jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,053
- 28,245
Kweli uzee waweza kuwa kitu kibaya sana kwa sababu kila kukicha unapata mshtuko wa moyo kwa mambo yanavyoendelea duniani na haswa nchini mwetu!
Ni Tanzania hii hii ambayo kuna baadhi ya wajukuu zangu wanadumaa kwa kushindia muhogo na chai kila siku inayoenda kwa mungu lakini ndani ya nchi hii hii kuna watu wanamiliki magari ya kifahari na makasri kuliko walivyokuwa wakoloni wetu wajerumani.
Sitaki kupiga porojo sana lakini ninashangazwa sana na siamini kama kuna watanzania wenye uwezo wa kununua au sijui nisema kukodisha hizi nyumba zinazojengwa na shirika la nyumba la Taifa (NHC) maarufu kama Meru Residential Apartments. Sielewi nyumba hizi zimejengwa kwa ajili ya watanzania wenye kipato cha namna gani. Naomba mwenye ufafanuzi anisaidie jamani. Mbona kama shirika hii linakomoa watanzania na kuwarudisha utumwani? Naona huruma sana kwa kizazi kitakachokuja miaka 50 baadae!
Ili uweze kutoa maoni zaidi hebu bofya www.nhctz.com/meru/
Ni Tanzania hii hii ambayo kuna baadhi ya wajukuu zangu wanadumaa kwa kushindia muhogo na chai kila siku inayoenda kwa mungu lakini ndani ya nchi hii hii kuna watu wanamiliki magari ya kifahari na makasri kuliko walivyokuwa wakoloni wetu wajerumani.
Sitaki kupiga porojo sana lakini ninashangazwa sana na siamini kama kuna watanzania wenye uwezo wa kununua au sijui nisema kukodisha hizi nyumba zinazojengwa na shirika la nyumba la Taifa (NHC) maarufu kama Meru Residential Apartments. Sielewi nyumba hizi zimejengwa kwa ajili ya watanzania wenye kipato cha namna gani. Naomba mwenye ufafanuzi anisaidie jamani. Mbona kama shirika hii linakomoa watanzania na kuwarudisha utumwani? Naona huruma sana kwa kizazi kitakachokuja miaka 50 baadae!
Ili uweze kutoa maoni zaidi hebu bofya www.nhctz.com/meru/