Profesa shida ya nchi yetu ni kutokutii sheria zilizopo na kutojali mipango tuliyojiwekea. Inasikitisha kuona miji mingi nchini ikikua kwa kasi-holela...kila mtu anajenga anavyotaka na hakuna mamlaka inayojishughulisha kuzuia hali hiyo.
Kama ulivyosema kupanga ni kuchagua. Nyie mliopewa nafasi ya kusimamia miji yetu ndiyo mnapaswa kuhakikisha sheria zilizopo zinafuatwa na kila raia. Pia wizara yako na halmashauri au manispaa zijitahidi kupima, kuuza na kusimamia uuzaji ardhi hasa za mijini kwa wananchi kuliko kuachia kila mtu auze kiholela hali inayopelekea ujenzi holela kuendelea kuwa tatizo kwenye miji yetu.
Mama hongera kwa kutujuza. Napenda kutoa mapendekezo machache kwenu mliopewa dhamana kutuongoza katika kipindi hiki:-
1. Ili kuondoa foleno DSM-jengeni reli kutoka bandarini hadi Chalinze na kuhakikisha kuwa Chalinze mnaweka bandari kavu kwa maana ya kuchambua mizigo inayokwenda Mby, Kigali malori ya kubeba mizigo, mafuta yote yaishie Chalinze wala yasiingie mjini
2. Wataalamu wako wa mipango miji wasikae ofisini huku wamefunga tai na AC wanatakiwa kuzunguka katika maeneo ambayo hayajapimwa wawapimie wenyeji wao uza viwanja na mashamba yao ili wanao nunua angalau wakute viwanja vilivyopimwa,
3. Kwa kweli hatuawaelewi mlioko serikalini mnatunia hekima ipi kuachia raslimali zetu kuondoka na wageni wakati bungeni na kwenye wizara zenu mnalalamikia bajeti ndogo.
4. Huo wimbo wa mji mpya wa Kigamboni ni kipaumbele cha nani,kma huko Manzese, Buguruni na kawe tunashindwa kulipia kodi ya elfu 20 Je ukijenga hayo maghorofa ya mji mpya tutaweza kuishi huko kweli au ndo lugha tunayoisikia kuwa Kigamboni imeuzwa?
5. Mama tutashukuru sana ukifunguka utueleze sawasawa maana humu ndani hatuna kanuni kandamizi na miongozo kama ya zamu ya Ndugai na Mama Makinda.
Tafakari!!!!!!!!!!!!!!!
Ndugu ZOMBA.
Ingawa mama hajaja na sijui atakuja lini kujibu, naomba nitofautiane na wewe kwa baadhi ya muono wako, wa kuhusu makazi. Nitaeleza kwa ujumla kwa sababu ya muda, na kusubiri majibu ya profesa Tibaijuka!
Kwanza naomba tuelewe serikali inauzoefu mkubwa sana, katika mambo mengi sana kuliko mtu/kampuni. Sababu serikali inaweza kuajiri mtaalam, kuandaa, kumsomesha na kumpatia exposure ( mfano ndo hata mama na uprof serikali imempeleka kujionea mambo Singapore) mtaalam yeyote mahili, kama itahitaji kufanya hivyo, Serikali imekuwepo kwa muda wa miaka 50 ( baada ya uhuru) hivyo hatuna mtu amefanya kazi 50 Years, ila kabati la wizara limekuwepo na nina amini uzoefu upo kabatini.
Kuhusu kamapuni binafsi, hapana sababu makazi ni mahitaji muhimu sana kwa binadamu. nakumbuka ni moja ya mambo ambao serikali duniani zinafanyia kazi kila siku. Ukisikia mtikisiko wa uchumi mojawapo ya sababu ni hayo mambo ya makazi. Hivyo ili kila mtu aweze kupata makazi stahili na bora serikali lazima ifanye kazi.
Real estate inahitaji mtaji mkubwa, siyo lelemama, ndo maana nilishauri baadala ya kuanzisha benki 3 kwa mwaka huu wa fedha wangeweza kuanzisha Real estate company, kama vipi NHC ijiunge stock market ipate mtaji mkubwa, then isiuze nyumba bali ipangishe na iboreshwe.
Siyo sehemu zote sekta binfsi imefanikiwa, mifano hai ipo siyo tanzania bali hata nchi jirani. Serikali itoe makazi kwa kupangisha, hapo itapanga mji (miji) na kulinda ukuaji wa uchumi wake.
Serikali itumie watalaam wake waliopo, ipange, isimamie mambo yataenda, sekta binafsi ije kujazilizia pale serikali inaona itahitajika na kufanya bei iwe ya kuangalia gharama halisi.
Hapo mwisho (rangi ya blue) mkuu tayari umeona hapo kuna deal, umejipigia pass mwenyewe, yaani wewe unaweza zaidi kuliko serikali? kazi ipo!!!!
0.5 cts
SP
Tatizo kubwa la Tz ni kujazwa kwa viongozi wasiojua wafanye nini. Kama kiongozi hajui afanye nini ni wazi hakuezi kuako na maendeleo.Leading from behind.
Waziri badala ya kutuambia mipango yake ni ipi na kashatekeleza ipi na anahitaji maoni wapi, anatupa li post la Singapore lisilo na kichwa wala mguu, full of generalities, no exactitude or specificity.
Sasa mimi nikikwambia New York City kuna underground train (subway) ndo itakusaidiaje wewe bongo ambaye rapid transit lanes na taa za barabarani zinakupiga chenga?
Na huyu ndo Ph.D ya ukwee, hao darasa la saba na Ph.D za kununua wakoje?
Tatizo kubwa la Tz ni kujazwa kwa viongozi wasiojua wafanye nini. Kama kiongozi hajui afanye nini ni wazi hakuezi kuako na maendeleo.
Maswali yamekuwa mengi kuliko majibu......
Master plans tunazo nyingi, lakini hazifanyiwi kazi. Mfano, Master plan ya Mtwara imekuwepo miaka nenda rudi lakini hakuna kinachofanyika.
Mara nyingi tunaongelea kuhusu mji mpya wa Kigamboni, lakini kuna mipango ya kundeleza miji iliyopo sasa tokea kipindi cha ukoloni hadi sasa bado haijatekelezwa.
Ama kweli wanayoiaribu nchi yetu ni wasomi, Mama Tiba naomba uirekebishe kwanza Manzese kisha uende kw Mnyamani Buguruni theni ukamalizaie ya kigamboni ndo uje hiyo ya singapore maan inaonekana mkijaenda namtumbo na kibandasamaki mtatuletea nyingine. fnya hivyo kabla ya 2015.
Nadahani wewe ndio ulitakiwa kuulizwa haya maswali... '' Je uholela unavumiliwa au kuendekezwa? Tupe habari.'' . Inakuwaje watu wanaachiwa kujenga holela na kukaa miaka hata zaidi ya arobaini(kama hamna serikali) halafu mkishaona mambo hayarekebishiki tena ndio mnakurukupa kurekebisha! Kwa mfano ghorofa lililojengwa holela likaporomoka na kuua ni nani aliacha mambo yaende holela?WanaJF
Nilikuwa mmojawapo wa viongozi tulioandamana na Mhe Rais katika ziara yake ya majuzi nchini Singapore. Ninawaletea sehemu ya Master Plan ya mji wao mpya unaojengwa kutokana na kuokoa ardhi baharini (reclamation). Unaona kila kipande cha ardhi mpya kimeshapangiwa matumizi yake na kuwekewa malengo ya majengo yanayotakiwa.
Kupanga ni kuchagua. Kunahitaji nidhamu na hakuna mchezo wala utani. Huwezi kuwa na mji uliopangwa kama unapenda na kuendekeza uholela na vurugu (chaos). Kinachotakiwa ni kushirikisha wadau wote kupanga malengo na viwango baada ya kupata maoni ya wataalam. Wanaoarithirika na kulazimisha kuhama kupisha maendelezo mapya wanalipw fidia stahiki na endelevu.
Anayedai vinginevyo si msema kweli. WaSingapore wamehaidi kutusaidia katika ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni. Ninakaribisha maoni yenu hasa nyie mlio nje na mnaishi katika miji iliyopangwa? Je uholela unavumiliwa au kuendekezwa? Tupe habari.
View attachment 97055
Mama Tibaijuka