Masoud Kipanya hii haiko sawa

Masoud Kipanya hii haiko sawa

Baba Wawili 2012

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2012
Posts
413
Reaction score
336
Natumai wote ni wazima.

Binafsi sijapendezwa na katuni iliyochorwa jana katika gazeti la Mwananchi kama ambavyo huwa inachorwa na Bwana Masoud.

Ki ukweli ukiiangalia kwa makini utagundua ina "Matusi" na waliochorwa katika katuni hiyo ni viongozi wa Taifa hili. Nadhani Mhariri wa gazeti la Mwananchi ni vyema wakaweka mipaka katika katuni zao. Ili kulinda heshima ya gazeti lao.

Mandla.

Masudi kipanya hii ya kidole cha kati haiko sawa, michoro yako daima ni ya busara anaeweza kutafisiri hata mtoto mdogo. Hapa ulikosea, binafsi sikuridhika!
 

Attachments

  • kipanya.jpg
    kipanya.jpg
    70.6 KB · Views: 12,412
attachment.php


Mbona mimi sijelewa.....?
Wewe ni kama huyo nywele nyeusi, hajaelewa mwenzake anamaana gani na hilo dole la kati! Dole lake kajielekezea! Mwenzake kaelekeza kunakotakiwa
 
attachment.php


Mbona mimi sijelewa.....?

Wote Mnaomlalamikia Masoud Kipanya Ni MAPOPOMA Tena MLIOTUKUKA Na Mmeonyesha Udhaifu Wenu Katika Mapokeo Na Tafsiri Ya Kitu au Mazingira Fulani ILA Kwa TULIOJAALIWA AKILI Kubwa Na Nyingi ZILIZOTUKUKA Tumemwelewa Vizuri Mno Na Sana Masoud Kipanya. Hivi Kwa Akili Yenu Tu Ya Kawaida Mnadhani Kama Hao Watu Wote Wawili Ambao Upinzani Wao Kisiasa Ulikuwa Ni Sawa Na Wa Simba Na Yanga Wakikutana Hawezi Kupeana Maneno Yetu Yale Ya Shombo?

Tunajifanya Hatujui Matusi Na Tunayakemea Kwa Kisingizio Cha Kuwa Na Maadili Kwa Watoto Zetu Wakati Hapo Hapo Sisi Hawa Hawa Tunawanunulia Watoto Zetu Simu Ambazo Wao Muda Wao Wote Wakiwa Nazo Kazi Yao Ni Kuangalia Na Ku Download Pono Tu Huku Wengine Hao Hao Watoto Zenu Mkiwanunulia Nguo Za Kihuni Na Mkiwasifu Wakiwa Wanazivaa, Lakini Kwa Masoud Kipanya Kuchora Hiyo Katuni Yenye Kidole Cha Kati Tunajifanya Tunawaka Na Kuhamaki.

UNAFIKI Mtupu Na Watanzania Hii Tabia Ya Kinafiki Ndiyo Inatumaliza. Mbona Humu Humu JF Watu Huwa Tunapeana Makavu Tena Kwa Mitusi ILIYOTUKUKA Na Hamsemi au Hamkemei? au Mnadhani Hao Watoto Wenu / Wetu Hawamo Humu?

Nyie Wenyewe Mnaojifanya Kuzingatia Maadili Mna Maadil Kweli Huko Mlipo? Kwendeni Zenu Huko!
 
Mi nadhani kabla hilo gazeti halijaprinti hiyo katuni bila shaka nao walitaka tafsiri, na waliporidhika na maelezo ya Masoud ndio wakachapisha.......
 
Uchambuzi wote huu ndiyo unaopelekea umaana wa sanaa... mitizamo tofauti kwenye jambo lile lile! Big Up Masoud! Ukiona huweze kuwa na tasfiri zaidi ya moja basi hiyo siyo sanaa!
 
Natumai wote ni wazima.

Binafsi sijapendezwa na katuni iliyochorwa jana katika gazeti la Mwananchi kama ambavyo huwa inachorwa na Bwana Masoud.

Ki ukweli ukiiangalia kwa makini utagundua ina "Matusi" na waliochorwa katika katuni hiyo ni viongozi wa Taifa hili. Nadhani Mhariri wa gazeti la Mwananchi ni vyema wakaweka mipaka katika katuni zao. Ili kulinda heshima ya gazeti lao.

Mandla.
 
Back
Top Bottom