Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Tajiri akifilisika MASKINI NDIO HUANZA KUFA, umeandika kiushabiki shabiki hivi na kama unaombea hayo yatokee haraka!
Kumbuka hako kamsemo hapo juu na katafakari.
 
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!

Hatuwezi kuishi kwa misaada pekee ....na inatakiwa kuulinda uhuru wetu kiukweli!!

UHURU wa kupora ushindi wa wazanzibar ndo mnaolinda nyie MAJIPU shida sana.

Alafu unajua misaada kiasi gani TZ tunawezafunga kupitia NGO zilizoajili watanzania wanaolipa PAYE?
 
kuna watu humu wanatetea uovu wa ccm badala ya kuangalia maslahi yetu kama taifa...tz tukiwekewa sanctions manayake sio tu kunyimwa misaada hata kufanya biashara na mashirika ya nje ya nchi hakuna......kampuni yoyote inayofanya kazi na Tanzania inapigwa ban marekani....iran baada ya sanctions kuisha juzi raisi wao bila kupoteza muda amekimbilia ulaya kutafuta wawekezaji na kununua ma ndege jinsi hali ilivokua ngumu, wana gesi nyngi walikua hawajui pa kuipeleka..leo hii kuna mburula humu wanakwambia sanctions sio tatizo tutarudi enzi za ujamaa yaani nchi badala ya kusonga mbele tunarudi nyuma kwenye ujamaa...ccm magufuli angalia maslahi ya nchi kwanza sio ccm
 
Nadhani tuchukue ile Nafasi aliyoiacha Iran Juzi juzi ya kuishi kwa Vikwazo... Cuba alikaza sana baadae kaona ni Ujinga kisa kiongozi wao alikuwa mbabe so wananchi ndio waliteseka... Kile kikundi cha kina Vuay na Kapteni wa Meli ndio Tatizo... maana wao ndio wanajiona zanzibar ndio yao hao wawili
 
EU na america ndio tunawategemea kiuchumi ktk utalii na misaada, sasa sijui hata soko la nje tutauziaa wap
Tatizo we mkuu Ibilisi inaelekea ni miongoni mwa watu wasiofuatilia mambo kwa karibu.
JPM anajenga Tanzania ya viwanda hivyo miaka kama miwili ijayo kama sio miezi sita kuanzia sasa, sisi tutakuwa main exporters kwenda kwa EU, USA na kwingineko na usije shangaa bandari ya Dar es Salaam itakuwa imejaa makontena ya export hata wezi wa makontena hawatakuwa na cha kuiba ndugu!
 
Hayo mazao kama mchele na mahindi na maharage unayokula huwa yanazalishwa na mabwana zako wa kizungu?
Hayo mahindi na mchele yanawasaidiaje ili kuongeza pato la taifa ? Au ni kula na kuongeza uchafu hapo Dar.?
Ngoja upigwe sanction kama utaweza hata kupata pembejeo za kulima hayo mahindi unayoyasema
 
Taifa la Marekani linatarajia kushusha rungu la aina yake kwa serikali ya Tanzania kufuatia hali ya sintofahamu inayoendelea nchini kutokana na sakata la uchaguzi mkuu wa Zanzibar.

Habari zinadokeza kuwa taifa hilo kubwa duniani litaweka vikwazo vya kiuchumi kwa Tanzania hali itakayopelekea Tanzania kuandika historia nyingine mbaya mbele ya uso wa dunia.
Serikali ya Marekani tayari imezuia misaada mbalimbali kwa Tanzania na pia ndiyo iliyoshinikiza Tanzania kunyimwa fedha za MCC. Hata hivyo serikali ya Tanzania bado haijatilia maanani jambo hilo huku ikioneknana kupuuza juhudi za kimataifa kuitaka kuumaliza kwa haraka mgogoro wa Zanzibar unaofukuta kwa kuacha haki ichukue mkondo wake.
Habari zinadokeza kuwa balozi wa Marekani nchini atatoa msimamo unaoelezwa kuwa 'mkali' ili kuishinikiza serikali ya Tanzania kuheshimu maamuzi ya wananchi kwenye uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika mwezi october mwaka jana ambao ulielezwa kuwa huru na wa haki.
Watuwekee tu vikwazo ili tuwasue viongozi maana watanzania ni waoga sana isee
 
hiyo misada ya mcc wabaki nayo kwasasa tanzania hatuitaki hata hivyo sisi siyo vilema wa kusaidiwa,hiyo misaada wawape mashoga wa hukohuko
 
Hivi kuna kitu tunategemea wamarekani wasipotupa tutakufa? maana naona kama vyakula tunalima wenyewe na ndio tunavyoishi, biashara tunafanya za kwetu ndani ya afrika mashariki na tukikomaa zaidi tunakwenda kwa marafiki zetu china, tumeanza kuthibiti mapata yetu ya ndani , kama mbwai na iwe mbwai sema no 2 ombaomba. Kama ni neti za mbu wala hazikutusaidia lolote kwani tulibadilisha matumizi na kuwa nyavu za kuvulia samaki , fensi za bustani na vibanda vya kutunzia vifaranga vya kuku
 
Hayo mahindi na mchele yanawasaidiaje ili kuongeza pato la taifa ? Au ni kula na kuongeza uchafu hapo Dar.?

Maskini wee hata hujui mambo ya uchumi.Pato la taifa unalipataje? ni pamoja na kujumlisha mapato yote waliyopata wakulima kwa kuuza mazao yao ya mahindi na mchele.Ukiwa kibaraka wa wazungu hata hujitambui na hukitambui cha kwako kinachangiaje pato la taifa!!!! Pole
 
Japo misaada sio jambo la kushabikia, kwa nchi maskini kama zetu lakini pia kwa baadhi ya nchi zilizoendelea, haikwepeki!

Kwa wanaofikiri tutaweza kusonga mbele wenyewe bila misaada wanaweka mbele ushabiki wa KISIASA. Ni vizuri wakajiuliza kwa nini nchi kama Iran pamoja na kuwa na hazina kubwa ya Mafuta na hata kuwa na maendeleo kuliko sisi, baada ya kuwekewa vikwazo, wamelegeza misimamo!

Vikwazo vina athari kubwa, tufikirie nje ya BOX!!
 
Nasemaje, wafute tu misaada yote, tutafute kwa jasho letu... watu wanaitumia hiyo misaada vibaya sana... Kuna project nyingi sana chini ya USAID zinazotakiwa zilipe wafanyakazi mishahara mikubwa sana... lakini unakuja kupewa punje punje tu zote wanachukua hao wanaaojita wakubwa...
mkuu elewa kitu kimoja hiyo misaada inaweza ikafutwa sawa tukajitaidi uzalishaji
hata kama
lkn kama NIGGERS walijitoa kimasomaso kujitoa utumwani mikononi mwao enzi hizo katika nchi yao sembuse sisi zama hizi tatzo kubwa waafrca tuna uroho wa madaraka na ndo mwanya anaoutumia mzungu kututawala yeye atajifanya yupo upande wa mnyonge kukusaidia kumbe anapenyeza yake(kama sasa znz)
kama mababu zetu waliziazisha njia za kumtoa mkoloni afrca kwann sisi tusiendeleze hizo mbio kwa kufanya ubaki uhusiano wa kibiashara tu wenye masilah kwa pande zote mbili kutokana na mkataba unavyoeleza kuliko kukaa kutegemea hao jamaa mfano nchi nyingu tungekaza uzi kuwa ka mugabe wangenyooka tu coz AFRICA ka kisima cha shamba rukaruka lkn lazima uje tu kisiimani
pumbavu zao WHITEFORKS
mkuu tutafoutishe msaada na vikwazo vya kiuchumi na misaada. tunaweza tukanyimwa misaada halafu tukatafuta njia ya kurecover hilo tatizo. shida ni pale unapoekewa vikwazo vya kiuchumi kiasi cha kwamba kuuza ama kununua vitu nje ni ngumu kiuhalisia hali itakuwa ni ngumu tena kwa nchi kama yetu ni bado sana. mfano irani sidhani kama wenyewe walihitaji msaaada wa fedha toka nje ila vikwazo vya kiuchumi vinawaasili hata kwa bidhaa ambazo unazalisha mwishowe mwenyewe unakaa mfano mwingine ni zimbabwe.
 
Sawa hata kama ni siasa zimetujaa lkn Mchaga hawezi tawala hii nchi, labda aende Kenya!
Mchaga katokea wapi hapa au anahusika vp na hii mada?
Ianzishie uzi labda utapata wachangiaji.
 
Tatizo we mkuu Ibilisi inaelekea ni miongoni mwa watu wasiofuatilia mambo kwa karibu.
JPM anajenga Tanzania ya viwanda hivyo miaka kama miwili ijayo kama sio miezi sita kuanzia sasa, sisi tutakuwa main exporters kwenda kwa EU, USA na kwingineko na usije shangaa bandari ya Dar es Salaam itakuwa imejaa makontena ya export hata wezi wa makontena hawatakuwa na cha kuiba ndugu!
Kiongozi unaposikia wanasiasa wanasema TZ itakuwa nchi ya viwanda usifikiri hili littakuwa kwa kipindi cha miaka miwili au mitatu labda km tunazungumzia viwanda vya kurecyle chupa ila viwanda vikubwa inaweza chukua hata miaka 5au zaidi mfano dandote ulizia leo ni mwaka wa ngap?
 
Back
Top Bottom