Mimi naona dunia iachane na mfumo dume na rasmi 50/50 ishike hatamu

Jadda

JF-Expert Member
May 20, 2019
29,327
83,771
Ndio, kuna msemo unasema "with great authority comes great responsibility" yani kila mamlaka makubwa huambatana na majukumu makubwa, lakini jambo la kushangaza ni kwamba wanaume wengi hasa wa kiafrika wanayataka hayo mamlaka tu ila majukumu hawayataki

Mimi naona ifike pahala dunia iachane rasmi na mfumo dume na haki sawa ishike hatamu, kwa sababu wanaume hawataki tena majukumu hivyo hata hayo mamlaka hayawafai, wanaume wengi hawataki haki sawa ila wanataka majukumu sawa tena ikibidi mwanamke ndio afanye zaidi ya mwanaume

MImi naona kusiwe tena na mgawanyo wa majukumu yani hata kazi za nyumbani zifanywe na wote kama ambavyo kutafuta pesa limekuwa ni jukumu la wote, majukumu ya mwanamke yabaki yale ya asili na ya kimaumbile tu ambayo ni kubeba ujauzito, kuzaa na kunyonyesha, hayo tu ndio ambayo mwanaume hawezi kuyafanya ila majukumu mengine yote ya nyumbani kama kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba, kulea watoto tangu wakiwa wachanga mfano kuwasafisha, kuwauguza wakiumwa, nk yafanywe na wote kwa usawa kabisa

Na vile vile kwa mfano mume akiweka laki mezani na mke naye aweke laki mezani mahitaji yote ya nyumbani wanunue kwa usawa bills zote walipe kwa usawa, na watoto wao wawahudumie kwa usawa ikiwemo kuwalipia ada na mahitaji yao mengine yote kwa usawa, hiyo ndio maana halisi ya 50 50 siyo mmoja anamtegea mwenzie eti mtu anataka pesa mtafute wote na bills mlipe wote, ila kazi za nyumbani na kulea watoto afanye mmoja na bado huyo mmoja amtii mwenzie na amlee kama anavyowalea watoto wake, what kind of cockamamie logic is this

Na jambo jingine naona pia tuachane na suala la mwanaume kumtawala mwanamke kila mtu ajitawale mwenyewe kusiwe na habari za kichwa cha familia, yani hakuna tena kusema kwamba mwanamke anatakiwa amtii mumewe kila mtu awe na maamuzi juu ya maisha yake mwenyewe, kusiwe na wa kumuongoza mwenzake na pia kusiwe na habari za kuoa wala kuolewa tena bali iwe ni kuoana

Mnawalaumu wanawake kuwa wanadai haki sawa halafu hawataki majukumu lakini mnasahau kwamba sababu ya wao kukataa hayo majukumu ni kwa sababu mnataka wafanye yale ya kwenu tu, ila ya kwao bado mmewaachia wenyewe hamtaki kuyafanya yani huwezi kumuambia mwanamke ajitafutie pesa zake na akusaidie majukumu, halafu hapo hapo bado unataka huyo mwanamke akufanyie majukumu ya nyumbani na bado akupe heshima na utii

Kwanza hapo huyo mke anakuwa siyo msaidizi tena bali ni kama business partner tu hivyo ondoa kichwani suala la kumlazimisha akutii, hivi mnadhani mwanamke aliambiwa amtii mwanaume kwa misingi gani kama siyo kuhudumiwa maana huwezi kukitawala kiumbe usichokihudumia, hakuna binadamu mwenye akili timamu anayefurahia kutawaliwa na binadamu mwenzie asiyewajibika kwa lolote juu yake na kiuhalisia ukitoa huduma zinazohusisha pesa hakuna wajibu mwingine mwanaume alionao juu ya mwanamke

Kama ikiwa mtoto anamtii mzazi wake kwa sababu amemzaa na amemlea, watu wa dini wanaitii miungu yao kwa sababu wanaamini imewaumba na inawapa uhai, je mwanamke anapaswa amtii mumewe kwa sababu gani, tena hata mtoto mwenyewe akishatoka kwao akaanza kujitegemea kinachobaki kwa mzazi wake ni ile heshima tu kuwa amemzaa, lakini huyo mzazi anakuwa hana mamlaka tena ya kumpangia mtoto maisha yake mfano afanye kazi gani au arudi nyumbani muda gani kwa sababu hamhudumii tena

Sasa inashangaza pale mwanaume anapotaka mkewe atafute pesa wasaidiane maisha kwa kisingizio kwamba mke naye ana mikono miwili na miguu miwili, ila huyo huyo mwanaume haoni ajabu kumtawala huyo mke mwenye mikono miwili na miguu miwili kama yeye, yani imefikia hatua wanaume wanaona uchungu kugawana mali na wake zao na wengine ndio kabisa hawataki kuoa kwa kisingizio kwamba eti wakishafanikiwa wake zao watadai talaka ili wagawane mali

Yani hawaconsider tena yale majukumu yote ambayo wake zao wanawafanyia pamoja na utii ambao wake zao wanawapa, siku hizi wanadai kwamba kila mtu ajitafutie pesa zake na ikitokea wameachana kila mtu aondoke na chake, lakini cha kushangaza kwenye majukumu mengine hawasemi kila mtu afanye kwa usawa na kwenye suala la mamlaka hawasemi kila mtu ajitawale mwenyewe

Wale waumini wa ukristo hasa wanaume kama mmeamua kufuata maandiko basi fuateni yote, na kama mmeamua kuyapuuzia basi yapuuzieni yote msichague yale yanayowanufaisha ninyi tu halafu mengine mnajifanya hamyaoni, kwa sababu maandiko yanasema mume ndio atakula kwa jasho na si mke, halafu mbele ndio yanaendelea kwamba mwanaume atamtawala mwanamke, yule mke mnayemuota wa Mithali 31 yalikuwa mawazo binafsi ya mfalme Suleiman na si maagizo ya muumba

Hivo basi ifike pahala wanaume mchague moja kati ya mwanamke mfanyakazi/mfanyabiashara au mama wa nyumbani, na aina yoyote utakayochagua hapo lazima ukubaliane na sifa zinazoambatana na aina hiyo ya mwanamke siyo unachagua mfanyakazi/mfanyabiashara mnasaidiana majukumu, halafu hapo hapo unataka awe kama mama wa nyumbani au unachagua mama wa nyumbani halafu hutaki kumhudumia unaanza kumuona golikipa
 
........Kwanza hapo huyo mke anakuwa siyo msaidizi tena bali ni kama business partner tu hivyo ondoa kichwani suala la kumlazimisha akutii, hivi mnadhani mwanamke aliambiwa amtii mwanaume kwa misingi gani kama siyo kuhudumiwa maana huwezi kukitawala kiumbe usichokihudumia, hakuna binadamu mwenye akili timamu anayefurahia kutawaliwa na binadamu mwenzie asiyewajibika kwa lolote juu yake na kiuhalisia ukitoa huduma zinazohusisha pesa hakuna wajibu mwingine mwanaume alionao juu ya mwanamke.......
 
Unayotaka hayawi, kwenye hili tutaendelea kuwa wakali kama Konyagi ya malawi
Hahaha we mzee wa vina hilo ndiyo suluhisho la kupunguza vilio vya wanaume kuhusu wanawake, lazima tuangalie tunakosea wapi siyo kila kitu tunakimbilia kuwatupia lawama wanawake, ni lazima tukubaliane na hali halisi vinginevyo tuendelee kulalamika tu hadi mwisho wa dahari
 
Iko hivi mwanamke mwenye pesa kukuzidi au mkalingana huyo kidume mwenzio, hapo ndani kuna njemba mbili, hapakaliki tena.

Mwanamke hapaswi kukuzidi kipato.

Mwanamke hapaswi kukuzidi elimu.

Mwanamke hapaswi kukuzidi umri.

Mwanaume ameumbwa kutii na sio kuheshimu, kuheshimu tunaheshimu mzazi tu labda, ila siwezi heshimu mwanaume mwenzangu. Ndio jeshini ukiona mwanaume anapewa adhabu na anafanya huo ni utii si heshima.

Mwanamke kaumbwa kuheshimu na kutii, amheshimu mumewe na kumtii.

Kwenye ndoa mwanamke apendwe, mwanaume aheshimiwe, hio ni asili huwezi badilisha.

Unachozungumza ni kama kusema wanaume na wanawake wote tufanane maumbile, wote tuwe na misambwanda, wote tubebe mimba, wote tuvae shimizi..

Wanawake hamuwezi haki sawa, mtaongea tu, lakini majukumu usawa kwa usawa na mwanaume yupo hamuwezi, mtaanza kutegea tu.

Mfumo dume uendelee, tena sasa hivi msiajiriwe kabisa mkae nyumbani.
 
Iko hivi mwanamke mwenye pesa kukuzidi au mkalingana huyo kidume mwenzio, hapo ndani kuna njemba mbili, hapakaliki tena.

Mwanamke hapaswi kukuzidi kipato.

Mwanamke hapaswi kukuzidi elimu.

Mwanamke hapaswi kukuzidi umri.

Mwanaume ameumbwa kutii sio kuheshimu, kuheshimu tunaheshimu mzazi tu labda, ila siwezi heshimu mwanaume mwenzangu. Ndio jeshini ukiona mwanaume anapewa adhabu na anafanya huo ni utii si heshima.

Mwanamke kaumbwa kuheshimu, amheshimu mumewe.

Kwenye ndoa mwanamke apendwe, mwanaume aheshimiwe, hio ni asili huwezi badilisha.

Unachozungumza ni kama kusema wanaume na wanawake wote tufanane maumbile, wote tuwe na misambwanda, wote tubebe mimba, wote tuvae shimizi..

Wanawake hamuwezi haki sawa, mtaongea tu, lakini majukumu usawa kwa usawa na mwanaume yupo hamuwezi, mtaanza kutegea tu.

Mfumo dume uendelee, tena sasa hivi msiajiriwe kabisa mkae nyumbani.
Mkuu nafikiri hayo ulitakiwa uwaambie wanaume wenzio kwamba wanaposema wanawake nao watafute pesa wasiwe ombaomba huwa wanamaanisha nini,

Ndio maana mwishoni nikamalizia kwa kusema lazima mwanaume achague mwanamke wa aina moja, kati ya hizo aina mbili na akubaliane na sifa za kila aina ya mwanamke, asilazimishe mwanamke wa aina fulani awe na sifa za mwanamke wa aina nyingine

Hapo kwenye suala la kutegea labda nikuulize swali hivi laiti kama tungeamua kuswitch majukumu kwa muda fulani, ya mwanaume afanye mwanamke na ya mwanamke afanye mwanaume unahisi ni nani atakuwa wa kwanza kusurrender, unaweza kulinganisha idadi ya wanawake wanaotafuta pesa na idadi ya wanaume wanaofanya kazi za nyumbani kila siku (achilia mbali wale wanaojifanya wanasaidia wake zao mara moja moja tena ni hadi waumwe)
 
Hayo yote katika sentensi moja ndiyo kile kichwa cha uzi pale juu mkuu
Sijajua usawa gani mnataka,mfano wewe binafsi,ushawahi kukosa Jambo lolote,nafasi,nyadhifa,au huduma kwasababu tu wewe Mwanamke??
Kama tatizo Hilo lipo basi sio Tanzania,Tanzania kuna rais Mwanamke,Spika Mwanamke..pia tuna mawazirii,wakurugenzi wanawake tangu enzi za Nyerere..turudi kwenye ngazi za familia
 
Iko hivi mwanamke mwenye pesa kukuzidi au mkalingana huyo kidume mwenzio, hapo ndani kuna njemba mbili, hapakaliki tena.

Mwanamke hapaswi kukuzidi kipato.

Mwanamke hapaswi kukuzidi elimu.

Mwanamke hapaswi kukuzidi umri.

Mwanaume ameumbwa kutii sio kuheshimu, kuheshimu tunaheshimu mzazi tu labda, ila siwezi heshimu mwanaume mwenzangu. Ndio jeshini ukiona mwanaume anapewa adhabu na anafanya huo ni utii si heshima.

Mwanamke kaumbwa kuheshimu, amheshimu mumewe.

Kwenye ndoa mwanamke apendwe, mwanaume aheshimiwe, hio ni asili huwezi badilisha.

Unachozungumza ni kama kusema wanaume na wanawake wote tufanane maumbile, wote tuwe na misambwanda, wote tubebe mimba, wote tuvae shimizi..

Wanawake hamuwezi haki sawa, mtaongea tu, lakini majukumu usawa kwa usawa na mwanaume yupo hamuwezi, mtaanza kutegea tu.

Mfumo dume uendelee, tena sasa hivi msiajiriwe kabisa mkae nyumbani.

......Mwanamke kaumbwa kuheshimu na kutii, mwanamke amheshimu mumewe na kumtii. Kwenye ndoa mwanamke apendwe, mwanaume aheshimiwe, hio ni asili huwezi badilisha......
 
Mkuu nafikiri hayo ulitakiwa uwaambie wanaume wenzio kwamba wanaposema wanawake nao watafute pesa wasiwe ombaomba huwa wanamaanisha nini,

Ndio maana mwishoni nikamalizia kwa kusema lazima mwanaume achague mwanamke wa aina moja, kati ya hizo aina mbili na akubaliane na sifa za kila aina ya mwanamke, asilazimishe mwanamke wa aina fulani awe na sifa za mwanamke wa aina nyingine

Hapo kwenye suala la kutegea labda nikuulize swali hivi laiti kama tungeamua kuswitch majukumu kwa muda fulani, ya mwanaume afanye mwanamke na ya mwanamke afanye mwanaume unahisi ni nani atakuwa wa kwanza kusurrender, unaweza kulinganisha idadi ya wanawake wanaotafuta pesa na idadi ya wanaume wanaofanya kazi za nyumbani kila siku (achilia mbali wale wanaojifanya wanasaidia wake zao mara moja moja tena ni hadi waumwe)
Wanaume wanao waambia wanawake kwamba watafute pesa zao wenyewe ni kwa sababu unakuta mwanamke anahitaji zaidi kuliko kile kilichopo, kwani mara ngapi mnahongwa magari, nyumba, biashara n.k?

Unampa mtu 500 uliyoitafuta kwa jasho halafu anakuambia umenionaje kunipa sh 500 hainitoshi, hivi huyo unamjibu vipi? hali ya kuwa ndicho ulichonacho? na mfukoni huna kitu.
Kingine ni nia ovu wanayokuja nayo wanawake kwa mwanaume.

Wanawake wanabadilika sana aisee, ndio maana wanawake wenye uchumi wanaogopwa na wanaume, hata kama ulianza nae kipindi hana uchumi mzuri siku akipata kuna dharau flani zinaanza automatically anaanza kuku treat kama second class citizens.
Sio inferiority complex lakini wanawake wenye pesa wamekaa ile kiboss sana, halafu minato na tambo flani ambapo hizo pigo na sisi ni moto na maji, ndio maana mahusiano mengi yanavunjika chap.

Kuhusu majukumu ya nyumbani ni kutokana na asili.
Na mie nikuulize kwenye kutongoza mbona mnategea sie ndie tuanze mnashindwa nini kuturushia mistari? kwa sababu kiasili wanawake wana aibu, asili ya mwanaume ni kutoka kwenda kutafuta ili familie ile, mwanamke alee watoto nyumbani.

Mwanzo 3:16​

Kisha akamwambia mwanamke, “Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa, kwa uchungu utazaa watoto. Hata hivyo utakuwa na hamu na mumeo, naye atakutawala.”

Mwanzo 3:17-24​

Kisha akamwambia huyo mwanamume, “Kwa kuwa wewe umemsikiliza mkeo, ukala matunda ya mti ambayo nilikuamuru usile; kwa hiyo, kwa kosa lako ardhi imelaaniwa. Kwa jasho utajipatia humo riziki yako, siku zote za maisha yako. Ardhi itakuzalia michongoma na magugu, nawe itakubidi kula majani ya shambani. Kwa jasho lako utajipatia chakula mpaka utakaporudi udongoni ulimotwaliwa
 
Ndio, kuna msemo unasema "with great authority comes great responsibility" yani kila mamlaka makubwa huambatana na majukumu makubwa, lakini jambo la kushangaza ni kwamba wanaume wengi hasa wa kiafrika wanayataka hayo mamlaka tu ila majukumu hawayataki

Mimi naona ifike pahala dunia iachane rasmi na mfumo dume na haki sawa ishike hatamu, kwa sababu wanaume hawataki tena majukumu hivyo hata hayo mamlaka hayawafai, wanaume wengi hawataki haki sawa ila wanataka majukumu sawa tena ikibidi mwanamke ndio afanye zaidi ya mwanaume

MImi naona kusiwe tena na mgawanyo wa majukumu yani hata kazi za nyumbani zifanywe na wote kama ambavyo kutafuta pesa limekuwa ni jukumu la wote, majukumu ya mwanamke yabaki yale ya asili na ya kimaumbile tu ambayo ni kubeba ujauzito, kuzaa na kunyonyesha, hayo tu ndio ambayo mwanaume hawezi kuyafanya ila majukumu mengine yote ya nyumbani kama kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba, kulea watoto tangu wakiwa wachanga mfano kuwasafisha, kuwauguza wakiumwa, nk yafanywe na wote kwa usawa kabisa

Na vile vile kwa mfano mume akiweka laki mezani na mke naye aweke laki mezani mahitaji yote ya nyumbani wanunue kwa usawa bills zote walipe kwa usawa, na watoto wao wawahudumie kwa usawa ikiwemo kuwalipia ada na mahitaji yao mengine yote kwa usawa, hiyo ndio maana halisi ya 50 50 siyo mmoja anamtegea mwenzie eti mtu anataka pesa mtafute wote na bills mlipe wote, ila kazi za nyumbani na kulea watoto afanye mmoja na bado huyo mmoja amtii mwenzie na amlee kama anavyowalea watoto wake, what kind of cockamamie logic is this

Na jambo jingine naona pia tuachane na suala la mwanaume kumtawala mwanamke kila mtu ajitawale mwenyewe kusiwe na habari za kichwa cha familia, yani hakuna tena kusema kwamba mwanamke anatakiwa amtii mumewe kila mtu awe na maamuzi juu ya maisha yake mwenyewe, kusiwe na wa kumuongoza mwenzake na pia kusiwe na habari za kuoa wala kuolewa tena bali iwe ni kuoana

Mnawalaumu wanawake kuwa wanadai haki sawa halafu hawataki majukumu lakini mnasahau kwamba sababu ya wao kukataa hayo majukumu ni kwa sababu mnataka wafanye yale ya kwenu tu, ila ya kwao bado mmewaachia wenyewe hamtaki kuyafanya yani huwezi kumuambia mwanamke ajitafutie pesa zake na akusaidie majukumu, halafu hapo hapo bado unataka huyo mwanamke akufanyie majukumu ya nyumbani na bado akupe heshima na utii

Kwanza hapo huyo mke anakuwa siyo msaidizi tena bali ni kama business partner tu hivyo ondoa kichwani suala la kumlazimisha akutii, hivi mnadhani mwanamke aliambiwa amtii mwanaume kwa misingi gani kama siyo kuhudumiwa maana huwezi kukitawala kiumbe usichokihudumia, hakuna binadamu mwenye akili timamu anayefurahia kutawaliwa na binadamu mwenzie asiyewajibika kwa lolote juu yake na kiuhalisia ukitoa huduma zinazohusisha pesa hakuna wajibu mwingine mwanaume alionao juu ya mwanamke

Kama ikiwa mtoto anamtii mzazi wake kwa sababu amemzaa na amemlea, watu wa dini wanaitii miungu yao kwa sababu wanaamini imewaumba na inawapa uhai, je mwanamke anapaswa amtii mumewe kwa sababu gani, tena hata mtoto mwenyewe akishatoka kwao akaanza kujitegemea kinachobaki kwa mzazi wake ni ile heshima tu kuwa amemzaa, lakini huyo mzazi anakuwa hana mamlaka tena ya kumpangia mtoto maisha yake mfano afanye kazi gani au arudi nyumbani muda gani kwa sababu hamhudumii tena

Sasa inashangaza pale mwanaume anapotaka mkewe atafute pesa wasaidiane maisha kwa kisingizio kwamba mke naye ana mikono miwili na miguu miwili, ila huyo huyo mwanaume haoni ajabu kumtawala huyo mke mwenye mikono miwili na miguu miwili kama yeye, yani imefikia hatua wanaume wanaona uchungu kugawana mali na wake zao na wengine ndio kabisa hawataki kuoa kwa kisingizio kwamba eti wakishafanikiwa wake zao watadai talaka ili wagawane mali

Yani hawaconsider tena yale majukumu yote ambayo wake zao wanawafanyia pamoja na utii ambao wake zao wanawapa, siku hizi wanadai kwamba kila mtu ajitafutie pesa zake na ikitokea wameachana kila mtu aondoke na chake, lakini cha kushangaza kwenye majukumu mengine hawasemi kila mtu afanye kwa usawa na kwenye suala la mamlaka hawasemi kila mtu ajitawale mwenyewe

Wale waumini wa ukristo hasa wanaume kama mmeamua kufuata maandiko basi fuateni yote, na kama mmeamua kuyapuuzia basi yapuuzieni yote msichague yale yanayowanufaisha ninyi tu halafu mengine mnajifanya hamyaoni, kwa sababu maandiko yanasema mume ndio atakula kwa jasho na si mke, halafu mbele ndio yanaendelea kwamba mwanaume atamtawala mwanamke, yule mke mnayemuota wa Mithali 31 yalikuwa mawazo binafsi ya mfalme Suleiman na si maagizo ya muumba

Hivo basi ifike pahala wanaume mchague moja kati ya mwanamke mfanyakazi/mfanyabiashara au mama wa nyumbani, na aina yoyote utakayochagua hapo lazima ukubaliane na sifa zinazoambatana na aina hiyo ya mwanamke siyo unachagua mfanyakazi/mfanyabiashara mnasaidiana majukumu, halafu hapo hapo unataka awe kama mama wa nyumbani au unachagua mama wa nyumbani halafu hutaki kumhudumia unaanza kumuona golikipa
Wanawake wengi wa Afrika, hususan vijana wa mijini, hawatapenda mfumo wa majukumu sawa na haki sawa, wengi wamezoea kudanga na kuletewa.

Wengine huwa wanatuambia kabisa hawapendi ufeminia kwa sababu unawapa majukumu mengi ambayo hawayataki.

Na huo ndio mfumo ambao wengi wamelelewa nao na wanaukubali.

Ukitaka kujua hilo, weka mada ya kupinga mahari, sema mwanamme kulipa mahari ni mfumodume, wanawake waolewe bila mahari.

Halafu angalia majibu ya wanawake.
 
Mwanamke hapaswi kukuzidi kipato.

Mwanamke hapaswi kukuzidi elimu.

Mwanamke hapaswi kukuzidi umri.

Mwanaume ameumbwa kutii sio kuheshimu, kuheshimu tunaheshimu mzazi tu labda, ila siwezi heshimu mwanaume mwenzangu. Ndio jeshini ukiona mwanaume anapewa adhabu na anafanya huo ni utii si heshima.

Mwanamke kaumbwa kuheshimu, amheshimu mumewe.

Kwenye ndoa mwanamke apendwe, mwanaume aheshimiwe, hio ni asili huwezi badilisha.
Nadhani umegusia mambo yote ya msingi 👆👆👆. Uzi unaweza kufungwa sasa. Asante!
 
......Kwenye ndoa mwanamke apendwe, mwanaume aheshimiwe, hio ni asili huwezi badilisha......

Waefeso 5:22-33​

Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.

Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.

Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.

Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.
 
Ndio, kuna msemo unasema "with great authority comes great responsibility" yani kila mamlaka makubwa huambatana na majukumu makubwa, lakini jambo la kushangaza ni kwamba wanaume wengi hasa wa kiafrika wanayataka hayo mamlaka tu ila majukumu hawayataki

Mimi naona ifike pahala dunia iachane rasmi na mfumo dume na haki sawa ishike hatamu, kwa sababu wanaume hawataki tena majukumu hivyo hata hayo mamlaka hayawafai, wanaume wengi hawataki haki sawa ila wanataka majukumu sawa tena ikibidi mwanamke ndio afanye zaidi ya mwanaume

MImi naona kusiwe tena na mgawanyo wa majukumu yani hata kazi za nyumbani zifanywe na wote kama ambavyo kutafuta pesa limekuwa ni jukumu la wote, majukumu ya mwanamke yabaki yale ya asili na ya kimaumbile tu ambayo ni kubeba ujauzito, kuzaa na kunyonyesha, hayo tu ndio ambayo mwanaume hawezi kuyafanya ila majukumu mengine yote ya nyumbani kama kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba, kulea watoto tangu wakiwa wachanga mfano kuwasafisha, kuwauguza wakiumwa, nk yafanywe na wote kwa usawa kabisa

Na vile vile kwa mfano mume akiweka laki mezani na mke naye aweke laki mezani mahitaji yote ya nyumbani wanunue kwa usawa bills zote walipe kwa usawa, na watoto wao wawahudumie kwa usawa ikiwemo kuwalipia ada na mahitaji yao mengine yote kwa usawa, hiyo ndio maana halisi ya 50 50 siyo mmoja anamtegea mwenzie eti mtu anataka pesa mtafute wote na bills mlipe wote, ila kazi za nyumbani na kulea watoto afanye mmoja na bado huyo mmoja amtii mwenzie na amlee kama anavyowalea watoto wake, what kind of cockamamie logic is this

Na jambo jingine naona pia tuachane na suala la mwanaume kumtawala mwanamke kila mtu ajitawale mwenyewe kusiwe na habari za kichwa cha familia, yani hakuna tena kusema kwamba mwanamke anatakiwa amtii mumewe kila mtu awe na maamuzi juu ya maisha yake mwenyewe, kusiwe na wa kumuongoza mwenzake na pia kusiwe na habari za kuoa wala kuolewa tena bali iwe ni kuoana

Mnawalaumu wanawake kuwa wanadai haki sawa halafu hawataki majukumu lakini mnasahau kwamba sababu ya wao kukataa hayo majukumu ni kwa sababu mnataka wafanye yale ya kwenu tu, ila ya kwao bado mmewaachia wenyewe hamtaki kuyafanya yani huwezi kumuambia mwanamke ajitafutie pesa zake na akusaidie majukumu, halafu hapo hapo bado unataka huyo mwanamke akufanyie majukumu ya nyumbani na bado akupe heshima na utii

Kwanza hapo huyo mke anakuwa siyo msaidizi tena bali ni kama business partner tu hivyo ondoa kichwani suala la kumlazimisha akutii, hivi mnadhani mwanamke aliambiwa amtii mwanaume kwa misingi gani kama siyo kuhudumiwa maana huwezi kukitawala kiumbe usichokihudumia, hakuna binadamu mwenye akili timamu anayefurahia kutawaliwa na binadamu mwenzie asiyewajibika kwa lolote juu yake na kiuhalisia ukitoa huduma zinazohusisha pesa hakuna wajibu mwingine mwanaume alionao juu ya mwanamke

Kama ikiwa mtoto anamtii mzazi wake kwa sababu amemzaa na amemlea, watu wa dini wanaitii miungu yao kwa sababu wanaamini imewaumba na inawapa uhai, je mwanamke anapaswa amtii mumewe kwa sababu gani, tena hata mtoto mwenyewe akishatoka kwao akaanza kujitegemea kinachobaki kwa mzazi wake ni ile heshima tu kuwa amemzaa, lakini huyo mzazi anakuwa hana mamlaka tena ya kumpangia mtoto maisha yake mfano afanye kazi gani au arudi nyumbani muda gani kwa sababu hamhudumii tena

Sasa inashangaza pale mwanaume anapotaka mkewe atafute pesa wasaidiane maisha kwa kisingizio kwamba mke naye ana mikono miwili na miguu miwili, ila huyo huyo mwanaume haoni ajabu kumtawala huyo mke mwenye mikono miwili na miguu miwili kama yeye, yani imefikia hatua wanaume wanaona uchungu kugawana mali na wake zao na wengine ndio kabisa hawataki kuoa kwa kisingizio kwamba eti wakishafanikiwa wake zao watadai talaka ili wagawane mali

Yani hawaconsider tena yale majukumu yote ambayo wake zao wanawafanyia pamoja na utii ambao wake zao wanawapa, siku hizi wanadai kwamba kila mtu ajitafutie pesa zake na ikitokea wameachana kila mtu aondoke na chake, lakini cha kushangaza kwenye majukumu mengine hawasemi kila mtu afanye kwa usawa na kwenye suala la mamlaka hawasemi kila mtu ajitawale mwenyewe

Wale waumini wa ukristo hasa wanaume kama mmeamua kufuata maandiko basi fuateni yote, na kama mmeamua kuyapuuzia basi yapuuzieni yote msichague yale yanayowanufaisha ninyi tu halafu mengine mnajifanya hamyaoni, kwa sababu maandiko yanasema mume ndio atakula kwa jasho na si mke, halafu mbele ndio yanaendelea kwamba mwanaume atamtawala mwanamke, yule mke mnayemuota wa Mithali 31 yalikuwa mawazo binafsi ya mfalme Suleiman na si maagizo ya muumba

Hivo basi ifike pahala wanaume mchague moja kati ya mwanamke mfanyakazi/mfanyabiashara au mama wa nyumbani, na aina yoyote utakayochagua hapo lazima ukubaliane na sifa zinazoambatana na aina hiyo ya mwanamke siyo unachagua mfanyakazi/mfanyabiashara mnasaidiana majukumu, halafu hapo hapo unataka awe kama mama wa nyumbani au unachagua mama wa nyumbani halafu hutaki kumhudumia unaanza kumuona golikipa
Hiyo 50-50 unaitaka katika familia yako pekee au dunia nzima na katika kila kitu? Kama ni katika familia yako haina tatizo ila ni kama ulivyoandika kwenye title ya uzi wako, I have bad news for you, ni kila kitu kitacollapse na ulimwengu wote utashindwa kua normal.

50-50 inaweza kua achieved katika household tena inategemea na aina ya mwanaume uliye naye ila katika overall life situation ya sasa haiwezekani na haitokuja kuwezekana na sababu kuu ya kutokuwezekana ni huyo huyo mwanamke.
 
Back
Top Bottom