Mapendekezo ya muundo wa baraza la mawaziri - 2010-2015

Gazeti la Rai leo limelalamika ya kuwa fitna zimetawala katika uteuzi wa baraza la mawaziri................................

Baadhi ya fitna ilizozibainisha ni kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa kwa makusudi mazima wakivujisha siri za uteuzi huo na huku wengine wakishinikiza kupewa nyadhifa za uwaziri wakati ni viongozi wadhaifu........................

Hizi habari siyo za kuzipuuza hata kidogo ....ieleweke gazeti la Rai lina sikio lake pale Ikulu na hivyo yaonyesha migawanyiko na mifarakano ya CCM inatokota ya kugombania vyeo.................ipo na inakolea.................................

Ingelikuwa ni Chadema imekumbwa na vurugu hizo ungeliyasikia magazeti ya CCM na serikali kama vile Uhuru, Habari leo, Daily News yakiona hicho ni kivuno cha kuuza magazeti..................................................

Nyufa hizi za kugombania vyeo ndani ya CCM ndizo baadaye zitaamua hatma ya Chama hiki kama kweli ni cha mkulima na mfanyakazi au watajwa hawa hutumiwa tu kama ni mtaji wa kisiasa......................

Kumbuka mwenye RAI ndiye anayejua nai kiongozi dhaifu na yupi si dhaifu , mwacheni atengeneze baraza bila kuingiliwa
 
Mkwere kama hayupo stable atatuletea madudu tena safari hii. Akiwaweka hao wanaomshinikiza au kwa kutaka kumlipa fadhira mtu fulani nchi itaishia kutafunwu tu kwani hao jamaa watakuwa wanajitahidi kujihifadhia mifewza kwaajili ya uchaguzi wa 2015. Tutaendelea kuwa waombaji na pesa yote itaishia vinywani mwa hao jamaa zake. haya na tusubiri tuone itakavyokuwa.


Nilitarajia RAI nalo linasubiri list ya mawaziri mara Rais atakapoitaja sawa na wananchi wengine sasa inakuwa je linapata access ya process ya uteuzi ?
 
Zhakia njia ya uwaziri iko wazi ili akatengeneze EPA nyingine, Mzee wa mvua na ndege ya uchumi naye yupo mbioni. Lazima wananchi tuandamane.
 
Gazeti la Rai leo limelalamika ya kuwa fitna zimetawala katika uteuzi wa baraza la mawaziri................................

Baadhi ya fitna ilizozibainisha ni kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa kwa makusudi mazima wakivujisha siri za uteuzi huo na huku wengine wakishinikiza kupewa nyadhifa za uwaziri wakati ni viongozi wadhaifu........................

Hizi habari siyo za kuzipuuza hata kidogo ....ieleweke gazeti la Rai lina sikio lake pale Ikulu na hivyo yaonyesha migawanyiko na mifarakano ya CCM inatokota ya kugombania vyeo.................ipo na inakolea.................................

Ingelikuwa ni Chadema imekumbwa na vurugu hizo ungeliyasikia magazeti ya CCM na serikali kama vile Uhuru, Habari leo, Daily News yakiona hicho ni kivuno cha kuuza magazeti..................................................

Nyufa hizi za kugombania vyeo ndani ya CCM ndizo baadaye zitaamua hatma ya Chama hiki kama kweli ni cha mkulima na mfanyakazi au watajwa hawa hutumiwa tu kama ni mtaji wa kisiasa......................

Na bado ana uteuzi wa failures wengine 7 ambao atawakweza uwaziri juu kwa juu. Msishangae kumsikia Masha, Batilda,.... wakiendelea kuwa mawaziri.
 
Mkwere asipoangalia atajimaliza na sisiem itamfia mikononi mwake!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kaburi ishachimbwa bado ibada tu.....RIP dear old CCM

Ni ukweli ulio wazi kuwa CCM haijawahi kuwa bogus kama kipindi cha uongozi wa Kikwete. Na Tanzania yetu haiwezi kupata mwamko wa maendeleo bila ya kuiondoa CCM madarakani kwani hiki chama sasa kimeibinafsisha nchi kwa mafisadi na familia zao.
 
Duh, udhaifu huo, kwani rais ni nani? na ana ubia na mtu pale?

Sio kwa Rais huyu tulienae. Rostam na Makamba wakisema nataka Makinda spika mzee anasema hewala hata kama anajua ngumu. Hana sauti dhidi ya majuha hawa. Leo Lowassa akisema weka Maji Marefu waziri wa wizara ya Unajimu na Mahusiano ya Wanga atamuweka na kuanzisha wizara hiyo.

Uwezo wa kimaamuzi kwa raisi wenu haupo na ndio maana watu wanafanya watakayo. NDANI YA CCM sasa hivi kila mtu kambale ana masharubu na hakuna namna tena acha tu tuendelee umia kwa muda huu tena
 
Mkwere kama hayupo stable atatuletea madudu tena safari hii. Akiwaweka hao wanaomshinikiza au kwa kutaka kumlipa fadhira mtu fulani nchi itaishia kutafunwu tu kwani hao jamaa watakuwa wanajitahidi kujihifadhia mifewza kwaajili ya uchaguzi wa 2015. Tutaendelea kuwa waombaji na pesa yote itaishia vinywani mwa hao jamaa zake. haya na tusubiri tuone itakavyokuwa.


Just for curiosity, hivi amewahi kuwa stable?
 
Gazeti la Rai leo limelalamika ya kuwa fitna zimetawala katika uteuzi wa baraza la mawaziri................................

Baadhi ya fitna ilizozibainisha ni kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa kwa makusudi mazima wakivujisha siri za uteuzi huo na huku wengine wakishinikiza kupewa nyadhifa za uwaziri wakati ni viongozi wadhaifu........................

Hizi habari siyo za kuzipuuza hata kidogo ....ieleweke gazeti la Rai lina sikio lake pale Ikulu na hivyo yaonyesha migawanyiko na mifarakano ya CCM inatokota ya kugombania vyeo.................ipo na inakolea.................................

Ingelikuwa ni Chadema imekumbwa na vurugu hizo ungeliyasikia magazeti ya CCM na serikali kama vile Uhuru, Habari leo, Daily News yakiona hicho ni kivuno cha kuuza magazeti..................................................

Nyufa hizi za kugombania vyeo ndani ya CCM ndizo baadaye zitaamua hatma ya Chama hiki kama kweli ni cha mkulima na mfanyakazi au watajwa hawa hutumiwa tu kama ni mtaji wa kisiasa......................

Rai ni gazeti la mafisadi, na hii ni angalizo kwa JK asikubali ushauri wa akina Membe kumpa 6 unaibu Waziri Mkuu. Cheki patamu hapo!
 
*Yeye asema tuyaache hayo, ni uvumi usio na msingi.

Na Tumaini Makene.
WAKATI Watanzania wakisubiri kwa hamu Baraza la Mawaziri la Rais Jakaya Kikwete litakalomsaidia kuongoza serikali katika ngwe yake ya mwisho, habari zimevuja zikimhusisha Mbunge wa
Monduli, Bw. Edward Lowassa na mikakati ya kukwaa moja ya wizara nyeti katika serikali mpya itakayoundwa na rais siku chache zijazo.

Bw. Lowassa ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu katika serikali ya Rais Kikwete kabla hajajiuzulu kufuatia kashfa ya Richmond iliyopewa zabuni ya kuzalisha umeme kinyume cha taratibu, anatajwa katika mikakati ya kuteuliwa waziri katika wizara itakayohusika na tawala za mikoa na serikali za mitaa.

Katika Serikali zilizopita ikiwamo ile ya awamu ya kwanza ya Rais Kikwete wizara hiyo ilikuwa ikijulikana kwa ufupisho kama TAMISEMI (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), na inaelezwa kuwa ni nyeti inayompa waziri fursa ya kuwa karibu zaidi na wananchi.

Vyanzo vya habari vilivyo karibu na duru za michakato inayoendelea serikalini juu ya uteuzi wa nafasi mbalimbali hususan zile za kisiasa, vimeliambia Majira kuwa upo msukumo mkubwa kutaka Bw. Lowassa ateuliwe katika nafasi hiyo kwa mustakabali wake kisiasa, hususan katika uchaguzi mkuu wa 2015.

Pamoja na kutoa taarifa hizo, watu hao walio karibu na Bw. Lowassa waliliambia Majira kuwa huenda yeye (Lowassa) hahusiki katika mikakati ya kuzishawishi mamlaka zinazohusika na uteuzi wa mawaziri, kumteua katika nafaii hiyo nyeti, lakini upo msukumo wa wazi kutaka hivyo.

Majira lilipomtafuta Bw. Lowassa juu ya tetesi hizo, alijibu kuwa yeye hajui lolote wala hajasikia kitu kama hicho.

"Sijui lolote wala sijasikia lolote kuhusiana na hicho unachokisema, tuyaacheni kwanza hayo mambo, la sivyo tutakuwa tunazungumzia speculations (tetesi, uvumi) bila sababu yoyote.

"Nasisitiza kuwa sina taarifa zozote kutoka mamlaka za uteuzi, sijasikia kitu kama hicho, ni speculations ambazo hazina maana yoyote ile," alisema Bw. Lowassa ambaye amekuwa swaiba wa karibu wa Rais Kikwete, kikazi na kimaisha, kwa muda mrefu.

Kabla ya kupatikana kwa habari hizo zikimhusiaha Bw. Lowassa na uteuzi wa waziri wa TAMISEMI, kulikuwa na tetesi zilizokuwa zikimtaja kuwa mmoja kati ya watu ambao wangeweza kuteuliwa tena katika nafasi ya waziri mkuu, lakini wadadisi wengi wamesema kuwa itakuwa ni vigumu kutokana na ukweli kwamba Bw. Mizengo Pinda bado ana nafasi kubwa ya kuendelea na Rais Kikwete kumalizia ngwe yao ya mwisho.

Uwezekano wa Bw. Pinda kuendelea na nafasi hiyo ya uwaziri mkuu umeelezwa kuwa ni mkubwa kutokana na uadilifu wake, kutokuwa mtu wa makundi ndani ya CCM na serikalini, akielezewa kuwa hapendi matumizi makubwa ya fedha za umma, huku pia akiwa hajawahi kukumbwa na kashfa yoyote, hali ambayo inamfanya akubalike kwa kadri upepo wa kisiasa ulivyo nchini kwa sasa.

Vyanzo vya habari vilivyo karibu kikazi na mbunge huyo wa Monduli, vimesema kuwa hali hiyo ya nafasi ya uwaziri mkuu kuonekana 'imejaa' ndiyo imeelezwa kuwa sababu ya Bw. Lowassa kutajwa katika uteuzi wa wizara nyeti ya TAMISEMI.

Pamoja na kuwa wengi wamekuwa wakiichukulia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kuwa ndiyo moja ya wizara nyeti nchini, maarufu kama 'njiapanda ya ikulu', baada ya kumtoa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa na Rais Kikwete, bado unyeti wa TAMISEMI katika utawala wa nchi haukwepeki kutokana na ukweli kuwa ndiyo wizara yenye mtandao mkubwa ndani ya nchi, ikiwa ni kiunganishi kati ya serikali kuu na serikali za mitaa.

Waziri wa wizara hiyo ambayo mara nyingi imekuwa ikiwekwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ikiwa pamoja na ile inayohusika na maafa na utaratibu wa bunge, ameelezwa kuwa ana afasi pana zaidi ya kukutana na wananchi wa kada mbalimbali katika shughuli mbalimbali za maendeleo zinazogusa maisha ya kila siku ya Watanzania, hasa wale wapiga kura.

TAMISEMI inaonekana kuwa ni wizara mtambuka, ikielezwa kuwa ni kiungo muhimu kati ya wizara za kisekta na asasi mbalimbali za Serikali za Mitaa. ikiwa na jukumu la kuhakikisha yanajengwa mazingira mazuri ya kuwezesha ushirikishwaji wa umma katika kujiletea maendeleo, kwa kuzingatia utawala bora.

Kwa mujibu wa mkataba kwa wateja wa wizara hiyo, kulingana na mpango uliopo sasa wa uboreshaji wa huduma kwa umma, TAMISEMI inategemewa kuongoza na kuwa kiungo kati ya mpango wa uboreshaji wa mfumo wa Serikali za Mitaa na Mpango wa Uboreshaji wa Wizara za Kisekta unaofanywa na sekta mbalimbali ngazi ya Taifa.

Katika kuonesha unyeti wa wizaya hiyo, mkataba huo unaeleza kuwa TAMISEMI ina wajibu wa kuratibu na kusimamia tawala za mikoa ili ziweze kuzisaidia halmashauri katika kutekeleza wajibu na majukumu yake; kutayarisha na kusimamia sera ya maendeleo vijijini; kusimamia utekelezaji wa Sera ya Maendeleo Mijini; kuendeleza programu ya uboreshaji wa mfumo wa Serikali za Mitaa nchini ili ziweze kutoa huduma bora.

Majukumu mengine yametajwa kuwa ni kuzijengea Serikali za Mitaa uwezo wa kusimamia mapato na matumizi; kuboresha miundo, hali ya watumishi na mifumo ya kazi ndani ya TAMISEMI, mikoa na halmashauri; kusimamia asasi, mashirika ya umma na miradi inayotekelezwa chini ya wizara hiyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM), kuratibu utekelezaji wa shughuli za hifadhi ya mazingira katika Serikali za Mitaa na pia kuratibu vita dhidi ya rushwa na UKIMWI.

Tangu kujiuzulu kwake uwaziri mkuu kwa kashfa ya Richmond, akiwa waziri mkuu wa kwanza kufanya hivyo nchini, mapema Februari 2008, Bw. Lowassa amekuwa kimya katika masuala mengi ya kitaifa, suala ambalo limekuwa likielezewa na wachambuzi wa mambo kuwa ni mkakati wake wa kisiasa kurudi katika uringo wakati mwafaka ukiwadia.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa waliozungumza na Majira, vikiwemo vyanzo hivyo vya habari, wamesema kuwa nafasi hiyo ya uwaziri wa TAMISEMI, utampatia nafasi nzuri Bw. Lowassa kurudi katika chati ya kisiasa hata kubadili upepo wa kisiasa hasa nje ya CCM ambapo imeelezwa kuwa umekuwa haumwendei vizuri, tangu alipoondoka serikalini.

Hivi karibuni, katika uchaguzi mkuu uliopita, mbunge huyo wa Monduli, alijipatia ushindi wa kishindo na kumshinda kirahisi mgombea wa CHADEMA, Mchungaji Amani Silanga.
 
source free media

UKWELI WA KAULI ZA KIKWETE KUWA URAIS NI SUALA LA FAMILIA YAKE IMEDHIHILIKA KWA KUWA HIVI SASA WABUNGE WENGI WA CCM WAJIPENDEKEZA KWA KUPANGA FOLENI KWA MAMA SALMA NA RIDHIWANI KIKWETE ILI WAWEZE KUPEWA NAFASI YA KUONGOZA WIZARA MBALIMBALI akiwemo SAMWELI SITA NA E. LOWASA
 
Wanabembeleza kupewa wizara zifuatazo;
1. Lowasa -tamisemi
2. Sita - mambo ya ndani
 
Lowassa hawezi kujipendekeza kwa Kikwete....Sitta ndo kabisa kishajeruhiwa hana hamu
 
40 kuunda baraza jipya la mawaziri
Sunday, 21 November 2010 21:29

kikwete-kuapishwa.jpg
Rais Jakaya Kikwete ambaye siku za hivi karibuni anatarajiwa kutangaza baraza jipya la mawaziri ambalo amedai litakuwa na wamtu waadilifu na wachapakakzi

Sadick Mtulya
BARAZA jipya la mawaziri linalotarajiwa kutangazwa wiki hii na Rais Jakaya Kikwete linatarajiwa kuwa na mawaziri kati ya 40 na 45, kati yao 23 wakiwa ni mawaziri kamili.Kwa maana hiyo, baraza hilo litakuwa na wizara 23 tu, Mwananchi imedokezwa.Habari ambazo Mwananchin imezipata zinaeleza kuwa katika baraza hilo jipya, ambalo litakuwa la tatu kwa Rais Kikwete tangu alipoingia Ikulu mwaka 2005, waliokuwa manaibu waziri watano katika baraza lililopita, watapandishwa na kuwa mawaziri kamili.

Vyanzo vyetu vya kuaminika vimeeleza kuwa idadi ya mawaziri wanawake itaongezeka kulinganishwa na baraza lililopita na kwamba uteuzi umezingatia umri, uzoefu pamoja na uwiano wa mikoa.Pamoja na kuwepo kwa sura mpya, idadi kubwa ya waliotajwa katika baraza hilo ni wanasiasa wakongwe ambao wengi wao walikuwamo katika baraza lililopita.
Chanzo chetu kimeeleza kuwa Rais Kikwete amekataa kuwapa nafasi ya uwaziri wabunge waliopata ushindi kwa kura chache katika uchaguzi mkuu uliopita.
Miongoni mwa wabunge waliokuwa manaibu kwenye baraza lililopita ni Emmanuel Nchimbi (Songea Mjini) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Adamu Malima (Mkuranga) aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini na Christopher Chiza (Buyungu) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji.
Wengine ni Dk David Mathayo (Same Magharibi) aliyekuwa Naibu Waziri wa Kilimo na Ushirika pamoja na Balozi Khamis Kagasheki (Bukoba Mjini) aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani.

Habari hizo zinasema kuwa Wizara ya Fedha na Uchumi itaendelea kuwa na manaibu waziri wawili kama ilivyokuwa katika ngwe ya kwanza ya miaka mitano ya serikali ya Rais Kikwete.
Mbali na wabunge 27 waliotajwa na gazeti hili jana wengine ambao wametajwa kuwemo kwenye serikali mpya ya Rais Kikwete ni Muhammed Seif Khatibu kutoka Jimbo la Uzini ambaye alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Stephen Wasira(Bunda) aliyekuwa Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, na Hawa Ghasia (Mtwara Vijijini) aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma.

Wengine ni Mustapha Mkulo (Kilosa) aliyekuwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Mathias Chikawe (Nachingwea) aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria pamoja na Aggrey Mwanri (Siha) aliyekuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi).
Wengine ni Bernard Membe (Mtama) ambaye katika serikali iliyopita alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikano wa Kimataifa na Emmanuel Nchimbi (Songea Mjini) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Mawaziri wengine waliokuwa katika Serikali iliyopita wanaotajwa kurejeshwa katika kipindi hiki cha mwisho cha utawala wa Kikwete ni Ezikeil Maige (Msalala) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, William Ngeleja (Sengerema) aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, na Celina Kombani (Ulanga Mashariki) ambaye alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi),
Wengine ni Profesa Juma Kapuya (Urambo Magharibi), aliyekuwa Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana, Profesa Mark Mwandosya (Rungwe Mashariki), ambaye alikuwa Waziri Maji na Umwagiliaji, Dk Hussein Mwinyi (Kwahani), aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Shukuru Kawambwa (Bagamoyo), aliyekuwa Waziri wa Miundombinu na John Magufuli (Chato) ambaye alikuwa Waziri wa Maendeleo Mifugo na Uvuvi.

Wabunge wanaotajwa kuingia katika baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza ni Anna Tibaijuka (Muleba Kusini), Samuel Sitta (Urambo Mashariki) na ambaye alikuwa spika wa Bunge la Tisa, Dk Harrison Mwakyembe (Kyela), Anne Kilango (Same Mashariki).
Wengine ni Januari Makamba (Bumbuli) ambaye alikuwa msaidizi wa rais katika awamu ya kwanza ya utawala wa Rais Kikwete, Salehe Pamba (Pangani), Steven Masele (Shinyanga Mjini), Gerson Lwenge (Njombe Magharibi) na Nyambari Nyangwine (Tarime).

Wengine ni Shamsi Vuai Nahodha (mbunge kuteuliwa) na alikuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Angela Mkwizu (Viti Maalum) na Amos Makala (Mvomelo) ambaye ni Mweka Hazina wa CCM, Said Bwanamdogo (Chalinze), Lazaro Nyarandu (Singinda Kaskazini) na Zakia Meghji (wa kuteuliwa).
Chanzo hicho kimebainisha kuwa Rais Kikwete amedhamiria kuunda baraza dogo la mawaziri litakalo kuwa na tija ikilinganishwa na alilounda wakati akiingia madarakani mwaka 2005, ambalo lilikuwa na mawaziri wapatao 60 na ambalo alilivunja Februari 2008 baada ya Edward Lowassa kujiuzulu wadhifa wa Waziri Mkuu.

Lowassa alijiuzulu kutokana na kashfa ya zabuni tata ya ufuaji umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni ya Richmond.
Hata hivyo, baraza jipya aliloliunda baadaye chini ya Waziri Mkuu mpya, Mizengo Pinda lilikuwa na mawaziri 27 na manaibu mawaziri 21.
Kati ya mawaziri ambao hawatarajiwi kurejea kwenye baraza jipya ni wale walioanguka katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM na wengine waliangushwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu.
Akilihutubia Bunge Alhamisi iliyopita, Kikwete alidokeza kuunda serikali itakayokuwa na watu waadilifu, makini na wachapakazi hodari.
Pia alisema ataunda serikali ya watu wachache ambao wataondoa urasimu watakaokuwa karibu na wananchi na kushirikiana vizuri na wabunge wote bila kujali vyama vya siasa wanavyotoka.
Source: Mwananchi.
 
Kama hili baraza ni kweli kama ilivyoandikwa basi 'Kikwete huimba kama Malaika na kucheza kama Shetani'
 
Sioni chochote cha maana katika orodha hiyo. Mambo yatakuwa vilevile tu. Watanzania wasitarajie chochote kutoka kwenye orodha hiyo.
 
Back
Top Bottom