Mama Tibaijuka, hongera kwa kujianika jamvini. Kwa uzoefu wako, ukiwa chuoni, WAMATA, Habitat na sasa Waziri, nilitegemea kabla ya kuwakilisha hoja yako basi ungewatumia wasaidizi wako na kujiridhisha kwa sana kabla ya kupost. Hiyo post yako ni sawa sawa na kuweka chumvi kwenye kidonda. Nikuambie kati ya wizara mbovu kiutendaji, kukosa weledi, uzalendo, kujawa na ubinafsi, na kuchangia kuiangusha kwa kila hali nchi yetu ni wizara yako. Sikutegemea kweli ungeweza kuibuka na kusingle out ka issue kadogo kwa taifa ukitegemea sympathy. Forget. Nikuambie, mimi ni mtumishi wa serikali ambaye karibu naelekea kustaafu maeneo ya Arusha. Nikuambie sasa nimeanza kuomba kupata kiwanja ili nijenge makazi yangu tangia 1996. Sijawahi kupata. Utasikia vimepimwa tena kidogo, lakini unakuja ona majina au kuambiwa wakubwa wamegawana or zoezi la upimaji limesimamishwa. Ni migogoro juu ya migogoro or ulipie mara mia. Huwezi kuniletea hadithi zako leo nikusifie wakati vitu vidogo na vya msingi kabisa katika mipango miji ni kugawa surveyed lands vinawashinda. Siwezi.
Sasa niseme, unaweza kuwa unania njema, lakini haitatekelezeka kwa sababu UWEZO HUNA. Serikali yako inayoongozwa na chama chako hawana uwezo huo kwa sababu. 1. Nyie nyote hamna vipa umbele. 2, Hamsimamii sheria zilizopo ambazo ni nzuri tuu. 3. Hamna mipango endelevu. 4. Suala lote la ardhi limezingirwa na Rushwa, Ubinafsi, Kujuana na akili ndogo isiyo na uzalendo kusimamia. Aliingiaga Magufuli wakati Fulani. Kulikuwa na impact japo naye hakukaaa. Sijui aligusa pabaya! Angalau alijaribu kutaka kurudisha nidhamu, kusimamia taratibu zilizopo, uwajibikaji nk.
Matatizo yote haya yamefanya serikali na nyie kina Tibaijuka kufikia mahali mnakuwa na narrow vision badala ya kuwa pana, mnafocus kwenye vitu vidogo, badala ya kitaifa, Waziri huwezi kujitapa na Kigamboni, wakati kila dakika li-squatter linazaliwa kwenye miji yetu. Mmegota, ni kama engine inayosumbua kila mara. Ukienda kwa fundi atakushauri very simple kuwa inahitaji overhaul. Ndicho kilichobaki. Muondoke waje wengine, or nchi ipate RAIS DIKTETA MZALENDO ambaye atakuwa anauliza maswali kama UTARATIBU UNASEMAJE? KWA NINI HAUKUFUATWA? BASI UFUATWE NA NIPEWE RIPORT YA UTEKELEZAJI BAADA YA SIKU SABA.
Mmetuharibia sana nchi yetu.