Mariam Wangwe na Jukwaa la Wahariri

Status
Not open for further replies.
Sidhani kama mtoa hoja alikuwa na nia mbaya na Dr. Slaa.Alichokuwa anamaanisha si kila neno utamkwa na kila kinywa hata kama ni kweli.

"Sijawahi kujuta kwa kukaa kimya" Luqman akimwambia mwanae
 
Sidhani kama mtoa hoja alikuwa na nia mbaya na Dr. Slaa.Alichokuwa anamaanisha si kila neno utamkwa na kila kinywa hata kama ni kweli.

"Sijawahi kujuta kwa kukaa kimya" Luqman akimwambia mwanae

Lakini mbona hapa jf tunatamka kila kitu? Tabia ya kufichiana ukweli katika nchi hii ndiyo iliyotufikisha hapa wakuu
 
Anayo sema Dr W. Slaa ni sahihi katika taratibu za kisheria anatambulika msimamizi wa mirathi mmoja tu aliyeteuliwa na familia. Katika tamaduni za wenzetu hao unaweza kuoa wake wengi na hata wanawake kuoana wenyewe wanaita ndoa ntobi sasa kwa ishu hii inaonekana hawa majamaa wameshamteka .Mafisadi bwana sio mchezo na lengo ni kuwasambaratisha watu wanaowaumiza vichwa kama Mzee Slaa. Wanachotakiwa kufanya sio kuzungumza na vyombo vya habari wayamalize wao kama familia kwanza.
 
Umetumwa nini?
Hebu soma hapa usikurupuke na wewe

ndugu yangu mbona wewe ndiye unayekurupuka???
hiyo habari ya gazeti la mwananchi mbona umei-edit??kwanini usii-copy na kui-paste kama ilivyo??wewe una lako jambo tena unataka kupotosha watu.

kwanini umeiondoa kauli ya dr.slaa kama ilivyonukuliwa kwenye gazeti(na mwandishi wa habari)??

yaani watu wengine sijui mkoje?yani akiguswa kiongozi wa chadema au chadema yenyewe povu linawatoka!!!

dr.slaa kwani yeye ni nani hadi asikosee?mara ngapi anachemka na watu tunaelewa kuwa amechemka. tatizo lenu wapambe kila jambo mnapinga tu bila hoja.
Imani yake ya ukatoliki haiingiliani na suala la ndoa ya mtu mwingine.
na mtu huwezi kuitambua/kutoitambua ndoa ya mwenzako kwa misingi ya imani yako isipokuwa kwa mujibu wa sheria na katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania,wala si kwa sheria za katoliki,lutheran,uislamu ama nyingineyo.

ukweli ni kuwa hapo dr.slaa ameyumba.

soma hapa kauli ya dr.slaa uliyoificha:
"Dk Slaa ambaye alisisitiza kwamba hamfahamu Mariam kama mke wa marehemu Wangwe, alisema anasikitishwa na kauli yake ambayo anaamini kuwa imelenga kukichafua chama".
 
Lakini mbona hapa jf tunatamka kila kitu? Tabia ya kufichiana ukweli katika nchi hii ndiyo iliyotufikisha hapa wakuu

Kutokutamka kila kitu haimaanishi kwamba unamficha mtu ukweli na si kila ukweli usemwa ndugu yangu.ndo mana watu wakasema unatakiwa kufikiri kabla ya kusema.kama unaongea kila kitu tena bila hata ya kufikria kwanza basi kuna tatizo.
 
nawewe soma hapa,inaonekana macho yako yanaangalia baadhi ya maneno yanayokufurahisha,yasiyokufurahisha huyaoni.na kwa faida ya wote tunaojadili naomba niiweke habari nzima bila kuipunguza au kuiongeza chochote kama ifuatavyo.

KIFO cha Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe kinazidi kuibua mengi baada ya mke wake wa kati Dotto Mohamed kukana maelezo ya mke mdogo Mariam Wangwe kwamba Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeitelekeza familia.

Akizungumza na gazeti hili jana, Dotto alisema kauli ya Mariam ni nzito mno kuitoa sasa kwani anaamini matukio yanayoendelea baada ya kutokea msiba huo, ndiyo yanayoweka pazia la mawasiliano kati ya Chadema na familia ya Marehemu.

"Sijaisoma taarifa yote ila mtoto wangu ameniletea gazeti ambalo bado ninalo. Mimi ninashindwa kufikiria wala kuwaza kuanza kukilaumu Chama kwamba kimetutelekeza kwani ni mapema mno kufanya hivyo na wote bado tuko kwenye majonzi," alisema Dotto na kuongeza:

Nasema nashindwa kukilaumu chama kwa sababu tangu kutokea kwa msiba huo hakuna aliyetulia, familia bado ina majonzi, chama chenyewe bado kinalia na hata jamii inaendelea kumlilia Wangwe nasema familia yangu bado ina imani na chama na hatuwezi kukilaumu sasa," alisema.

Dotto alisema anaamini Chadema inaongozwa na watu wenye busara hivyo hawezi kuinenea mabaya kabla ya kuridhika kwamba viongozi hao wameanza kupingana na busara hiyo.

"Ninihitaji muda kupima hekima ya chama kabla sijakihukumu kwani kinyume chake nitakuwa sijakitendei haki," alisema.

Alisema mpaka sasa bado anaamini kuwa Chadema iko sambamba na familia ya marehemu Wangwe kwani hata kwenye arobaini iliyofanyika kijijini Komakorere chama hicho kilituma wawakilishi.

Mke huyu wa pili wa Chacha Wangwe anaishi jijini Mwanza na jana alikuja jijini Dar es Salaam kuwachukua watoto wake wawili waliokuwa wakiishi na Mariam, mke mdogo wa Wangwe.

Jana Dotto aliiambia Mwananchi kuwa katika safari yake hiyo pia amepanga kukutana na Mariam na kuzungumza naye ili ajue kiini cha shutuma zake kwa Chadema.

"Kuja kwangu Dar es Salaam ni pamoja na kuwachukua wanangu wawili ambao wamekuwa wakiishi na Mariam; katika ujio huo tutakaa tuzungumze anieleze kwa nini ameamua kuzungumza maneno hayo sasa,".

Alisema hata kama Mariam atafanikiwa kumshawishi aamini maneno yake, bado atahitaji muda kukubaliana naye kwani anaamni kuwa bado ni mapema mno kutoa shutuma hizo.

"Sisi bado tuna imani na Chama na hatuwezi kujua chama kinatuwazia nini hivyo narudia: ni mapema mno kutoa shutuma hizo kwani wote bado tuko kwenye majonzi," alisisitiza.

Akizungumzia kauli ya Dotto, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema ndiyo aliyotarajia kusikia kutoka kwa familia ya marehemu Wangwe.

"Nafikiri kauli hiyo ndiyo niliyotarajia kutoka kwa familia ya Wangwe ninayemfahamu kwa sababu kama utakumbuka tangu mwanzo wa msiba, sisi (CHADEMA) tulikuwa tukisakamwa sana lakini tulikaa kimya kwa busara ili tusimkamate mchawi asiyetuhusu," alisema.

Dk Slaa ambaye alisisitiza kwamba hamfahamu Mariam kama mke wa marehemu Wangwe, alisema anasikitishwa na kauli yake ambayo anaamini kuwa imelenga kukichafua chama.

Hiki anacholalamikia kwamba Chadema hawakuhudhiria arobaini ya mume wake, nashindwa kuelewa. Kumbuka mimi nina miaka 60 na tangu nianze kufahamu arobaini, najua zinafanyika mahala alikozikwa marehemu.

Wangwe alizikwa Komakerere na arobaini yake ilifanyika huko na Chadema tulituma mwakilishi. Hii arobaini aliyoifanya Mariam na Profesa Wangwe Dar es Salaam hatukuijua wala wao hawakutaka Chadema iijue," alisema.

Akifafanua alisema ingawa Mariam alitoa taarifa ya arobaini aliyoifanya Dar es Salaam, waalikwa katika taarifa hiyo ni wabunge kwa majina yao na sio Chadema kama taasisi.

Alisema pamoja na kasoro hiyo wabunge wa Chadema Suzan Lyimo na Grace Kihwelu walihudhuria kwa kofia zao lakini waliwakilisha chama kwa salamu ambazo zilisomwa na Lyimo katika hafla hiyo.

"Mimi Dk Slaa nilialikwa kwa ubunge wangu na sio ukatibu mkuu wa Chadema na Mbowe alialikwa kwa jina lake na sio uenyekiti wa Chadema vivyo hivyo wabunge wengine. Sasa Chadema inapolaumiwa tunashindwa kuelewa," alisema na kuendelea

"Mimi namshauri Mariam akutane na wazee wamshauri kwanza badala ya kukurupuka na kutoa maneno ya kukipaka matope chama. Yeye anataka athaminiwe, atathaminiwaje kama yeye Mariam hataki kukithamini chama," alihoji

Kauli ya Dotto na Dk Slaa imekuja siku tatu baada ya mke wa tatu wa Marehemu Wangwe kuzungumzia utata wa kifo cha mumewe na kukitupia lawama Chadema kwamba kimeitelekeza familia baada ya kifo hicho.

Mariam alienda mbali zaidi na kumtaka spika wa Bunge Samwel Sitta kuchunguza kifo hicho akidai kuwa haridhiki na uchunguzi uliofanywa na jeshi la polisi.

Wangwe, mwanasiasa machachari aliyepata umaarufu kwa kuibua hoja tata bungeni, alifariki dunia katika ajali ya gari wakati akisafiri kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam kuhudhuria mazishi ya mfanyabiashara na mbunge wa kwanza wa jimbo la Tarime Bhoke Munamka.

Lakini mazingira ya kifo chake yalizua utata mwingi baada ya kuchukuliwa kama agenda ya uchaguzi mdogo katika kampeni zinazoendelea sasa jimboni humo kumpata mrithi wa kiti chake.

Tayari Jeshi la Polisi limemfungulia mashtaka Deus Mallya aliyekuwa akisafari na marehemu kwa tuhuma za kusababisha mauaji hayo.

Lakini mke huyo mdogo wa Wangwe anaona juhudi hizo za polisi ni ndogo na hivyo, serikali na Spika Sitta hawana budi kuongeza uzito wao.

“Sipendi mambo haya yaishe hivi hivi," alisema mama huyo. "Familia ya Wangwe haijaridhishwa na namna polisi wanavyofuatilia kifo cha Wangwe."

"Wasiwasi wangu ni uchunguzi unaofanywa na polisi kwani hawajawahi hata kufika kuniuliza kuhusu kifo cha Wangwe nikiwa kama mke wake.“Labda maelezo yangu yangewasaidia kwa kiasi fulani.

Akizungumzia hali ilivyokuwa katika kipindi cha kuelekea kifo cha mumewe, Mariam alisema mambo yalikuwa magumu sana nyumbani, hasa baada ya Wangwe kusimamishwa nafasi yake ya makamu mwenyekiti wa Chadema.

Pia Mke wa pili wa marehemu Chacha wangwe,Doto amesema cha msingi ni viongozi kusaidi kulea watoto tisa aliowaacha marehemu ambao ni Zakayo na Rhobi (1 ambao ni mapacha, Bob (17), Pendo (16), Beatrice, (15) na Wangwe mwenye miaka 14 ambao ni watoto wa mke mkubwa nayeitwa Ghati.

Kwa yeye Doto ana watoto wawili, Mwajuma (11) na Ghati (6) wakati Mariam ana mtoto mmoja anaitwa King (1).

Naye Beatrice Charles, anaripoti kuwa viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Dar es Salaam kimemtaka katibu wa chama hicho, Wilbroad Slaa kumuomba radhi mjane wa marehemu chacha Wangwe kwa kutomtambua kuwa ni mjane wa Chacha Wangwe.

Akizungumza na waandishi wa habari Jiji jana katibu wa vijana Wilaya ya Kinondoni Mauld Mkwanji alisema Dk Slaa anapaswa kumuomba radhi mjane huyo kutokana kutomtabua.

“Kauli hiyo imetukwaza sana sababu marehemu Wangwe hakuwa msiri na wakati wa uhai wake alimtambulisha mkewe wake kwa viongozi wa chama na walikuwa wanamfahamu vizuri sasa iweje wasimtambue,” alisema Mkwanji.

Alisema kitendo cha Dk Slaa kutomtambua mjane huyo ni kutomtendea haki na kwamba anapaswa kumuomba radhi.

Alisema kitendo cha katibu huyo kinaweza kuendeleza chuki katika familia hiyo.
 
Una maana ya "fitina ama zengwe la ukabila" linawatafuna kama mchwa? Hivi unadhani kuanguka kwa CHADEMA ni faida kwako na kizazi chako ama? Kaka CHADEMA yapaswa kulindwa kwa hali na mali kwa faida ya maendeleo ya demokrasia ya ushindani nchini mwetu na vilevile kupunguza nguvu za manyang'au kuligeuza taifa letu kuwa mafia-state kama ilivyo Kenya, Italia, Pakistan na kwengineko. Ama zaidi kutufikisha walipo Zimbabwe, Somalia na pengine kubaya zaidi ya huko.

Kama unadhani kutafunwa kwa CHADEMA kunaiumiza CHADEMA tu fikiria zaid maana kama wewe ni mmoja wa wale wenye ndoto ya kuwa CCM itabadilika kutoka ndani basi ujue kama CCM itashinda TARIME huo utakuwa ni mwisho wa ndoto zako. Ni wazi kuwa mafisadi na wapambe wao wataongeza nguvu ndani ya CCM na kuonyesha kuwa umafia na ufisadi unalipa na bado tegemeo kwa maslahi ya genge lenu.....

Kumbuka waweza kuwa unafaidika na kutafunwa kwa CHADEMA sasa lakini jiulize kuhus ndugu zako na vizazi vyko huko mbaleni....laana ya ufisadi ni lazima iwaangukie hivyo kuwa makini na ushabiki wako kaka....

Tanzanianjema

TanzaniaNjema,

Nakuheshimu sana, kunawiri au kuanguka kwa Chadema hakunihusu unless unazungumzia upinzani at large. Before Chadema comes into picture tulikuwa na powerful NCCR hapa halafu CUF wamevurunda kwa upuuzi wao na wamekufa kifo cha mende na kama Chadema ( na kwa mwendo huu they will ) wataanguka so be it watakuja wapinzani wengine bado tupo katika evolution stage ya upinzani mpaka hawa wababaishaji watakapoondoka wote then hao manabii wa kweli ndio watakuja. Mimi sina jukumu la kui babysit Chadema they r old enough kujua wanayoyafanya hayana tija kwa taifa.

Tanzanianjema unataka watanzania wote tuwe Chadema? why not CUF, TLP. NCCR waambie hao jamaa zako kwa mwendo huu wanatupeleka siko na hatuko tayari kuburuzwa, eti Chadema yafaa kulindwa kwa hali na mali! r u kidding me?

Chadema hawatafunwi wanajitafuna wenyewe kwa siasa zao chafu za "kushughulikiana" ( political of elimination ) kila wanapotafautiana na wenzao. Safisheni nyumba yenu msitafute mchawi kutoka nje mchawi ( ukabila ) mmeu asisi wenyewe....
 
Namtafuta Mwarabu wa Tabora, tajiri mmoja hivi aliyezaa watoto wawili na Mariam ambaye baada ya kufilisika Mariam alimuacha na kukimbilia kuolewa na Wangwe. Kuna maneno Mariam ameyasema leo, nataka sana kuongea na huyu mwarabu kupata kauli yake. Nisaidie namba yake tafadhali. Hili suala libaki kwenye siasa kwa kuwa kuna kauli nzito imetolewa kuhusu Samuel Sitta na siasa za Tabora.

PM
 
TanzaniaNjema,

Nakuheshimu sana, kunawiri au kuanguka kwa Chadema hakunihusu unless unazungumzia upinzani at large. Before Chadema comes into picture tulikuwa na powerful NCCR hapa halafu CUF wamevurunda kwa upuuzi wao na wamekufa kifo cha mende na kama Chadema ( na kwa mwendo huu they will ) wataanguka so be it watakuja wapinzani wengine bado tupo katika evolution stage ya upinzani mpaka hawa wababaishaji watakapoondoka wote then hao manabii wa kweli ndio watakuja. Mimi sina jukumu la kui babysit Chadema they r old enough kujua wanayoyafanya hayana tija kwa taifa.

Tanzanianjema unataka watanzania wote tuwe Chadema? why not CUF, TLP. NCCR waambie hao jamaa zako kwa mwendo huu wanatupeleka siko na hatuko tayari kuburuzwa, eti Chadema yafaa kulindwa kwa hali na mali! r u kidding me?

Chadema hawatafunwi wanajitafuna wenyewe kwa siasa zao chafu za "kushughulikiana" ( political of elimination ) kila wanapotafautiana na wenzao. Safisheni nyumba yenu msitafute mchawi kutoka nje mchawi ( ukabila ) mmeu asisi wenyewe....

MMhh! Pesa ya Rostam Azizi hiyo. Kazi kweli kweli!
 
Wanabodi,

Binafsi sidhani kama kuna kitu kimeharibika hapa kiasi kwamba lawama ziwe za chama.
Nimesoma maelezo ya Dr.Slaa na inaonyesha wazi kwamba amekuwa akisisitiza kulingana na madai ya Marium kuwa yeye pamoja na viongozi wote wa Chadema walialikwa Hitma (Arobaini) kama watu binafsi..
Na ndio Utaratibu wakidunia huwezi kualika watu msibani kutokana na nyadhifa ama mtazamo wao kichama...Watu hualikwa msibani ama ktk harusi kama watu binafsi na familia zao..
Kuna misiba kibao ya viongozi wa juu CCM wameondoka na hatukuona viongozi wa chama wakihudhulia (Arobaini) wala sio swala la kulaumu hata kidogo kwa sababu hitma haikamiliki kwa kuhudhulia viongozi ama vigogo isipokuwa dua za watu ndio hitma yenyewe.. Again, bado inatuonyesha sisi kuwa waafrika bado kabisa tunaamini na kuabudu zaidi watu badala ya maandiko - neno la Mungu.

Kwa hiyo, hili linajibu swali la Marium anapojaribu kuhusisha msiba na siasa za chama. Na Dr.Slaa aliposema hamtambui Marium kama ni mke wa Marehemu ni mawazo yake Dr.Slaa binafsi na pengine anazo sababu za kuweka madai hayo..Yawezekana kabisa kuwa Marium kaolewa nje ya sheria hizo hizo mnazotaka kumfunga Dr. Slaa..Sina hakika Marium ni dini gani lakini yanipa fikra tofauti hapa kuwa yawezekana wamefunga ndoa Halmashauri ya jiji, kienyeji, msikitini ama kanisani.
Kisheria ni hadi pale ndoa hiyo imekuwa registered ndipo hutambuliwa kisheria kwa sababu hizo option zote za kufunga ndoa hazihalalishi ndoa isipokuwa pale inapokuwa registered. Mara nyingi watu wengi hufikiria kwamba wakienda kuoana katika Ofisi za Halmashauri. msikitini ama kanisani basi ndoa zao zimefuata sheria..
Pili yawezekana kabisa kwamba Marium alitambulishwa kwa baadhi ya viongozi wa Chadema na sio yeye kwani nina hakika kabisa kuwa hata Kikwete leo hii pamoja na kwamba ana mke wa pili wapo viongozi wa juu CCM hawafahamu wala hawajapata kujulishwa..Hivyo siku huyu mkewe akitoa madai fulani yanayokilenga chama ni muhimu afahamu nafasi yake pia inaweza kupingwa na baadhi ya viongozi... Kwa sababu hawamtambui kama ni mke wa rais hata kama habari hizi wamezipata kupitia vyombo vya habari.

Mwisho kama utasoma vizuri habari hii kama ilivyoandikwa, inaonyesha wazi ni viongozi wa Chadema waliosema Dr. Slaa anatakiwa kumwomba radhi Marium.. hivyo kwa nini lawama hizi zinawashukia Chadema kama chama..
Kabla huyu mama hajajitokeza ktk vyombo vya habari kuna mmoja wenu alimfahamu huyu mama kama mjane wa marehemu?...yeye analalamikia viongozi wa Chadema kutohudhuria Arobaini mbona yeye hakuhudhuria mazishi ya mumewe!...kuna kosa hapa duniani kwa mke wa marehemu kutohudhuria mazishi ya mumewe?...unless huyu mama Marium hatambuliwi na familia ya marehemu kwa hiyo kuna utata mkubwa ktk ndoa hii, laa sivyo angekuwepo Tarime kama mjane wa marehemu.
 
Wanabodi,

Binafsi sidhani kama kuna kitu kimeharibika hapa kiasi kwamba lawama ziwe za chama.
Nimesoma maelezo ya Dr.Slaa na inaonyesha wazi kwamba amekuwa akisisitiza kulingana na madai ya Marium kuwa yeye pamoja na viongozi wote wa Chadema walialikwa Hitma (Arobaini) kama watu binafsi..
Na ndio Utaratibu wakidunia huwezi kualika watu msibani kutokana na nyadhifa ama mtazamo wao kichama...Watu hualikwa msibani ama ktk harusi kama watu binafsi na familia zao..
Kuna misiba kibao ya viongozi wa juu CCM wameondoka na hatukuona viongozi wa chama wakihudhulia (Arobaini) wala sio swala la kulaumu hata kidogo kwa sababu hitma haikamiliki kwa kuhudhulia viongozi ama vigogo isipokuwa dua za watu ndio hitma yenyewe.. Again, bado inatuonyesha sisi kuwa waafrika bado kabisa tunaamini na kuabudu zaidi watu badala ya maandiko - neno la Mungu.

Kwa hiyo, hili linajibu swali la Marium anapojaribu kuhusisha msiba na siasa za chama. Na Dr.Slaa aliposema hamtambui Marium kama ni mke wa Marehemu ni mawazo yake Dr.Slaa binafsi na pengine anazo sababu za kuweka madai hayo..Yawezekana kabisa kuwa Marium kaolewa nje ya sheria hizo hizo mnazotaka kumfunga Dr. Slaa..Sina hakika Marium ni dini gani lakini yanipa fikra tofauti hapa kuwa yawezekana wamefunga ndoa Halmashauri ya jiji, kienyeji, msikitini ama kanisani.
Kisheria ni hadi pale ndoa hiyo imekuwa registered ndipo hutambuliwa kisheria kwa sababu hizo option zote za kufunga ndoa hazihalalishi ndoa isipokuwa pale inapokuwa registered. Mara nyingi watu wengi hufikiria kwamba wakienda kuoana katika Ofisi za Halmashauri. msikitini ama kanisani basi ndoa zao zimefuata sheria..
Pili yawezekana kabisa kwamba Marium alitambulishwa kwa baadhi ya viongozi wa Chadema na sio yeye kwani nina hakika kabisa kuwa hata Kikwete leo hii pamoja na kwamba ana mke wa pili wapo viongozi wa juu CCM hawafahamu wala hawajapata kujulishwa..Hivyo siku huyu mkewe akitoa madai fulani yanayokilenga chama ni muhimu afahamu nafasi yake pia inaweza kupingwa na baadhi ya viongozi... Kwa sababu hawamtambui kama ni mke wa rais hata kama habari hizi wamezipata kupitia vyombo vya habari.

Mwisho kama utasoma vizuri habari hii kama ilivyoandikwa, inaonyesha wazi ni viongozi wa Chadema waliosema Dr. Slaa anatakiwa kumwomba radhi Marium.. hivyo kwa nini lawama hizi zinawashukia Chadema kama chama..
Kabla huyu mama hajajitokeza ktk vyombo vya habari kuna mmoja webu alimfahamu huyu mama?...yeye analalamikia viongozi wa Chadema kuhusu Arobaini mbona yeye hakuhudhuria mazishi ya mumewe!...kuna kosa hapa duniani kwa mke wa marehemu kutohudhuria mazishi ya mumewe?...unless huyu mama Marium hatambuliwi na familia ya marehemu kwa hiyo kuna utata mkubwa ktk ndoa hii laa sivyo angekuwepo Tarime kama mjane wa marehemu.

Highlighted says it all, kama ni kweli hakuhudhuria mazishi hii kali asipige kelele kwenye 40...
 
Wanabodi,


Mwisho kama utasoma vizuri habari hii kama ilivyoandikwa, inaonyesha wazi ni viongozi wa Chadema waliosema Dr. Slaa anatakiwa kumwomba radhi Marium.. hivyo kwa nini lawama hizi zinawashukia Chadema kama chama..
Kabla huyu mama hajajitokeza ktk vyombo vya habari kuna mmoja wenu alimfahamu huyu mama kama mjane wa marehemu?....

Viongozi gani wa CHADEMA waliosema hayo? Hebu tupeni majina na nafasi zao kama ni wasemaji wa CHADEMA. Isije ikawa kama kawaida yao mafisadi wanavika mtu cheo hapo kuwa msemaji wa CHADEMA muhuni tu wa mtaani na wote mnaingia mkenge!

Asha
 
Namtafuta Mwarabu wa Tabora, tajiri mmoja hivi aliyezaa watoto wawili na Mariam ambaye baada ya kufilisika Mariam alimuacha na kukimbilia kuolewa na Wangwe. Kuna maneno Mariam ameyasema leo, nataka sana kuongea na huyu mwarabu kupata kauli yake. Nisaidie namba yake tafadhali. Hili suala libaki kwenye siasa kwa kuwa kuna kauli nzito imetolewa kuhusu Samuel Sitta na siasa za Tabora.

PM

Heee. Jamani, ni kweli kuwa Mariam alimuacha mumewe mwenye watoto naye wawili halafu akaenda kuolewa na mwanaume mwingine aliyekuwa na wake wawili tayari? Au mnataka tu kutunyanyasa kijinsia? Kuna mtu mwenye namba ya Mariam Mwanakijiji afanye naye interview?

Asha
 
Asha Abdalla,
Utanisamehe, kulingana na mwandishi kwani huyo Beatrice ni nani?
Kisha elewa nachozungumza hapa kabla hujarukia ngamia huyu..
Binafsi sioni kosa hata kama ni viongozi wa Chadema kwa sababu ni wao wameliona kosa na wanakumbuka kwamba Marehemu kisha wahi kuwatambulisha..
Kwa hiyo sioni kosa la kuweza kukilaumu chama kizima wakati ni chama hicho hicho kilicho tufahamisha kuhusiana na Marium kutambuliwa kama ni mke wa marehemu.
 
Wanabodi,

Binafsi sidhani kama kuna kitu kimeharibika hapa kiasi kwamba lawama ziwe za chama.
Nimesoma maelezo ya Dr.Slaa na inaonyesha wazi kwamba amekuwa akisisitiza kulingana na madai ya Marium kuwa yeye pamoja na viongozi wote wa Chadema walialikwa Hitma (Arobaini) kama watu binafsi..
Na ndio Utaratibu wakidunia huwezi kualika watu msibani kutokana na nyadhifa ama mtazamo wao kichama...Watu hualikwa msibani ama ktk harusi kama watu binafsi na familia zao..
Kuna misiba kibao ya viongozi wa juu CCM wameondoka na hatukuona viongozi wa chama wakihudhulia (Arobaini) wala sio swala la kulaumu hata kidogo kwa sababu hitma haikamiliki kwa kuhudhulia viongozi ama vigogo isipokuwa dua za watu ndio hitma yenyewe.. Again, bado inatuonyesha sisi kuwa waafrika bado kabisa tunaamini na kuabudu zaidi watu badala ya maandiko - neno la Mungu.

Kwa hiyo, hili linajibu swali la Marium anapojaribu kuhusisha msiba na siasa za chama. Na Dr.Slaa aliposema hamtambui Marium kama ni mke wa Marehemu ni mawazo yake Dr.Slaa binafsi na pengine anazo sababu za kuweka madai hayo..Yawezekana kabisa kuwa Marium kaolewa nje ya sheria hizo hizo mnazotaka kumfunga Dr. Slaa..Sina hakika Marium ni dini gani lakini yanipa fikra tofauti hapa kuwa yawezekana wamefunga ndoa Halmashauri ya jiji, kienyeji, msikitini ama kanisani.
Kisheria ni hadi pale ndoa hiyo imekuwa registered ndipo hutambuliwa kisheria kwa sababu hizo option zote za kufunga ndoa hazihalalishi ndoa isipokuwa pale inapokuwa registered. Mara nyingi watu wengi hufikiria kwamba wakienda kuoana katika Ofisi za Halmashauri. msikitini ama kanisani basi ndoa zao zimefuata sheria..
Pili yawezekana kabisa kwamba Marium alitambulishwa kwa baadhi ya viongozi wa Chadema na sio yeye kwani nina hakika kabisa kuwa hata Kikwete leo hii pamoja na kwamba ana mke wa pili wapo viongozi wa juu CCM hawafahamu wala hawajapata kujulishwa..Hivyo siku huyu mkewe akitoa madai fulani yanayokilenga chama ni muhimu afahamu nafasi yake pia inaweza kupingwa na baadhi ya viongozi... Kwa sababu hawamtambui kama ni mke wa rais hata kama habari hizi wamezipata kupitia vyombo vya habari.

Mwisho kama utasoma vizuri habari hii kama ilivyoandikwa, inaonyesha wazi ni viongozi wa Chadema waliosema Dr. Slaa anatakiwa kumwomba radhi Marium.. hivyo kwa nini lawama hizi zinawashukia Chadema kama chama..
Kabla huyu mama hajajitokeza ktk vyombo vya habari kuna mmoja wenu alimfahamu huyu mama kama mjane wa marehemu?...yeye analalamikia viongozi wa Chadema kutohudhuria Arobaini mbona yeye hakuhudhuria mazishi ya mumewe!...kuna kosa hapa duniani kwa mke wa marehemu kutohudhuria mazishi ya mumewe?...unless huyu mama Marium hatambuliwi na familia ya marehemu kwa hiyo kuna utata mkubwa ktk ndoa hii, laa sivyo angekuwepo Tarime kama mjane wa marehemu.

Mkandara,
Nakubaliana karibu na yote uliyoyandika juu ya hili.

Hivi ni kweli huyu mama hakwenda kwenye mazishi ya mumuwe Tarime? Sijawahi kusoma popote kama hakwenda.
 
Asha Abdalla,
Utanisamehe, kulingana na mwandishi kwani huyo Beatrice ni nani?
Kisha elewa nachozungumza hapa kabla hujarukia ngamia huyu..
Binafsi sioni kosa hata kama ni viongozi wa Chadema kwa sababu ni wao wameliona kosa na wanakumbuka kwamba Marehemu kisha wahi kuwatambulisha..
Kwa hiyo sioni kosa la kuweza kukilaumu chama kizima wakati ni chama hicho hicho kilicho tufahamisha kuhusiana na Marium kutambuliwa kama ni mke wa marehemu.

Jamani, mi sijasoma. Nitajie basi jina la huyo kiongozi wa CHADEMA na nafasi yake. Isije ikawa ni wale wanaojipachika vyeo na kujiita wasemaji wa chama ngazi yao kumbe ni gelesha.

Asha
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom