Mashujaa wa kweli Tanzania hawakumuogopa Hayati Dkt. Magufuli

Toka Mwaka 2015 mpaka March 17 2021 wanaume walibaki wawili tu,TUNDU ANT-PASS LISSU na JOHN POMBE MAGUFULI.
Mpaka sasa nina uhakika 100% Tundulissu akifa Leo itatuchukua miaka mingi Sana kuzaliwa mtu wa aina yake
Hata Magufuli atamkumbuka huko aliko😆😆😆

Hawa vidume kila mmoja alikuwa tayari kufa kwa kusimamia anachokiamini,bad luck dhaifu zaidi ndio kafariki!Ila hakika wameingia kwenye historia ya Tanzania.
Kampeni ya uchaguzi mkuu 2020 haitasahaulika, Magufuli hakuweza hata kutamka jina la Tundu Lissu hadharani.
 
1,lissu alikimbia na kudai hana imani na usalama alio nao.

3,kibatala ni wakili msomi ambaye anasimamia taaruma yake pekee,labda ungesema kama nayeye ni mwanaisiasa au mwanaharakati.ndio sababu amekuwa si muhanga muda wote.ukichanganya siasa na taaluma umechagua usumbufu.

4,wale mashangazi wawili,inafahamika shida yao ya msingi ni njaa na ulafi wa vyeo.sasa kwa sababu ccm haihitaji watu wasio wavumilivu ndio sababu wameachwa waendelee kuropoka kama warevi,hakuna anayeshughulika nao.
Umetokota,wale mashangazi hawana njaa kama unavyofkkiri baba zao wako vizuri na wao wamesoma na wako vizuri pia
 
Umetokota,wale mashangazi hawana njaa kama unavyofkkiri baba zao wako vizuri na wao wamesoma na wako vizuri pia
wako vizuri!!! unajua kuwa vizuri ni swala pana sana.

unadhani mama salma kakosa nini mpaka akagombea ubunge tena!!!
 
wako vizuri!!! unajua kuwa vizuri ni swala pana sana.

unadhani mama salma kakosa nini mpaka akagombea ubunge tena!!!
Wenye njaa wote walisalim amri wakaunga mkono juhudi,kuwa upinzani ni risk kwako kiuchumi,we jua wale mashangazi hawaendekezi njaa,wangeendekeza njas wangeunga mkono juhudi na wangepewa vyeo
 
Wenye njaa wote walisalim amri wakaunga mkono juhudi,kuwa upinzani ni risk kwako kiuchumi,we jua wale mashangazi hawaendekezi njaa,wangeendekeza njas wangeunga mkono juhudi na wangepewa vyeo
ndio maana nikakwambia wale hawatafuti ugali mkuu.unaelewa mtu akijiita mwanaharakati!!!
kwanza ni kosa kubwa sana kama mnawachukulia kama wapinzani wenzenu.
 
1,lissu alikimbia na kudai hana imani na usalama alio nao.

3,kibatala ni wakili msomi ambaye anasimamia taaruma yake pekee,labda ungesema kama nayeye ni mwanaisiasa au mwanaharakati.ndio sababu amekuwa si muhanga muda wote.ukichanganya siasa na taaluma umechagua usumbufu.

4,wale mashangazi wawili,inafahamika shida yao ya msingi ni njaa na ulafi wa vyeo.sasa kwa sababu ccm haihitaji watu wasio wavumilivu ndio sababu wameachwa waendelee kuropoka kama warevi,hakuna anayeshughulika nao.
Umepuuzwa na jumuia ya JF.
 
Wanajamvi,

Kuna watu wanastahili nishani. Kukosa uoga kwao hakuelezeki. Wakati Mwendazake anafungwa watu, kuharibu biashara zao, kuwapakazia makosa yasiyokuwa na dhamana, na wengine kuuawa, hawa jamaa hawakunyaza kimya. Kilikuwa kipindi kigumu cha kuogopesha sana. Watu hawakuwa huru kuongelea serikali na siasa mbele ya watu wasiowafahamu. Hawa jamaa hawakuyumba. Hebu tuwataje:

1) Tundu Lissu - Kwa kifupi tu - Huyu alindamana kupinga udikteta. Alikuwa na jeuri ya kumwita Mwendazake dikteta uchwara. Alifunguliwa kesi zisizokuwa na mashiko. Alipigwa risasi 16 na Mungu akamponya. Baadae akaja kumpinga Mwendazake katika uchaguzi! Katika mazingira na hofu iliyojengwa na Mwendazake, huu ulikuwa ni ujasiri wa kupewa nishani.

2) Lawrence Mafuru - Huyu alikuwa ni Managing Director wa NBC Bank na baadae Msajili wa Hazina. Alikuwa na hali nzuri tu ya maisha na angeweza kunyamaza tu akaendelea na maisha bila bughudha. Wakati Mwendazake anatimua timua watu waliokuwa wanapingana naye, Mafuru alidiriki kupingana na Mwendazake mchana kweupe kwenye TV wakati akijua wazi kuwa atapoteza kazi yake. Mwendazake aliwashutumu watu wa benki kuwa wanaweka fedha za serikali katika fixed deposit the kulamba faida kwa manufaa yao. Mafuru akiwa Clouds 360, alimpinga Mwendazake kwa kusema kuwa huo ni uongo kwa vile jambo hilo kwa taratibu za benki haliwezekani. Haikuchukuwa juma moja, Mafuru akafukuzwa kazi na Mwendazake.

3) Wakili Kibatala na jopo lake - Hawa jamaa wamesimama na wapinzani kwa kipindi ambacho Mwendazake alifanya Watanzania kuogopa Upinzani kama ukoma. Hawa jamaa hawakuterereka hata kidogo. Siyo wengi wenye msimamo huu ktk Tanzania. Wengi wanaangalia matumbo yao tu. Hawa jamaa wanastahili nishani kwa kutoogopa udikteta ule.

4) Mashangazi Maria Sarungi na Wakili Fatuma Karume - Hawa wamempinga Mwendazake hata pale ambapo watu waliogopa hata kukohoa katika vyumba vyao vya kulala. Wanastahili kupewa nishani ya ushajaa.

5) Taja wako kama wapo
Mzee Shamte wa TPSF, alimsahihisha Magufuli juu ya private sector.
Aliishia kubambikwa kesi ya uhujumu uchumi na alifia jela mzee wa watu.
Magufuli alikuwa shetani.
 
Back
Top Bottom