Na bila yeye wangekufa watu wengi sana.
Mpe heshima yake kwa kusimamisha genocide mkuu pia huwezi tambua ilivyo vigumu kuishi na watu wenye chuki/sumu rohoni ni ngumu sana na kama huamini niambie kwanini jana, leo na mpaka kesho machafuko hayataka yaishe Afghanistani ni kwanini?
Unaweza ona watu wanachekeana tuu lakini ukijua lililo mioyoni mwao utapigwa na butwaa.
Nimeishi na watu wenye chuki hivyo naelewa kwanini ubabe unahitajika kuwanyamazisha watu vinginevyo akilegeza tuu yatatokea machafuko mengine tena yasiyoisha. Na nikwambie tuu chuki huishi vizazi na vizazi na from my experience mababu zangu waliwahi kuzulumiwa hii kitu hainifurahishi japo ni miaka mingi sana hata kabla sijazaliwa
So kwa taifa kama Rwandese unategemea nini? Hii chuki haiishi mjomba yani ngoma inaendelezwa vizazi na vizazi ndio maana nguvu kubwa inatumika kuwazima watu midomo ili maisha yaende.
Tutsi na Hima kusameheana hiyo sahau labda miujiza ya Mungu ifanyike.