Reverend Masanilo,
Kuna mahali nilichangia kwenye thread aliyoianzisha mkandara leo alfajiri nikasema
Mkandara,
Hoja nzuri sana umetoa.Kama demokrasia ingekuwa universally beneficial kwa mataifa yote basi tungekuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kunufaika.Kwa hali ilivyo sasa,ni kweli kuna kila Dalili kwamba Demokrasia imetushinda tunaifanyia majaribio tu bado tena kwa mbinu na mikakati ile iliyoshindwa
Kwa kweli hii dhana tuliyoletewa ya Demokrasia,imesababisha sisi kurudi nyuma.Hatuna tofauti na mfumo wa kisultani.Leo hii maamuzi magumu ya hayawezi kuchukuliwa kwa hoja ya kipuuzi kabisa mkuu wa nchi yupo nje ya nchi.Rais akiwa nje kuna VP na wengineo,katiba yenye maono ya demokrasia inasema hivyo.
Ni bora turudi kwenye mfumo wa chama kimoja utakaozuia fikra ili sisi wengine tusiopenda kuburuzwa tutumie nguvu za kimapinduzi kwa kusukumwa na uzalendo wetu tuchukue nchi tuongeze kidikteta lakini kizalendo.Tunahitaji utawala kama wa Gaddaffi,tunahitaji mfumo kama wa kagame na Hugo Chavez.tunahitaji mfumo kama wa Evo morales,kusema kweli na siogopi kusema Democracy does not Suit us.bado hatujajiandaa,hii ni imported vice ! ! !
Kama si kuitikia wito na kukubali kuburuzwa na mfumo wa kibeberu,leo hii ningekuwa kwenye kambi,milima ya mbali na au hata msituni kujiandaa kizalendo.Ningekuwa na sababu za kutosha ! ! ! Huwezi kuwa na demokrasia ya kweli kama wananchi wako ni maskini,wanasumbuliwa na maradhi na Ujinga....Huwezi kuwa na uongozi ambao ni zao la Demokrasia bila kuwa na msingi wa imani ya kisiasa,kiuchumi na kijamii katika kiungo cha uongozi na utawala (namaanisha ideology).
Leadership tuliyo nayo ni hadaa tu,sio kwa serikali tu hata kwa vyama vingine vya siasa.Tunapata pigo kubwa sana kwa ngumi iliyovaa gloves za demokrasia(Pseudo democracy).jaribu kufikiria na kutafakari juu ya mfumo wote wa vyama vya siasa Tanzania,jaribu kufuatilia mfululizo wa matukio kwenye vyama hivyo.Kila siku tunapiga hatua kuwasukuma vijana wazalendo kuingia kambini,milimani au misituni.kila dakika ambayo tunahubiri democracy na vijana wazalendo kweli kweli kwa nchi yao hawaoni uhalisia na matunda yatokanayo na dhana hiyo basi tunawatoa kwenye Demokrasia tunawapeleka misituni.
Haya yana Mwisho,kinachohitajika ni hatua za haraka zichukuliwe ama la basi yatatimia.Carl max,alisema...'A single step in the Revolutionary movement worths a Dozen programmes'