Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

pitia post vizuri mkuu najua fika siwezi linganisha nayo 7bu yenyewe inajitegemea zaidi kwa soko la ndani nimejalibu kuelezea tu ni vipi tukiamua tunaweza
Kha! mnaweza nini? watu mna import mpaka njiti ya kiberiti halafu unajidai mkiamua, amuweni basi.
 
Tuishauri serikali vizur! Kama kikombe cha vikwazo kinaepukika ni vyema tukakiepuka, la sivyo mapenzi ya Mungu yatimizwe
 
Wakitaka waweke vikwazo vya chuma kabisa lakini hawatutishi mbona wameweka vikwazo vingi sana kwa nchi nyingi za afrika lakini zinapeta tu kwani tunategemea nini kutoka marekani manina zao.
 
Kha! mnaweza nini? watu mna import mpaka njiti ya kiberiti halafu unajidai mkiamua, amuweni basi.
Nyie wakenya shida yenu hamnaakili mnadhani Tanzania inamambo ya kijinga kama yenu sisi tutasonga tu.
 
With all due respect, kwa differing opinion ya baadhi yetu, kwanza naheshimu mawazo ya wengi na kuna sehemu tuko pamoja, ile sehemu ya Mhe. Masele hakupaswa kuyasema haya!. Aliyepaswa kuyasema ni MFA, Mhe. Benard Membe!.

Sasa naomba niwarudishe nyuma kidogo, tangu enzi zile za kuupinga mfuko wa Jimbo, kuna "watu" walitoa fedha kwa NGO zikafanya uhamasishaji wa hali ya juu, zikaweka hadi kambi Dodoma wabunge waupinge mfuko wa jimbo, lakini wengi wa wabunge wetu walivyo njaa kali, walivyo walafi, walivyo wachumia matumbo, very few can say no to ulaji!, mfuko wa jimbo ukapita!. TISS wanajua who was behind!, JK anajua!, Membe anajua!, ilikuwa ni kinyume cha Viena Convention!, lakini wote walijinyamazia kimya simply kwa kitu kinachoitwa "Diplomasia!".

Eti huwezi kulikata tawi la mti ulioukalia!, au mkono unaokulisha ukipakwa ma..!, huwezi kuukata!, utausafisha tuu na kuendelea kuutumia kula chakula!, na ikitokea hakuna maji ya kuusafishia, unaufuta tuu na kuulia!, au ufe njaa?!. Hiki ndicho Tanzania tunachokifanya siku zote!. Tumeonewa Kiasi cha Kutosha, Tumenyanyaswa Kiasi cha Kutosha, Tumedhalilishwa kiasi cha Kutosha, Tumepuuzwa Kiasi cha kutosha!. Unyonge wetu ndio umetofanya, tuonewe, tunyanyaswe, tupuuzwe na kudhalilishwa!. Mhe. Masele ametufundisha tunaweza kusema no!.

Lilipokuja suala la gesi asilia, sio wengi humu mnafahamu ni kampuni gani ndilo lenye vitalu vingi na wanaendelea kuomba vitalu!. Hilo kampuni lilipanga wajenge LNG Plant floating kule kule high sea ili watuibie vizuri gesi yetu!. Serikali ilipopitisha uamuzi wa LNG Plant lazima ijengwe on the land!, uamuzi huo ukawa ni pigo kwa mabeberu, wakoloni mambo leo hawa, ambao wameamua kutuibia mchana kweupe!. Ule upinzani wa bomba la gesi ulichochewa ili bomba lisijengwe!, TISS wanamfahamu "mchochezi huyo!", JK anamfahamu!, Membe anamfahamu, Mhongo anamfahamu!, wenye ufahamu, wanamfahamu!, ila wote walimnyamazia kwa kile kile kinachoitwa "Diplomasia ya Beggars Syndrome Cowardice!".

Kwenye hili la gesi, nililizungumza siku nyingi Gesi asili: Is it "day light robbery?!"- Watanzania Tunaibiwa Mchana Kwepee! tangu 27th July 2012 04:34 masikini wana JF, ni wachache wetu wenye uelewa wa baadhi ya haya mambo, thread ile ya iliishia page 1!.

Lilipokuja suala la Bajeti ya Nishati na Madini, "insiders" walijua nini kinachoendelea, bahati nzuri wizara ile sasa imeshikwa na really people who plays real game! na sio kuendelea kuwategemea hawa "kujikomba komba politicians kwa jina la diplomasia!" Mhe. Masele (by nature Wasukuma ni masikini jeuri!, sio watu wa kujikombakomba kwa lolote na kwa yoyote!), akaamua to hell with what is called "diplomsia na kuamua to take the bull by its horns!", kama ni kumuua nyoka!, you start by hitting the head! not the tail, and when you decide to strike, you just hit the target and where it hurts most and not the usual way of beating around the bush!.

Tuhuma zile ni nzito!, zimetolewa bungeni!, nilitegemea au Ikulu ingetoa official statement ku clarify!, na waziri Membe angekuja na kauli ya serikali bungeni!, kama Masele amezungumzia Bungeni, official channel!, kisha Balozi Sefue anajibia "gengeni" huku Membe yuko kimya na sasa Balozi anakuja kujisafisha kwa jinsi walivyotusaidia na watakavyoendelea kutusaidia! badala ya kujibu tuhuma!, unategemea nini?!.

Huu umasikini wetu, uomba omba wetu, utembezaji bakuli wetu, usitufanye tuendelee kudhalilishwa!, wengi mnaujua "uwezo wa JK" na boldness yake ya "udhaifu" and so does Membe!, hawangethubutu!, nilidhani by now Masele angeishafanywa ndiye "kondoo wa kafara!", ikibidi punda afe lakini mzigo ufike!.

Mhe. Masele ameonyesha ushupavu wa hali ya juu sana! na kitendo alichokifanya ni cha kishujaa sana mpaka pale hoja zake ama zitapojibiwa kibunge!, au zipanguliwe hoja kwa hoja na sio kama hali ilivyo sasa hoja zinapanguliwa na viroja! halafu watu wanashangilia ujinga!.

NB. Kama mtaninote sizungumzii kabisa "fedha na escrow account" that is pure bussiness!. Hapa tunazungumzia kitu kinaitwa "patriotism, sovereignty na national pride!", Tanzania is never poor!, huku kuomba omba na kutembeza bakuli kila siku ni tabia!. Gesi ni yetu!, tunabembeleza as if hakuna mwingine yoyote mwenye kuweza kuichimba!.

Tufike mahali Watanzania wote tuwe kama Wasukuma!, ukitendewa visivyo, unasema No! no matter what and you mean no!, Mwanza walisema No to ujinga ujinga, Nyamagana pia wakasema no tu ujinga ujinga!, japo ukabila sio kitu kizuri!, lakini kuna makabila fulani fulani kazi yao ni kujikombakomba tuu, kamwe hawawezi kusema no kwa ujinga ujinga wowote!, hata wafanywe vipi, wao watacheka tuu!, kama huamini shuhudia jinsi baadhi ya omba omba wanapotupiwa pesa na wenye magari, wanavyozikimbilia kwa furaha!, au nenda kampe omba omba noti yoyote huku unamtukana aone atakavyokushukuru!. Hivi ndivyo tulivyo!. ikibidi sasa, tuyahamasishe yale makabila machache ya "no nonsense!" yaseme no kwa ujinga ujinga ndipo tutaweza kutoka humu tulimo vinginevyo we are doomed!!. Mhe. Masele ni shujaa!, ameonyesha njia!, he has the guts to say no to nonsense!.

Wale wengi wenzangu na mimi, wenye high sense of nationalism na patriotism, lets join forces to say no to ujinga ujinga wowote against our sovereignty for restoration of our national Pride!. Nyerere aliweza na kuna wakati aliwagomea Waingereza!, aliigomea IMF na WB, japo watt walivaa magunia na uniform zilikuwa madurufu, but we were proud Tanzanians!.

Yes We Can!.

Pasco

Pasco hongera kwa waraka huu...
 
kwan bila marekani tutakufa njaa
japo siafik ubakaji wa demokrasia uko ZNZ lkn shobo za kuwashobokea WHITE FORKS sizipendi kinoma mbna KOREAKASKAZINI wameweza bila marekani japo wakati wanaanza kukaza uzi walibezwa sana najua HATUWEZI KUJIFANANISHA NA KOREA KASKAZINI ila zama za sasa tujitengenezee mazingila ya kujitegemea wenyewe muda ndo huu wa kujenga nchi yetu TANZANIA afrca kwa ujumla tufufuke tuache uchu wa MADALAKA wangapi wababe walikuwapo leo awapo duniani
koba
MOBUTU SESESEKO JONAS SAVIMBI SANKARA wako wapi wamefukiwa na Bado maisha yanaendelea dunia tunapita tu
Kwenye red=mazingira,madaraka.
 
Wewe ndio huna uhakika, jiandae kuishi kwa kutegemea wahisani, kwa taarifa yako hadi sasa kwa mwezi January mapato yameisha vuka lengo 2trions zishaingia hazina. Wewe wasubiri baba zako commonwealth na wamarekani wakubebe.
Hizo 2trillion zimetoka wapi kwa kulima mahindi hapo msata?!

Au kufanya biashara na nchi nyingine?!

Unajua kama wakiweka vikwazo hata kufika hizo 2trillion itakuwa ni ndoto?!

Unajua au hujui ila unajifanya unajua...?!
 
Kwa miaka mingapi wanavijiji wameishi bila huo umeme?
...Kwahiyo, waendelee kuwa hivyo? Umeme ni sawa na elimu, maji na huduma ya afya. Ni wa muhimu! We hutumii umeme?

Hao wenye umeme kama Dar si lamu wana kipato zaidi ya kinachopendekezwa?
...Kipato kipi kinapendekezwa? We huna umeme?

Uwezo wa kukusanya na kufinance hiyo miradi upo ni upuuzi tu wa tabia za wapuuzi mithili ya hawa wanaolilia mabwana wa kizungu.
...Kumbe unajua! Kwahiyo tuko pamoja, kwamba, umeme ni muhimu, sio?

Solar kwa ajili ya kituo cha afya inaweza kucost sh milioni 6 ...je kiasi hiki kinashindikana mpaka tusubiri msaada wa wazungu?
...Hakuna kinachoshindikana. Ila, kama umeme wa nyaya upo karibu, ni bora kuliko wa solar.
 
Wanaweza kuweka vikwazo lakin si vya kiuchumi...wao wanafaidi zaid kwa kuacha milango ya uchumi kuliko kuifunga...hey...guys kuna china hapo....unadhan ana muda na ccm au cuf huko znz...he is for business....! Sana sana ninachoona mimi ni kwamba watu flanfaln watazuiwa kusafir huko ulaya na marekan...of which si hoja bse pombe walishawawekea watu wake vikwazo...! Think!
 
Ka

Kanuni na sheria za nchi husika zinaeleza wazi utaratibu WA uchaguzi ambao unaanzia kwenye kupiga kura,kuhesabu kura,na kutangaza matokeo ya kura,hakuna kipengele cha kufuta Uchaguzi baada ya kuhesabu kura ilhali process zilizotangulia zilienda kwa uwazi na haki,hivyo basis uchaguzi WA Zanzibar pamoja na procedures zake ulikuwa halali,na hill hata were unalijua,kitu pekee cha haramu kilikuwa no kitendo cha jecha kutangaza kufuta so matokeo tu,Bali uchaguzi mzima,na hicho ndicho kinachowashangaza wafadhili wenu,na hili li jingalao linaropoka eti hatuhitaji msaada,wakati ni viongozi wake ndiyo waliyoifungia hii nchi kwenye utegemezi,wachina wakitupa misaada yenye maslahi kwao munafurahi na kudai hao ni ndugu zenu,mmarekani akiwanyima tonge kwa upuuzi wenu wenyewe munaanza kuongea mbofu mbofu eti nyoo hatuitaji misaada,,kumbaf sana
Hivi maalim seif kujitangaza ilikuwa demokrasia ??

Huo usahihi wa mgombea kujitangaza umeanza lini??

Hata uchaguzi wa mwaka huu tumegharamia ....tunaweza kabisa kujitegemea ni lazima mstari uchorwe....Huko ugiriki wako hoi kiuchumi pamoja na kuwa mababa wa demokrasia sasa wewe unatuletea mbwembwe za kulilia waume wa kizungu...!!dunderhead
 
...Kwahiyo, waendelee kuwa hivyo? Umeme ni sawa na elimu, maji na huduma ya afya. Ni wa muhimu! We hutumii umeme?


...Kipato kipi kinapendekezwa? We huna umeme?


...Kumbe unajua! Kwahiyo tuko pamoja, kwamba, umeme ni muhimu, sio?


...Hakuna kinachoshindikana. Ila, kama umeme wa nyaya upo karibu, ni bora kuliko wa solar.
Hebu jitulize ndio unijibu...!

Nakuuliza tena ...leo hii huko vijijini umeme hamna wanaishije?

Hapo Dar ulipo umeme ukikatika unaishije?

Usiifanye umeme kama basic need ya kuuza utu na uhuru wako...yaani wewe unaweza toa hata ule mtandao kwa ahadi ya umeme tu!!

Pato la mtu wa Dar salaam(kwenye umeme) kwa sasa lina utofauti wa maana ukilinganisha na pato la mtu wa Rombo au Hanang??

Issue hapa ni kutokuwekewa conditions wakati sisi ni Taifa huru...na kwa msingi huo machi 20 itapita salama na wakazi wa Zanzibar wataendelea na maisha yao kama ilivyo sasa halafu na nyie vibaraka mnaotaka kuuza nchi tutawasamehe tu!!


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
Kwa hiyo siku hizi ukitaka kushinda uchaguzi unawahi kujitangaza???

Hujui unachokipalilia wewe...kila mgombea akitumia technique ya kujitangaza kabla wenye mamlaka hawajatoa jina la mshindi kutakalika??

Kama mnapendwa hadi na jumuia ya kimataifa rudini kwenye uchaguzi mchaguliwe tena...mnachoogopa ni kipi kama hamkuchakachua?

Kwanza unajua mimi ni chama gani?au unafikiri wanachama wote wa CCM tunahunga mkono mambo ya kulitia aibu Taifa letu, tangu vyama vya upinzani viruhusiwe nchini kuna chaguzi hata moja ya Urais imewahi kupita bila labsha/malumbano na vitimbwi vingine chungu nzima huko visiwani - mnashindwa nini kufanya chaguzi za kistaarabu - we unafikiri mabango ya kibaguzi yaliyo kuwa yanaonyeshwa na vijana bila ya kukemewa na yeyote, yakitokea matatizo Visiwani si yatatumika kama ushahidi huko the Hague ua wewe ulioni hilo??

Mimi nalitakia mema Taifa letu ndio maana nakuwa muwazi, JK played his part kuwasuruhisheni msitegemee atahitwa tena ku-reinvent the wheel.

Unaweza kudhani ninayo zungumza hapa hayana mantiki, tuombe uzima urudi hapa jamvini baada ya miezi mitatu ili utupatie kilicho jiri visiwani, nakwambia mambo yatajirudia yale yale ya kutaka muhafaka!!!
 
Tusipokuwa makini suala la Zanzibar linaweza kufuta sifa zote nzuri za Taifa letu pamoja na Serikali ya JMT, may be Serikali ya Zanzibar inajiona hawana cha kupoteza ndio maana wanaonekana kutojali maoni ya International Community - lakini wakae wakijua kwamba stance ya Serikali ya Zanzibar kuhusu kurudiwa tena uchaguzi zitamwaribia sana Dk.Magufuli kimataifa.
...Kama ile barua iliyoonekana hapa toka kwa DPs ni ya kweli, uchaguzi ukirudiwa hao jamaa hawatautambua. This will be a first in our history, and surely will tarnish our image.

Narudia tena kusema kwamba wasitake kulingiza Taifa letu pamoja na Dk.Magufuli katika hali ngumu, tutakuja kutengwa Kimataifa na kuwekewa vikwazo tukaponzwa na misimamo yenu hisiyo eleweka/yenye utata mtupu, tukumbuke hasiye kubali kushindwa simshindani.
...I can see a possibility.
 
kwan bila marekani tutakufa njaa
japo siafik ubakaji wa demokrasia uko ZNZ lkn shobo za kuwashobokea WHITE FORKS sizipendi kinoma mbna KOREAKASKAZINI wameweza bila marekani japo wakati wanaanza kukaza uzi walibezwa sana najua HATUWEZI KUJIFANANISHA NA KOREA KASKAZINI ila zama za sasa tujitengenezee mazingila ya kujitegemea wenyewe muda ndo huu wa kujenga nchi yetu TANZANIA afrca kwa ujumla tufufuke tuache uchu wa MADALAKA wangapi wababe walikuwapo leo awapo duniani
koba
MOBUTU SESESEKO JONAS SAVIMBI SANKARA wako wapi wamefukiwa na Bado maisha yanaendelea dunia tunapita tu
Kawaulize wa Iran, watakupa jibu zuri mno
 
Kwanza unajua mimi ni chama gani?au unafikiri wanachama wote wa CCM tunahunga mkono mambo ya kulitia aibu Taifa letu, tangu vyama vya upinzani viruhusiwe nchini kuna chaguzi hata moja ya Urais imewahi kupita bila labsha/malumbano na vitimbwi vingine chungu nzima huko visiwani - mnashindwa nini kufanya chaguzi za kistaarabu - we unafikiri mabango ya kibaguzi yaliyo kuwa yanaonyeshwa na vijana bila ya kukemewa na yeyote, yakitokea matatizo Visiwani si yatatumika kama ushahidi huko the Hague ua wewe ulioni hilo??

Mimi nalitakia mema Taifa letu ndio maana nakuwa muwazi, JK played his part kuwasuruhisheni msitegemee atahitwa tena ku-reinvent the wheel.

Unaweza kudhani ninayo zungumza hapa hayana mantiki, tuombe uzima urudi hapa jamvini baada ya miezi mitatu ili utupatie kilicho jiri visiwani, nakwambia mambo yatajirudia yale yale ya kutaka muhafaka!!!
Kwa mantiki yako unafikiri wanaCUF wote wanaunga mkono kususa uchaguzi??

Sishangazwi na comment zako kuhusu hili huku ukijiita mwanaccm...sielewi mantiki yako ni nini hasa...ninachokumbuka kuwa ndani ya CCM wapo mafisadi,vigeugeu,waoga n.k...walifurushwa baadhi na wakaenda kujiunga na wasanii wenzao wa Ukawa.
Baadhi wapo lakini wameshika adabu!!

Hapa siongei au kujadili mada hii kama mwanachama wa chama flani bali najadili kama mtanzania mzalendo....


Hapo Zanzibar hakuna option zaidi ya option yakurudiwa kwa uchaguzi na atakayechaguliwa na wananchi wa Zanzibar ndio awe Rais ....Napenda kusema abayependwa ndiye atakayeshinda ....mwenye hofu ya uchaguzi basi kuna jambo alilifanya ambalo kwa sasa hatakuwa na fursa hiyo....

Wanaong'ang'ania mshindi atangazwe ni vilaza tu kwani madhara ya kutangazwa mshindi ilihali ushaambiwa uchaguzi ulikuwa na makandokando mengi ni kutafuta full blown chaos....

Kwa mfano ikatangazwa mshindi ni Shain wafuasi wa CUF watafanyaje??

Kwa mfano akitangazwa Seif wafuasi wa CCM watareact vipi??

Uchaguzi uliopita umevurugika na unarudiwa mbona ni rahisi tu....kuna chaguzi ngapi zilizovurugika hapa Tanzania na tukarudia na mshindi akapatikana na maisha yakasonga mbele....!

Why not this time??...

TAIFA LA TANZANIA NA SERIKALI YA JMTZ ILIYOWEKWA KIHALALI KABISA LIKO TAYARI KUMKABILI YOYOTE ATAKAYELETA CHOKOCHOKO IWE ANATOKEA NDANI AU NJE YA MIPAKA YETU...!!
 
kama nchi za scandinavia na japan ndio wangeweka vikwazo ningeshituka kwani marekani msaada wao huwa hauna nguvu pesa nyingi zinarudi kwao na kwa kasi ya kukusanya mapato ya tra sioni tishio lolote kama maji yakizidi unga itabidi tubane matumizi yasiyo ya lazima kama posho za wabunge,ruzuku za vyama na mifuko ya jimbo nawashukuru sana wakizuia misaada kwani ndio tutaona uwezo wa watendaji wetu
 
Hebu jitulize ndio unijibu...!
...Ukiwa hujatulia unaona wote tuko sawa?

...Wewe na YEHODAYA ni mtu mmoja? maana hujatulia, unawashwa, unajikuna, hadi kusahau context ya hoja hii.

Nakuuliza tena ...leo hii huko vijijini umeme hamna wanaishije?
Hapo Dar ulipo umeme ukikatika unaishije?
...Wanaishi kwa taabu. Nami pia!

Usiifanye umeme kama basic need ya kuuza utu na uhuru wako...yaani wewe unaweza toa hata ule mtandao kwa ahadi ya umeme tu!!
...Unafahamu REA inachangiwa na kina nani?

...Unafahamu REA ni yetu wenyewe kwa fedha zetu wenyewe?

...We umezoea kuuza uhuru? Inaonekana humfahamu mzaziyo we!

Pato la mtu wa Dar salaam(kwenye umeme) kwa sasa lina utofauti wa maana ukilinganisha na pato la mtu wa Rombo au Hanang??
...Tofauti ni kubwa! Unafikiri kwanini vijana wanakimbia huko kwenda Dar kutafuta maisha?

Issue hapa ni kutokuwekewa conditions wakati sisi ni Taifa huru
...Kama haujui. Kila siku tunakubali conditions!

...Issue hapa haikuwa kuwekewa hiki au kile! Issue ni REA kama mradi wa maendeleo, ambao wewe a.k.a YEHODAYA umeupondea!

On a side note, ina maana miradi yote hii ya umeme ambayo Serikali inawekeza, inapoteza muda na fedha?
 
Hizo 2trillion zimetoka wapi kwa kulima mahindi hapo msata?!

Au kufanya biashara na nchi nyingine?!

Unajua kama wakiweka vikwazo hata kufika hizo 2trillion itakuwa ni ndoto?!

Unajua au hujui ila unajifanya unajua...?!
Tutaishi kwa tulichonacho
 
...Ukiwa hujatulia unao wote tuko sawa?

...Wewe na YEHODAYA ni mtu mmoja? maana hujatulia, unawashwa, unajikuna, hadi kusahau context ya hoja hii.


...Wanaishi kwa taabu. Nami pia!


...Unafahamu REA inachangiwa na kina nani?

...Unafahamu REA ni yetu wenyewe kwa fedha zetu wenyewe?

...We umezoea kuuza uhuru? Inaonekana humfahamu mzaziyo we!


...Tofauti ni kubwa! Unafikiri kwanini vijana wanakimbia huko kwenda Dar kutafuta maisha?


...Kama haujui. Kila siku tunakubali conditions!

...Issue hapa haikuwa kuwekewa hiki au kile! Issue ni REA kama mradi wa maendeleo, ambao wewe a.k.a YEHODAYA umeupondea!

On a side note, ina maana miradi yote hii ya umeme ambayo Serikali inawekeza, inapoteza muda na fedha?
Again jaribu kutulia mkuu!!

Labda unanijibu kwa kunifananisha na YEOHADA...ndio maana unajibu vitu visivyoeleweka.

Kwa hiyo leo nikikuwekea umeme shida zako zitakuwa zimeisha na utaanza kuishi kwa raha??
 
Tutaishi kwa tulichonacho
Huna chako hapo ulipo hiyo bandari itabakia na stori tu vikwazo vikianza, hiyo dhahabu hutauza, hiyo Tanzanite utapopolea ndege... Hiyo Pamba utakula mwenyewe hakuna kiwanda kitacho survive hapo

Mnajipa matumaini kama wagonjwa wa ukimwi lakufikiria la muhimu ni kudai haki hapo Zanzibar... Hii kujitia ujuaji itawatokea puani
 
Back
Top Bottom