. Nilimuuliza na mwenzangu na yeye akawa kapata pia email hiyo kwa hiyo tukajua kabisa kwamba sisi wote wawili tunahitajika kwa line Manager wetu hiyo saa tatu asubuhi kesho yake. hatukuwa na wasiwasi tukajua kabisa sasa mambo yameiva.... tukajua yawezekana tukaambiwa sisi ndiyo tusimamie hiyo installation yote Rwanda, Kenya, Burundi na Uganda..... nikahisi Mungu kafungua mbingu, neema imetushukia....

Sehemu ya Tatu.

Saa tatu kamili tuliingia chumba cha mkutano, tukamkuta Sales Manager pia yumo ndani, baada ya kusalimiana tukajulishwa kwamba OM (Operation Manager) kajuliswa na CEO kwamba tumepata potential customer ambaye anataka kutumia technologia yetu, yeye na Sales Manager wakatushukuru mno kwa hilo. Akaendelea kutuambia kwamba pamoja na asante hiyo ...

Akaendelea kutuambia kwamba pamoja na asante hiyo tumevunja itifaki ya kampuni kwa kupeleka deal moja kwa moja kwa CEO badala ya kupitia kwake OM ambaye ndiye line manage wetu.. hii tuliambiwa mapema wakati wa orientation yetu, kwa hiyo ni lazima tuchukuliwe hatua za kinidhamu huku akitoa ka kitabu hako ka Policies & Procedures na kutuambia tusome ukurasa wa kumi ambapo ulieleza endapo mfanyakazi ambaye si wa idara ya mauzo endapo atapata mteja ama biashara je afanyaje?.

Wakati huo Sales Manager alikuwa kimya akituangalia kwa makini, tuliambiwa kama tuna utetezi wowote tuuseme muda huo kabla hatujapewa adhabu yetu ingawa aligusia kwamba adhabu inaweza kufikia hata kufukuzwa kazi..

Sikuamini... sikuamini; Yaani kumbe kujiongeza kwangu kote kule nilidhani naisaidie kampuni yangu kumbe ndiyo nimeharibu kabisa.. sikuamini.. Chumba kilikuwa na AC kali ila tulianza kutoka jasho jembamba... kabla ya utetezi nilianza kulia huku nampigia magoti OP wangu, nikaishiwa nguvu nikaanguka kwenye kapeti - mwenzangu kichwa kikaangukia meza kimyaaaa.....

Nikasikia kwa mbali OP akisema you need to see the company secretary immediate after this...wakatoka wakatuacha - tulibakia pale conference kwa muda kama nusu saa, nikazinduka nikamshtua mwenzangu nikamwambia kaka jikaze huu ndiyo ukubwa, tayari tushaingia cha kike - wamesema tukamwone secretary pale chini hatuna namna... Kosa letu kubwa tunatuhumiwa nalo kujaribu kujipatia commission bila kufuata utaratibu... tume pindisha deal kwa makusudi ili tujipatie fedha huku tukijua kufanya hivyo ni kosa kubwa.

Tulitoka huko, baadhi ya staff wakitushangaa mno kulikoni?? maana hatuwashirikisha kwa lolote kwa hiyo hawakujua what is going on...
Tulifika pale reception, tukakuta barua tayari zilishachapwa na kusainiwa tayari kwamba kwa kosa tulilofanya hatuwezi kuvumilika hivyo sisi si wafanyakazi tena wa kampuni kuanzia muda huo - tutapewa mshahara wa mwezi mmoja kama sheria inavyotaka na tunatakiwa kukabidhi vitu vya office siku hiyo hiyo na kuondoka.

Aisee nilitamani nife kabisa, niliona maisha yangu hayana maana tena - nilifikiria je ntalipaje pango, nitakula nini? maisha magumu.. kikakabidhi vitu vyao nikachukua barua yangu ya kufukuzwa nikasepa - mshikaji wangu pia hivyo hivyo tukaondoka - kabla ya kuagana kituo cha basi tukapanga tukutane kesho getoni kwangu tupange nini cha kufanya......

Sehemu ya Nne

Jamaa yangu alifika asubuhi saa tatu, tulianza mjadala moja kwa moja - mjadala ulikuwa mgumu na fikirishi mno - Hoja mezani zilikuwa Je twenda kuomba msamaha au lah? Je kuna uhumimu gani au faida gani tutapata endapo tutaomba msamaha? Je ni hasara ama faida endpo hatutakwenda kuomba msamaha ? Je msamaha wenyewe ni wa kurejeshwa kazini ama ni wa kutusafisihia tu CV zetu zilizochafuka? Je ni nani tunakwenda kumwomba msamaha huo, ni CEO ama ni line manager wetu?

Tulivutana mno, mwenzangu alishauri tuachane nao na maisha yaendelee kwamba hakuna haja ya kumpigia magoti mwanadamu, sisi bado vijana na tuna future kubwa mbele yatu ukizingatia kozi tulizo soma zina uhitaji (market) kubwa. Mimi nani nilisimamia msimamo kwamba ni sawa anavyopendekeza ila umuhimu wa kusafisha majina yetu ni mkubwa mno kwa maana kokote tukakapokwenda tutaulizwa previous job reference, tumefanya kazi wapi na wale watu wanaotaka kutuajiri watahitaji kupata fununu juu ya tabia zetu na utendaji wetu wa kazi.

Mjadala ulikwenda hadi alasiri, tunasikia njaa tukaamua tutoke kwende pale Rose Garden, si mbali sababu wote tulikuwa tunaishi Sinza na kwa wakati huo kiwanja hicho kilikuwa ndiyo makutano ya hasa vijana kubadilishana mawazo huku walipata chakula... Tulikaa wenyewe tu ili tumalizie mjadala wetu na kabla ya siku kuisha tuwe na msimamo mmoja.

Baada ya chakula tuliendelea na mjadala huku tukigonga glass moja moja tukipeana matuamani ambayo ki ukweli hayakuwepo, mwishoni tukaafikiana twende tukaombe msamaha kwa CEO na si wa line Manager wetu sababu kuu kwamba yeye ndiye aliyelishughulikia jambo letu toka mwanzo - na msamaha tunaokwenda kuomba si wa kurudishwa kazini hapana ila tu ni wa kusafisha CV zetu ili tupate reference nzuri endapo zitahitajika na waajiri wengine. Hoja ya mwisho ilikuwa tunakwenda kwa CEO ofisini kwake ama nyumbani kwake? hapa napo tulivunata mno, kwa kauli moja tukaafikiana twenda nyumbani kwake badala ya ofisini - twende kama vijana wake..tuliona ni rahisi kumpigia magoti CEO kuliko line manager wetu. Tuliagana pale mida ya saa mbili usiku kila mmoja akienda getoni kwake kupumzika.

Sehemu ya Tano.

Kesho ikafika na jioni ya saa 11 mwenzangu alifika kwangu, tulipanga tuondoka mida hii ili walau tuwahi kufika kwa CEO mida ya saa 12 na nusu ama saa moja moja hivi - CEO alikuwa anaishi Upanga kwa hiyo tukaanza safari yetu toka sinza mida hiyo. Tulifika Upanga karibu na nyumbani kwake saa 12 kasoro, tukawa pale nje kwa mbali kidogo tukipiga soga ili tuhakikishe kafika then ndiyo twende. Kufika saa 12 unusu tulianza safari ya kwenda getini kwake, kuna walinzi pale lakini tukajipa matumaini hawawezi kutuzuia maana tutasema sisi ni wafanyakazi wa ofisini na tuna jambo la muhimu la binafsi la kumwambia (Personal issue).

Tulifika pale tukajieleza kwa mlizi, akatuambia tumsubiri huko huko nje .. alikwenda moja kwa moja ndani... sasa nikawa na na mawazo fikirishi kwamba hivi alimjibu hataki kuongea na sisi tutasemaje? ama akaja akatufokea mbele ya walinzi hawa? au akaamua kutuchukulia hatua kwamba tumekwenda kumsumbua nyumbani kwake? nikakumbuka wazo la mwenzengu kwamba tungeachana na haya mambo ya kuomba msamaha maana yanaweza kutuletea mambo mengine tena.

Wakati natafakari mara namuona CEO pamoja na mlinzi wanakuja main gate tulipokuwepo, aisee nikahisi sasa mbivu na mbichi ndiyo hiii - kwa sasa ningetumia jina la "Mwana kuli-find....." Kwa mbali tulijaribu kusoma sura ya CEO maana kwa mwanadamu unaweza kusoma sura ukajua lililomo moyoni kwako kabla....wakasonge karibu nasi......mwili wangu ni kama ulipata ganzi hivi..

Bila kuamini kilichotokea alipofika kama hatua tatu tu toka tulipokuwepo aliniitaja jina langu huku akitabasamu na kutukaribia, alitusalimia kwa tabasamu kubwa..huku aliweka mikono yake mabegani kwetu kulia na kushoto huku tukitembea kuelekea nyumbani kwake. Alitutambulisha kwa mkewe na watoto wake 2, Huyu CEO hakuna mzee hapana ni kijana tusema wa miaka 35 - 40 hivi nafikiri alipata cheo hiki kwa werevu wake alionao.

Alituomba tupate bites kidogo na drinks ila tulikataa tukamwambia tuna jambo kidogo tumekuja kushare na yeye na si wakaaji - lakini wapi alitushawishi hadi tukapata hizo bites na soft drinks... so wakati nataka kuanza kumweleza jambo letu lilolotupeka hapo yeye akadaikia akasema " I know what you want to tell me, please come to my office tomorrow morning 9 am", akakataa kata kata tusimwambie kitu bali tufike ofisini kwake hiyo kesho.

Tulimazia bites zetu na vinywaji na kisha tukaaga na kuondoka, alitusindikiza kadi nje, akamwambia dereva wake atufikishe hadi makwetu...akatuaga kwa kutumbia " Ok we meet tommorow" cheers!!

Ndani ya gari mawazo mengi, hiyo kesho anakwenda kutuambia nini ambacho asingetuambia hapa hapa, nikakumbuka tunakwenda tena kukutana na line manager wetu maana huwezi kuingia ofisini mule bila wao kujua. nikafiri namna wafanyakazi wenzetu wanakavyotuchukulia maana wote sasa washajua kwamba tumeshatimuliwa kazi. Mawazo haya yalinizunguka kwenye fikra zangu nafikiiri hata mwenzangu alikuwa akiwaza hivyo hivyo kwamba huenda tukawa tumelikorogoa zaidi kwenda kuaibika huko. Nikakumbua wazo na mwenzangu kwamba tungeamua kuachana na haya mambo ya msamaha tukajali maisha yetu.

Gari ikafika mitaa ya sinza tukashuka, tukamshukuru dereva - hapo tukaagana na mwenzangu pia ili sasa kesho tukutane ofisini kwa CEO saa tatu asubuhi... Kwangu usiku ulikuwa mfupi, sikutana asubuhi ifike mapema maana nilihofu ni nini kinakwenda kutokea hiyo kesho, wazo la kutokwenda tuliona halitakuwa na uungwana cha msingi twende tu tukajue ni nini hasa. Tulijua kwamba kama kufukuzwa tumefukuzwa sasa kinachokwenda kutokea yawezekana ikawa ni kudhalilishwa mbele ya staff wote wa kampuni.. Usingizi ulinipitia kama kipanga.. nafikiri kwa sababu ya uchovu wa mawazo..

Sehemu ya Sita.

Ndugu msomaji wangu wa kisa hiki, usiku wa deni huwa haukawi kucha, asubuhi ikafika, nikajua sasa leo ni leo, hitimisho la jambo letu limewadia, ni mawili moja tujisafishe kwa maana tusamehewe ili tuwe huru kwa tuhuma hizo ama tudhalilike zaidi tena mbele ya wafanyakazi wenzetu wa zamani.

Tulifika mapema pale ofisini, ila tukabana sehemu kwanza maana kuna kama ka-aibu furani hivi machoni mwetu - hatukutaka kukutana na staff wenzetu pale nje. Saa tatu kasoro dk tano tulifika pale ofisi ya mapokezi, dada ali kama shtuka hivi na kweli macho yalipogongana na yetu kukawa kama kuna kama jambo lilokuwa ndani yake kuhusu sisi - tulimsalimia na tukamwambia tuna miadi ya CEO - bila kuchelewa akasema habari hizo anazo kwa hiyo twende ofisini kwake kashafika...

Tulipita bila kuangalia kushoto na kulia hadi ofisi ya CEO, masijala alitupokea akatuambia tupite moja kwa moja - tulipofika kama kawaida alitupokea kwa tabasamu tukaketi... Akatuuliza kama tupo sawa, tukajibu ndiyo!! Mimi tayari nishaanza kupata wasiwasi moyoni kwamba leo ndiyo leo - mbivu na mbichi zinakwenda kujulikana.

Alinyenya simu yake ya mezani na kupiga, mara nikasikia anaita jina la yuel line Manger wetu wa zamani, akamwambia aje ofisini kwake.... Mungu wangu... Mwili wote ulikufa ganzi nikajiona mtu nisiye na bahati kabisa duniani - aibu hii yote kwa nini lakini nimeshawishika kuja huku? Mara Operation Manager akaingia ofisini na tabasamu lake kama la kejeli hivi.. (nilihisi), akatusalimia akaketi.

CEO akasema huku amemwangalia Operation Manger " As i discussed with you this morning, i think we agreed that these two boys......" Yaani alipofika pale nilitamani ardhi ifunguke nijifishe kwa aibu inayokuja mbele yetu... akaendeea " Tumewasamehe kwa yote yale waliyoyafanya sababu kubwa ya kuwasamehe ni vijana bado wadogo hawana experience ya maisha ya kazi - tunatakiwa kuwalinda na kuwajenga, ni wajibu wetu... akamalizia CEO huku akigekia kutuangalia sisi.. hapo nilishusha punzi kama nimejitua gunia la kokoto kichwani... akaendelea.. Tumefarijika sana kuwa mmejua kosa lenu na hii ndiyo kigezo kikuu tulichotumia kuwasamehe - kwamba yawezekana mlikuwa na nia nzuri mno na kampuni yenu lakini hamkufuata utaratibu, kwetu katika kampuni hii usipofuata utaratibu (Policies & Procedures) huwezi kuvumilika kabisa, hata uwe CEO kama mimi ni lazima utachukuliwa hatua tu - hakuna aliye juu ya Policies hakuna. (No one is above the polices ) akamalizia kwa lugha hiyo ya kimombo ambayo anaimudu mno.

Kwa hiyo tumewasamehe na kwa sasa mtakuwa na kikao kingine cha Operation Manager na Finance Manager baada ya hiki cha kwangu - nawatakia kazi njema. akamaliza huku akisimama kunipa mkono mimi na mwenzangu - Tulisimama tukaondoka ofisini kwake bila kuamini tulichokisikia toka kwake...

Hitimisho:

Tulitembea hadi ofisi ya Finance Mananger huku yeye akiwa katangulia - alikuwa mzee wa hekima wa age kama 55 - 60 hivi, tuliingia tukaketi pia baada ya muda Operation Manager na yeye akaingia ndani. Hatukuwa na wasiwasi tena maana kama ni msamaha tulishapata toka kwa CEO haya yanayofuata si ya hatari tena.

Finance akaanza - Kama mlivyosikia kwa CEO wetu, leo asubuhi kabla hamjafika tulikuwa na kikao cha uongozi kwa hiyo haya ntakayoyasema tulishayafanyika maamuzi ila tulisubiri mfike tu ili tuyabariki.. Sitaki kurudia hayo yote yaliyotokea kwenu hapana, waungwana na wasomi huwa wana focus yaliyo mbele yao na hii ndiyo kazi yangu mimi na Mwenzangu hapa.

Kwanza kabisa PONGEZI nyingi sana nazitoa kwenu toka kwa kampuni yetu kwa kutuetea mteja ambaye kwa tetesi tulizopata alikuwa afunge mkataba na kampuni nyingine siku chache kabla ya ninyi kufanya mazungumzo na yeye, ila kwa weredi wenu mmeweza kumshawishi na mmetuletea project kubwa sana. Muda huo nilikuwa naendeea kuchekea tumboni...

Akaendelea Pili kampuni yetu pamoja na hayo yote imeamuwa kuwazawaidia ajira MPYA...... kwa muda mrefu tulikuwa tuna mpango wa kufungua tawi letu Arusha, ila tulikuwa tunakwamba kidogo kwa hiyo kukawa tunaendelea kuwatumia mawakala - sasa napenda kuwajulisha kwamba Mmechaguliwa ninyi wawili kwenda kufungua tawi hilo ambalo kwa kuanza litashughulika na kazi sa Sales / Marketing pamoja na Technical na viongozi mtakuwa ni ninyi.

Akanitaja mimi ( Nitakuwa Head wa Marketing / Sales) na mwenzangu atakuwa upande wa Technical. Kwa sababu position hizi ni kubwa na ninyi hamna uzoefu mkubwa basi mtafanya in-line na Operation Manager na Sales Manager wa Hapa Headquarters wakati wa kutimiza majukumu yenu huko. Kwa hiyo kwa wiki mbili hizi mtafanya kazi hapa bega kwa bega na hawa watu ili mjue nini majukumu yenu mapya... Sambamba na hilo kikao cha leo kimeamua kuwapa 5% ya thamani ya projet kama asante kwenu.

Muda huo nilibakia nimeduwaa siamini kinachoendelea pale, jamaa yangu ndiyo kabisaa alikuwa mbali, nilishtuka wakati anasema " I think your comfortable with these positions in front of you right? nikashtuka kidogo nikasema Yes, na Mwenzangu Yes.

Operation Manager naye akasema kuwa kwa wiki hizi mbili zijazo tutafanya kazi naye pamoja na yule wa Sales (Building capacity) kabla hatujasafiri kwenda kwenye majukumu mapya.. Pamoja ya yeye tukapewa jukumu la kusimamia hii project nzima. Walisimama wote wakatupa hage la nguvu la Hongera na kututakia mafanikio mema... Tulisimama na kuondoka, ili kesho yake tuanze rasmi majukumu hayo mapya ya orientation.

Tulitoka, wakati natoka nilihisi miguu nyepesi sana, yaani siamini kama kweli yametukuta haya, tulifika reception tukaaga - dada aka smie na kutumbia Hongera... tulitabasabu sababu tunamjua. Tulifika nje ya office pale wawili wote tuliangaliana na kukumbatiana wa furaha kubwa, tukaagana ili tukapumzike baada ya kazi ngumu ya siku tatu mfululizo. Nilifika nyumbani nilipiga magoti kumshukuru Mungu wangu kama kawaida yangu kwa yote mema aliyonitendea kwa kutujaza Hekima mpaka kumelimaliza jambo letu salama.

Tulianza orientaion yetu vizuri, tukawa tunaingia kwenye Management meeting..., kule tukaanza kujua na kujadili future focus ya kampuni, financial, Sales na Technical strategies etc... Baada ya wiki mbili tulipata ile 5% yetu - pesa nyingii sana... tuliaga na kwenda Arusha kuanza kazi. Tulifanya kazi yetu vizuri kule Arusha huku tukireport moja kwa moja kwa CEO, na huko ndipo nikakomaa kwenye idara zote za mauzo na ufundi - pamoja na mwenzangu tukajifunza kufuata MISINGI ya kazi - Taratibu zilizopo na kutii mamlaka na kufuata itifaki.

Poleni kina Mdee, mimi nilivuka kwa style hii - ninyi nafikiri bado mna nafasi kubwa ya kusamehewa kama kweli mlikuwa na dhamira ya kweli ya KUJENGA badala ya KUBOMOA, Sisi mlango ulifungwa ila ukafunguliwa tena kwa stle hii ya kipekee - bado naamini mna NAFASI.


-------------------------------- END ---------------------------------
Aiseeeee nimefarijika kuona story imekua na Happy Ending,

Nimejifunza pakubwa, Ahsante sana Bro.
 
Story nzuri sana, Ila kwenye uandishi hitimisho huwa ni samarized ya kile ulichokisema tangu mwanzo na si kuendelea na story, ndiyo nijuavyo Mimi
 
Wiki ya juzi alitrend Halima Mdee na wenzake.
Wiki Jana alitrend aliyenunua gari ya milioni 460
Wiki hii anaye trend Ni kijana mmoja mwenye mikosi lukuki aliyeshindwa kuapa. Just imagine kusoma kiswahili.
Yajuwe maajabu ya Jimbo la Kilwa alikotoka Mhe. Ndulane (Mb)

Jimbo aliloshinda Mhe.
Ndulane lina sifa zake 3 za ziada;
1. Mgombea mmoja alishinda kura za maoni CCM alipitiliza na Gari hadi Baharini hadi leo hajaonekana.

2. Mgombea mwingine alishinda Ubunge lakini hakuliona Bunge hadi amefariki baada ya kupigwa upofu.

3. Mhe. Ndulane ameshinda kupitia CCM lakini alikuwa mshindi wa 3 kwenye kura za maoni.

4. Gari zote alizotumia ndulane zilinock Engine mpaka akaanza kutumia pikipiki....!
 
Hahaha kwa hiyo CEO akasema "Laura take care of THIS young boys" au siyo?

Na nyinyi mlikua wawili? Halafu ni "... THIS young boys"
....Dah, Mkuu! Yaani katika Story yoote we we umeona hili kosa tu ambalo inawezekana CEO alisema 'These' lakini labda mleta mada alisikia 'This'? Yaani katika Story nzima we we umeona hili Kosa dogo tu LA Kiufundi na hukujifunza chochote kikubwa Mkuu??? Dah!
 
....Dah, Mkuu! Yaani katika Story yoote we we umeona hili kosa tu ambalo inawezekana CEO alisema 'These' lakini labda mleta mada alisikia 'This'? Yaani katika Story nzima we we umeona hili Kosa dogo tu LA Kiufundi na hukujifunza chochote kikubwa Mkuu??? Dah!
Mzee wakati naandika alikua amesema stori itaendelea.

Yaani wewe kama kuna kitu umejifunza ni umejifunza baada ya stori kuendelea muda huo nilishaandika hiyo koment na sikurudi tena mpaka ulivyoniquote.
 
Back
Top Bottom