Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Kwa msaada wa watu wa Marekani......hao hao wamarekani ndio waliotumia kila njia mpaka tukaungana na Zanzibar mwaka 1964, lakini kwa sababu tishio la ukomunisti limekwisha hata muungano wetu kwao umepoteza umuhimu. Hizo ndizo siasa za dunia hii, zimekaa kimaslahi zaidi. DR Congo vita haviishi kwa sababu ya utajiri ambao Mungu ameijalia nchi ile, lakini siku madini yakikata wazungu na wavamizi wengine wote wataondoka. Ujanja ni kama alisema Mwalimu Nyerere, kujitegemea kwa kila hali.
 
Maskini wee hata hujui mambo ya uchumi.Pato la taifa unalipataje? ni pamoja na kujumlisha mapato yote waliyopata wakulima kwa kuuza mazao yao ya mahindi na mchele.Ukiwa kibaraka wa wazungu hata hujitambui na hukitambui cha kwako kinachangiaje pato la taifa!!!! Pole
Hahahaha!!! Kibaraka ni wewe na viongozi wako mnaopokea misaada.

JK alikwambia ukienda huko nje hela zipo nyingi tu ukiwaomba wanakupa misaada.

Kama pato la taifa limeongezeka vipi deni la taifa nalo limekwea namna hiyo??
Mlikopa zaidi au mliongeza pato kwa sana?
 
Nenda rudi! Mzungu bado ni bora sana Afrika! Ata ufanye nini, huruki! Mtalii ni Mzungu!. Kuuza bidhaa nje ni Mzungu anausika.Kununua vitu nje Mzungu anausika. Irani na ubishi wao wote Vikwazo vya wazungu walikubali kushindwa.Ayatollah Khomeini na dini ilivyomjaa lakin kaufyata.Wana Mafuta ya kutosha lakini walikua hawauzi nje zaid ya kuiuzia India kwa asilimia 5% tu.Wakajadili wakakubali ya kwamba bado Mzungu ni nomaaa.Mzungu akisema hununui wala huuzi, Mchina mwenyewe anasanda.Usijidanganye duniani kubali yaishe!!.
 
Taifa la Marekani linatarajia kushusha rungu la aina yake kwa serikali ya Tanzania kufuatia hali ya sintofahamu inayoendelea nchini kutokana na sakata la uchaguzi mkuu wa Zanzibar.

Habari zinadokeza kuwa taifa hilo kubwa duniani litaweka vikwazo vya kiuchumi kwa Tanzania hali itakayopelekea Tanzania kuandika historia nyingine mbaya mbele ya uso wa dunia.
Serikali ya Marekani tayari imezuia misaada mbalimbali kwa Tanzania na pia ndiyo iliyoshinikiza Tanzania kunyimwa fedha za MCC. Hata hivyo serikali ya Tanzania bado haijatilia maanani jambo hilo huku ikioneknana kupuuza juhudi za kimataifa kuitaka kuumaliza kwa haraka mgogoro wa Zanzibar unaofukuta kwa kuacha haki ichukue mkondo wake.
Habari zinadokeza kuwa balozi wa Marekani nchini atatoa msimamo unaoelezwa kuwa 'mkali' ili kuishinikiza serikali ya Tanzania kuheshimu maamuzi ya wananchi kwenye uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika mwezi october mwaka jana ambao ulielezwa kuwa huru na wa haki.

HESHMA YA NCHI INALINDWA KWA KUSIMAMIA UHURU NA TARATIBU ZAKE. IFIKE MAHALI TUACHANE KUSHABIKIA MISAADA NA TUJIJENGEE UTANADUNI WA KULIPA KODI NA KUKUSANYA MAPATO KWA UADILIFU. TAKWIMU ZA MAPATO YA NOVEMBA NA DESEMBA 2015 ZINAONYESHA TUNAWEZA KUSANYA MAPATO YATAKAYOTOSHELEZA KUTEKELEZA BAJETI YOTE. JINAMIZI MISAADA NI WAKALA WA UMASKINI NA UTUMWA WA KIFIKRA. TUNA KILA KITU NA MH. RAIS ANADHAMIRA YA DHATI. TUULINDE UHURU WA TANZANIA NA TUULINDE MUUNGANO WETU KWA NGUVU ZOTE. MAPINDUZI YA ZANZIBAR HAYANA BUDI KULINDWA NA KUHESHIMIWA KWA GHARAMA YOYOTE MAANA NDIO FAHARI YA KILA MZANZIBARI NA ISHARA YA UHURU WAO NA VYOMBO VYAO VYA MAAMUZI.
 
Hivi kuumaliza mgogoro ni kuwapa madaraka cuf...?!
Kuumaliza mgogoro ni kumtangaza mshindi kwa nafasi ya urais kwa uchaguzi uliofanyika 25.10.2016 ambao CCM walitumtumia Jecha na majeshi kutengeneza mkwamo.

Kwa Mwenyekiti wa ZEC kushindwa kumtangaza mgombea wa CCM kuwa ni mshindi katika nchi ambayo "CCM ni nambari one" ni muujiza iliotokea tarehe 28.10.2015.

Hivi utaumalizaje mkwamo kama sio kuruhusu mkwamo uondoke?

Link Msaada: Nini kitatokea iwapo CUF hawatashiriki uchaguzi wa marudio Zanzibar?
 
nitaona ajabu nchi kama marekani kutokufuata katiba kanuni sheria za nchi husika
Wanasimamia Katiba za nchi zisizojielewa. Kifungu gani katika sheria ya Zanzibar kinaruhusu kufutwa uchaguzi na kufanya marudio.?
 
Mgogoro uishe haraka,wanamaslahi gani kwani?
Mashauriano huwa hayaendi haraka haraka.
 
Enyi kizazi cha nyoka, mnaopenda misaada na hisani za wafadhili yawapasa mbadilike.

Kama taifa, tusiruhusu kuvurugwa na watu kutoka nje.
Watoto watano wa Tanzania wenye ulemavu wa ngozi waliokuwa wamekatwa viungo vya miili yao wamewekewa mikono na miguu ya bandia katika hospitali iliyopo nchini Marekani. Watoto hawa ni miongoni mwa mamia ya watu wanye ulemavu wa ngozi nchini humo ambao wamekuwa wakiwindwa na watu wanaotaka viungo vya miili yao kwa shughuli za kishirikina Watoto hao, mmoja wa kike na wanne wa kiume kutoka mikoa ya Kaskazini Magharibi na Kusini Magharibi mwa Tanzania, wamekuwa wakipokea matibabu hayo katika hospitali ya watoto Philadelphia Shriners Hospital iliyopo jijini New York.

Link 1. Albino 5 Tz warejeshewa viungo Marekani - BBC Swahili

Link2. Watoto Albino wapatiwa viungo marekani - BBC Swahili
 
Nasemaje, wafute tu misaada yote, tutafute kwa jasho letu... watu wanaitumia hiyo misaada vibaya sana... Kuna project nyingi sana chini ya USAID zinazotakiwa zilipe wafanyakazi mishahara mikubwa sana... lakini unakuja kupewa punje punje tu zote wanachukua hao wanaaojita wakubwa...
nadhani hujaelewa maana ya sanction,sio misaada tu bali hakuna kuuza wala kununua kwa nchi washirika wa marekani sasa pamba yako utamuuzia nani,tanzanite yako utapigia ndege
 
kwan bila marekani tutakufa njaa
japo siafik ubakaji wa demokrasia uko ZNZ lkn shobo za kuwashobokea WHITE FORKS sizipendi kinoma mbna KOREAKASKAZINI wameweza bila marekani japo wakati wanaanza kukaza uzi walibezwa sana najua HATUWEZI KUJIFANANISHA NA KOREA KASKAZINI ila zama za sasa tujitengenezee mazingila ya kujitegemea wenyewe muda ndo huu wa kujenga nchi yetu TANZANIA afrca kwa ujumla tufufuke tuache uchu wa MADALAKA wangapi wababe walikuwapo leo awapo duniani
koba
MOBUTU SESESEKO JONAS SAVIMBI SANKARA wako wapi wamefukiwa na Bado maisha yanaendelea dunia tunapita tu
 
nisawa kushinikiza serikali kusimamia demokrasia. Haina maana kuisaidia nchi alafu kesho wanapigana vita na kaharibu vyote mlivyowasaidia!
mataifa yanayotusaidia yawabane hawa viongozi wetu ili tuepuke majanga.
Wao wanatusaidia kwa hela ya walipakodi huko kwao ajabu huku hatukusanyi hiyo kodi ili nasisi tujisaidie. Tunaskia tuu mara lake oil mara azam...iv serikali iliyopita iliwezaje kuwa dhaifu kiasi hiki? Maana ata roho itakusuta kuacha kampuni kuubwa na kukimbilia kodi ya vigenge vya kinamama.
 
Kwani tunazungumzia vikwazo vya kiuchumi? au tunazungumzia kusitishiwa misaada? tujue utofauti wa hivi viwili ndipo tuongelee kujitafutia na kujitegemea....🙁
 
nadhani hujaelewa maana ya sanction,sio misaada tu bali hakuna kuuza wala kununua kwa nchi washirika wa marekani sasa pamba yako utamuuzia nani,tanzanite yako utapigia ndege

Nchi za kifaransa na wachina...
 
Mimi nasema Marekani na nchi nyingine zote ziondoe misaada yake haraka iwezekanavyo. Ni aibu kwa nchi tajiri kama hii kutegemea misaada kwa Marekani na nchi nyinginezo wakati kuna watu wanaingia bidhaa nchini bila kulipa, huku wahusika waliopewa thamana ya kulinda maslahi ya Watanzania, wakishirikiana nao kutuhujumu!

Wafunge virago vyao! Tubaki na nchi yetu. Misaada hiyo inawanufaisha wao, sio sisi.

Tutatue migogoro yetu wenyewe, uwezo huo tunao.
 
Inawezekana s/kali ya Jk ndo mbovu kuliko zingine zote zilizopita.Lakini kwa muda huu mfupi s/kali ya awamu ya 5 iliyokaa madarakani wameonesha udhaifu kiasi kwamba watu wenye akili nzuri na wenye maono ya mbali wanaona kwamba ndo itaku Mbovu kuliko hata ile iliyopita.2020 si mbali
 
Back
Top Bottom