Mkuu watu wengine sijui wanaishi Dunia gani? Haya mambo ya kujitia masikini jeuri hayatatufikisha popote!
Tusipokuwa makini suala la Zanzibar linaweza kufuta sifa zote nzuri za Taifa letu pamoja na Serikali ya JMT, may be Serikali ya Zanzibar inajiona hawana cha kupoteza ndio maana wanaonekana kutojali maoni ya International Community - lakini wakae wakijua kwamba stance ya Serikali ya Zanzibar kuhusu kurudiwa tena uchaguzi zitamwaribia sana Dk.Magufuli kimataifa.
Ni jambo lililo wazi wanataka kulazimisha mambo na kuiweka Tanzania kwenye hali tete, kama matokeo ya vituo karibu 30+ matokeo yake yalisha bandikwa ukutani kulikuwa na ulazima gani wa kufuta uchaguzi? Kwani kuna ulazima gani wa Chama tawala kushinda Bara na visiwani, Watanzania si wanabaki wale wale bila ya kujali itikadi ya vyama vyao, mbona manispaa za Ilala na Kinondoni zinaongozwa na Mameya wa vyama vya Upinzani - kwani kuna kitu gani kilicho haribika.
Tufike mahali tukomae kisiasi tusipalilie vurugu na machafuko yasiyo ya lazima - na ukiangalia kwa umakini wanao palilia sintofahamu wengi umri wao umekwenda wanategemea vijana watajifunza/rithi kitu gani cha maana kutoka kwao.
Narudia tena kusema kwamba wasitake kulingiza Taifa letu pamoja na Dk.Magufuli katika hali ngumu, tutakuja kutengwa Kimataifa na kuwekewa vikwazo tukaponzwa na misimamo yenu hisiyo eleweka/yenye utata mtupu, tukumbuke hasiye kubali kushindwa simshindani.