Marekani yatambua kuwa bila mawasiliano na China ni vigumu kufanikisha utatuzi wa changamoto zinazoikabili dunia

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111464510405.jpg


Muda mfupi baada ya mkutano kati ya Rais Xi Jinping na Rais Joe Biden wa China kukutana na kufanya mazungumzo mjini San Francisco nchini Marekani wachambuzi na wadau mbalimbali wa mambo ya siasa na uchumi wamekuwa wakitafsiri umuhimu wa mkutano kati ya viongozi hao wawili, na matokeo yake kwa hali ya usalama, uchumi na hata siasa za kimataifa.

Mmoja kati ya wanasiasa waliokuwa wa kwanza kupongeza kukutana kwa Rais Xi Jinping wa China na Rais Joe Biden wa Marekani alikuwa ni gavana wa jimbo la California, Bwana Gavin Newsom aliyewapokea marais hao wawili katika jimbo analoliongoza na kutaja kuwa kukutana kwa viongozi hao wawili ni jambo muhimu sana kwa uchumi wa dunia, na pia ni jambo muhimu sana katika kutatua changamoto za mabadiliko ya tabia nchi.

Akiongea kuhusu umuhimu wa Rais Xi na Rais Joe Biden kukutana, Gavana Gavin Newsom amesema China na Marekani ni nchi zinazoongoza kiuchumi, pamoja na kuwa hakuna kitu kinachoitwa G2 kama ilivyo kwa G7 na G20, kiuhalisia ni kwamba kukutana kwa viongozi hao kunaweza kuchukuliwa kuwa ni mkutano wa G2, kwani mambo kuhusu uchumi wanayojadili viongozi wa nchi hizo mbili, ikiwa ni pamoja na makubaliano na tofauti kati yao, vinakuwa na matokeo kwa nchi nyingine zote.

Moja kati ya mambo muhimu ambayo Gavana Newsom aliyotaja ni suala la mabadiliko ya tabia nchi. Alisema hakuna uwezekano wa kupiga hatua yoyote kwenye kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi hata nchi zote duniani zikichukua hatua kwa pamoja, bila ushiriki wa China na Marekani, ambazo kwa pamoja huzalishwa zaidi ya asilimia 40 ya hewa zinazosababishwa kuongezeka kwa joto duniani. Lakini hata ukubwa wa uchumi wa nchi hizi mbili peke yake unakaribia nusu ya ukubwa wa uchumi wa dunia nzima, kwa hiyo kukutana kwa viongozi hao ni muhimu sana kwa dunia nzima.

Mwanahabari wa gazeti la the Guardian la Uingereza Bw. Christopher S Chivvis, amempongeza sana Bwana Joe Biden kwa kukutana na Rais Xi Jinping, na kusema Bw. Biden kufanya mazungumzo na Rais Xi Jinping katika mazingira yasiyo rafiki ya siasa za ndani za Marekani, kunaonesha juhudi za Rais Biden na serikali yake kurekebisha makosa ya mtangulizi wake ya kuweka uhasama na China, bila kujua kufanya hivyo ni kuhatarisha usalama wa Marekani yenyewe na dunia nzima kwa ujumla.

Wakati dunia ilipokuwa na ncha mbili, lilikuwa jambo rahisi kwa Marekani kuzipuuza nchi ilizoziona kuwa haziendani na mfumo inaotaka au haziendani na matakwa ya Marekani, lakini nchi hizo zilikuwa ni nchi ndogo ndogo na zenye uchumi mdogo, China ni tofauti kabisa ambayo haiwezi kupuuzwa. Bwana Biden kutambua hili ni moja kati ya mambo muhimu ya kuangalia namna ya kutatua changamoto za uchumi wa dunia au hata kuweka sawa mambo ya dunia.

Ni wazi kuwa China na Marekani ni nchi kubwa zenye nguvu zaidi ya kiuchumi duniani, na nchi hizi mbili zina mitazamo tofauti kwenye baadhi ya mambo, lakini kukaa na kuzungumza kumeonekana kuwa ni njia nzuri inayoweza kuondoa changamoto, kwa kuwa si kila nchi inakubali kuburuzwa kama ilivyozoeleka kwenye miaka ya nyuma.
 
Back
Top Bottom