Mapinduzi yaja Tanzania

Mkuu Barubaru kwani wewe ni mtanzania wa wapi? mbona unajitoa?ama ulishaukana uraia wako! Kauli zako kwakweli zinanihamasisha hata kuvaa bomu!!!

Jamaa anaishi Yemen aliisha ukana Utanzania!
 
iiiiiiiiii hiiiiiii nhiiiii hiiiiiii hi hi hiiiii iiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii nalia kwa uchungu, ndugu zetu vijijini wanaumia sana
 
Yaani hata mimi nimelishuhudia......Ikitokea uchaguzi unafanyika kesho.....sisiemu lazima chali......hata wakiwaleta magwiji ya kuchakachua matokeo ya uchaguzi hawata fua dafu......

Ila ninachoomba tu haya mapinduzi yasimwage damu na kutuacha na makovu yasiyo sahaulika.......amani mbeleeeeee maslahi ya nchi mbeleeeeee

Signature ya Dr. Kitila Mkumbo inasema "A struggle without casualities is no struggle-Steve Biko".
 
jk sio mawingu y mvua aende akanyeshe mtera.. Hii kauli sitausahau..jibu rahisi kwenye mambo magumu ..

inanikumbusha mke wa raisi wa kumi wa ufilipino alisema kuwa ni lazima kwake kujirimba na kuonekana mzuri kwasababu wanahitaji kuwa na mke wa raisi mrembo ambaye wanaweza kumwangalia kutoka ktk vibanda vyao vya kismakini. ila siku ambayo walikuja kumtimua mume wake ikulu hakuamini. sasa siku tukimtimua ****** ndio atajua kuwa alikuwa na uwezo wa kunya mvua
 
Nguvu ya mabadiliko Tanzania inakuja kwa kasi ya ajabu. Hakuna kinachoweza kuzuia nguvu ya umma. Kila sehemu ya maisha wananchi wa kada zote wanaonyesha kutofurahia serikali iliyopo madarakani. Ugumu wa maisha na kushamiri kwa rushwa ni kero kubwa kwa Mtanzania wa kawaida.

Ubarikiwe Baba Mchungaji Masanilo,

Waambie wananchi kuwa wasichukuwe matatizo yao kivyao( individually), kwa mfano Ukikosa chakula wewe binafsi tatizo linakuwa lako na humwambii mwenzio, na kama unamwambia unasema uongo kwa kuona aibu, hivyo linakuwa sio la jamii ingawa ukiangalia katika mzio mpana nitatizo la jamii kwani watu milioni 20 kwa wakati huo watakuwa hawana chakula. Hivyo hivyo kwa kukosa hela ya ada kwa mwanao, hela ya kwendea hospitali kutibiwa, kukosa umeme siku mzima nauli ya kwendea kazini nakadhalika.

Ni jukumu la nani kusema kwamba ambao hawana chakula, dawa, ada, nauli umeme au kazi leo wakutane mnazi mmoja ili kilio chao kisikike?

Kunguru wakilia kwa sauti, wanakosesha amani kwa nini sisi na akili zetu tunalila moyoni,kwa nini hatutoi sauti, mbona hatulalamiki, pamoja na ukweli kuwa vitu tunavyokosa ni haki yetu na sio fadhila???????

Utu wetu wa kudai haki u wapi?????
 
..... usitegemee kabisa eti hali tuliyopo Tanzania saizi itarekebishwa tu Chama kingine kikiingia Serkalini... Hapa tulipowekwa na CCM ni pabaya mno and itachukua mda kuweza weka mstari ulonyoooka na kuwafaa Wananchi... na wala Usitegemee eti Mwananchi wa kawaida atanufaika au kuboreshewa maisha yake at a personal level (bado safari ndefu...) - Maana ukweli ni kwamba CCM Wameshindwa... na kuja kwa CDM ni ile tu kubadilisha the name of the system itakayo kuwepo madarakani.... But for change eti ionekane.... Time ndio itasema... Na IMO siamini hilo...

Kauli kama hizi zinatumika sana kuwakatisha tamaa wananchi wakati wa kupiga kura. Utasikia kauli kama hata Slaa hawezi kuondoa rushwa, mara hata Marekani kuna rushwa, heri sisi hatuna njaa kama hao mnaotaka kuwapa madaraka n.k. Ukweli ni kwamba kuna mambo ambayo yanaweza kushughulikiwa ndani ya muda mfupi na mengine ni ya muda mrefu.

CCM wameshindwa hata yale ya kufanya ndani ya muda mfupi kama kupunguza bei ya Sukari. Hii imeshindikana kwa sababu wafanyabiashara hawaiogopi tena serikali, hawamwogopi wala kutii kauli ya rais kwa sababu ndio wanaochangia kampeni. Huwezi kuung'ata mkono unaokulisha. Kuna suala la nidhamu na uwajibikaji kazini, hili linawaumiza sana watu wa kada ya chini maana wanalazimika kutoa rushwa kabla ya kupata huduma. Hili ni suala la muda mfupi tu, wafanyakazi wakijua tu kwamba rais hataki mchezo na suala la uwajibikaji, hawatazembea. Mfano mzuri ni Rwanda-rushwa haijakwisha, lakini imepungua kwa kiasi kikubwa sana, mwananchi wa kawaida hanyanyasiki kama hapa kwetu.

Masuala ya uchumi, hayo yaweza kuchukua muda mrefu kidogo maana yanahusisha kubadilisha sera na kufuatiwa na utekelezaji na hivyo kuchukua muda kuona matunda yake. Kwa hiyo tusikatishe watu tamaa, kwamba mambo hayawezekana hata tukibadili uongozi. Hii kauli si ya kweli maana hata kuwa na uwezo wa kubadili uongozi ni kitu muhimu kwakuwa hata anayeingia (na chama chake) anajua anaweza kuondolewa muda wowote.
 
Hii ni Mada yenye akili,

Wananchi wengi wamebadilika, lakini huwa nakutana watu wengi pia ambao hawajui kinachoendelea, wao kila kitu poa tu Mungu ndie anajua, anajuaa nini wewe chukua hatua fikiria miaka yako ya kuishi hapa duniani inavyofupishwa na mfumo uliopo katika utawala wa nchi hii, baada ya miaka yako hapa duniani utasema na wewe umefanya nini kweli?, jamani kujadili tu bila kuwa na mikakati kweli haisaidii na wala hatutakaa tubadili kitu, Dr wa Ukweli Slaa alishaeleza ukweli na sote tuliofumbuka macho tumeona, sasa tatizo ni watu kufia dini!, chama!, kabila!, ukanda!. yaani kunawatu hataukiwatazama wanapoongea yaani unaanza kujiuliza hivi huyu haoni haya yanayotendeka kweli!?

Katibu mkuu anachangisha pesa ili kuhonga Bunge lipitishe Budget ya uongo na ya kuwatapeli wananchi, kweli watu wengine hawaoni ni mapungufu ya utawala!?, na kama bunge lingekuwa makini hata Budget ya Elimu ingetupwa ni wizi na ubabaishaji mtupu.

Hawa Jamaa wa usalama wa taifa ndio kabisa wengi walevi wa pombe na visasi vya kuonyeshana ubabe na wananchi, eti utaona usalama wataifa utakavyokushughulikia, usalama wa taifa saidieni taifa na taifa sio watu wachache amabo hawazidi hata laki moja, taifa ni milioni 40 ambao ndio wanalipa kodi na ndio shughuli zote zinafanyika kwa jasho lao, hata mishahara yenu pia ni jasho la hao 40m na ndio tunategemea usalama wa taifa uwasikilize na kuwalinda.

kwa upande wa Jeshi yaani JWTZ sina hakika, ila nilikaa na askari polisi mmoja alichoniambia ni hatari sana! yaani anasema askari wa chini hata wao wamechoka sana ila wafanye nini , wakubwa wao wamepewa marupu rupu mazuri hivyo wao ni watoa amri tu.

wewe fikiria Trafic police anayefanya kazi kwa uhakika na kufuata sheria hapendwi! yaani ukikamata gari kula rushwa ndio mpango mzima, ukiandikia watu charge imekula kwako hata hiyo sehemu unahamishwa na hata hiyo kofia ya trafic wanachukua,

sasa katika hali kama hii unafikiri nchi hii kunakubadilika? we real need change na kama tunakaa kimya kwa kuogopa usalama wa taifa tujue kabisa hatuwatendei haki watoto na wajukuu wetu.
 
Nyie wengi ni wanafiki na kwa kuwa nchi mlipewa kwa njia ya barua basi mtasubiri hivyo hivyo mpaka barua nyingine ije.

1961 ni tofauti na 2011, watu tofauti, aina ya ukoloni tofauti, uelewawa watu ni tofauti, matatizo tofauti etc
 
WaTanganyika msijiongopeee HAMNA KABISA UJASIRI huo wa kuleta mapinduzi zaidi ya mapinduzi ya kilimo kuita kilimo kwanza.

Mapinduzi yanataka watu thabiti na waliojitolea kutetea maslahi ya wengi kwani lolote linaweza tokea. Nyie wengi ni wanafiki na kwa kuwa nchi mlipewa kwa njia ya barua basi mtasubiri hivyo hivyo mpaka barua nyingine ije.

Poleni sana

Kwenye red, haupo peke yako unaefikiri hivyo, hata magamba wanafikiri hivyo hivyo. Kitu msichofikiria ni kwamba NJAA inafundisha mambo mengi! Wale vijana wa Mwanza wana njaa na hatimaye njaa imewafundisha kwamba "if u want something done, u have to do it urself!". Naam, naamini watu wengi watajifunza kuleta mabadiliko wao wenyewe, bila kuwatumia wanasiasa ambao wanakumbuka walichotumwa baada ya miaka yao mitano kukaribia kwisha!
 
Emancipate yourselves from mental slavery
None but ourselves can free our minds
Have no fear for atomic energy
'Cause none of them can stop the time
How long shall they kill our prophets
While we stand aside and look?...... bob marley

Songs of freedom are what we need and not mapenzi yana run dunia, nitarejea, etc zinadumaza watanzania
 
Sitaki kuwa negative lakini mpaka niletewe ushahidi from the ground ndio nitaamini.Kama ni kusema mitandaoni tulishafanya sana hivyo kuanzia kitambo,hadi ikafikia pahala Kina Invisible na Max wakatishiwa maisha na JF ikawa off air kwa muda.JF founders wakawa kama wakimbizi.Hapo tulijuwa wamechokonoleka.Sasa ni tofauti kidogo.Wamegundua wananchi wa kawaida wamelala.Unless a few people sacrfices themseleves for the rest.Msitegemee ya Misri ama Tunisia.Mtangoja saana.
Kwasababu kama ni shida wabongo washazoea.Hadi watakapopata shida ambazo ni zaidi na masimulizi ya wazazi wao ndiyo wataingiza akili.
 
mapinduzi yapo tu wakati ukifika wala hatutaumia muda mrefu au hata nguvu tuome Mungu tu yote yanawezekana tutaondokana nauongozi huu uliojaa dharau na ujinga kupita maelezo hata hawasomi nyakati
 
Wendawazimu ninyi mlinyonya wiki ngapi? Mtu aliyenyonya vizuri hawezi kufurahia machafuko. Mbona mnafikiri kwa kutumia kamasi?
 
Wendawazimu ninyi mlinyonya wiki ngapi? Mtu aliyenyonya vizuri hawezi kufurahia machafuko. Mbona mnafikiri kwa kutumia kamasi?
Unajua maana ya machafuko wewe?Kwanza we njuka nani unamwita mwendawazimu?Wewe unatumia nini kufikiri?Makalio ama yanayotoka kunako?Kwa taarifa yako maisha ya wabongo wengi ni mabaya zaidi ya machafuko yenyewe.Inategemea na hayo machafuko.Kuna nchi zilizomo kwenye machafuko na wananchi wake wanaishi better than us tulioko kwenye amani ya kitumwa.Bisha.
 
Kuna wakati nilikuwa naatend mafunzo fulani katika moja ya vyuo vya ufundi vya kijeshi hapa nchini. Na wakati wa mapumziko nilikuwa nimekaa na wanajeshi wapatao kama 30 had 40 hivi tunapiga story. Tulikuwa kwenye vikundi vya watu watatu hadi wanne tukipiga story.

Mimi nikaingiza tu wazo la hali ya nchi inavyokwenda na kuilaumu serikali akiwemo Rais Kikwete. I expected kwamba jeshi lingekuwa kinyume na mimi or wangenishambulia. Huwezi amini, baada ya kuanzisha topic hiyo wanajeshi wote walinyamaza kimya wakanisogelea kunisikiliza, na mmojawapo akasema yafuatayo: "Sisi kama jeshi hatuwezi kufanya mapinduzi, maana tukifanya hivyo tunaweza kujikuta tumekosa support ya wananchi. Ninyi wananchi ndiye mnayechangua serikali mnayoitaka, na sisi kama wanajeshi tunasimamia maamuzi ya wananchi. Lakini ikitokea kwamba wananchi hao hao walioichagua serikali wakaamua kuikataa serikali yao, sisi kama jeshi la wananchi bado tutakuwa upande wa wananchi" mwisho wa kunukuu.

Kwa hiyo wakuu habari ndiyo hiyo. Sina uhakika kuhusu usalama wa taifa, kwa kuwa hao najua wanaingia kwenye hizo nafasi kwa upendeleo na kujuana, kwahiyo wanaweza wasiwe tayari kuwaangusha wale waliowapa hayo maulaji. But kwa upande wa jeshi, ninawahakikishieni kwamba the moment wananchi wanaamua kwa dhati, jeshi litakaa pembeni kulinda maandamano yao. Jeshi ni la wananchi na lipo kwa ajili ya kulinda usalama wa wananchi.

Ninajua na ninaamini kwamba jeshi litaua kadhaa siku za kwanza kabla ya jeshi kuintervene na kuamua kulinda na kusimamia maamuzi ya wananchi. Hata kama generali Mwamunyange ni swahiba mkubwa wa Kikwete, naamini atapingwa vikali na wenzake ndani ya jeshi iwapo ataamua kuwageuka wananchi.

Kwa upande mwingine fuatilieni matokeo ya kura za uchaguzi ya mwaka jana. Kambi nyingi za jeshi zilimpa kura Slaa. Kikwete alipata kura chache sana kutoka kwa wanajeshi. Kazi kwenu kufanya maamuzi.

Mkuu umenirudishia moyo, maana nilikuwa nalifiria sana hili kuwa je wenzetu wanalionaje hili, nakubaliana nawe kabisa sasa ni muda wa sisi wenyewe kulianzisha tena kwa bidii bila kusubiri 2015 Jamani wana JF leteni hapa michango yenu ya Dhati kabisa tulianzishe Jamani let history be wrote in our names for the sake of Nation and future Generations, Taifa Jamani Taifa kwanza, Dodoma hawawezi hili ni sisi leo hii tuamue sasa kwa mikakati ya dhati hata kama ni kwa kuwachangia fedha watu ambao wapo tayari na kuwawezesha lazima tupige kotekote.

Jamani hawa watu wanakula na kusaza na kumwaga wakati kuna wanaolala njaa, hawa watu wanatuibia na bado wakiumwa mafua wanaenda kutibiwa Ulaya kwa kodi ya nchni, mmeona hapa ABBAS wa Babati alikuwa anaugulia ndani kwa kukosa kwenda KCMC tu hapo! hawa watu hawana huruma nasisi tuamke leo tusingoje kesho.
 
Back
Top Bottom