Maoni yangu kuhusu Meru Residential Appartments

hivi katiba yetu inasema tanzania ni nchi ya kibepari?
Hakuna haja ya katiba kukuambia kuwa Tanzania ni nchi ya kibepari, ili mradi ubepari usipingane na katiba ya Tanzania, hakuna kitu kwenye katiba kinachozuia ubepari.

Kwa mfano tu katiba ya Marekani haisemi kuwa Marekani ni nchi ya kibepari.
 
Hakuna haja ya katiba kukuambia kuwa Tanzania ni nchi ya kibepari, ili mradi ubepari usipingane na katiba ya Tanzania, hakuna kitu kwenye katiba kinachozuia ubepari.

Kwa mfano tu katiba ya Marekani haisemi kuwa Marekani ni nchi ya kibepari.

lakini nchi yetu si ya kijamaa na kujitegemea?anyway kinadharaia ni hivyo lakini kiutendaji si hivyo.tuachane na hayo,hivi kwa nini tunafanya maamuzi ambayo yanawakandamiza wazawa?kumuambia mtanzania alipe milioni 175+ wakati unajua pato lake ni dogo,hii ni akili au ujuha?hivi hawa wanakaa chini na kuamua haya wanaishi nchi gani?
 
Mortgage loan ya miaka 15 utalipa karibia 1,000,000 kwa mwezi bado maintance charges hata madokta wetu bado hawawezi kuafford.Walengwa ni wakina nani?
 
Kwa taarifa yako Babu, kuna mtu yupo NHC hapa ananidokeza kuwa hizo nyumba tayari zimeshanunuliwa zote kwa bei hio ya zaidi ya Tsh 175,000,000/=. Na walionunua ni Watanzania.
Usiseme sisi Watanzania ni Masikini, sema Mtanzania Mimi ni masikini
 
hebu tuangalie hii

"...............The Corporation Established in 1962, was Reconstituted in its present form by the Act of Parliament No. 2 of 1990. The Purpose of this reconstitution was to enable NHC Play aggregate role in the housing sector.
In this endeavor, NHC 's mission is to provide and facilitate the provision of serviced land, housing and other buildings in Tanzania for use by members of the public for residential, business, industrial and other purposes. The vision of NHC is to become a major mass housing producer and commercial property developer. These responsibilities enhance the limited traditional role of inch of constructing low-cost rental residential buildings in urban areas.................
"

tuendelee kujadili.....

kwa maoni yangu Meru apartments siwezi kuziita low-cost...........kipato cha wastani cha Mtanzania hakiwezi kukidhi mahitaji ya malipo ya hizo Meru apartments.......

Je Kuna miradi ya low cost housing inayobuniwa hivi sasa na NHC?
 
Loan Mortgage ya miaka 15 utalipa karibia 1,000,000 kwa mwezi bado maintance charges hata madokta wetu bado hawawezi kuafford.Walengwa ni wakina nani?

hili ndilo swali ninalojiuliza walengwa ni sisi kajambanani au la.au labda awamu yetu bado!
 
Kwa taarifa yako Babu, kuna mtu yupo NHC hapa ananidokeza kuwa hizo nyumba tayari zimeshanunuliwa zote kwa bei hio ya zaidi ya Tsh 175,000,000/=. Na walionunua ni Watanzania.
Usiseme sisi Watanzania ni Masikini, sema Mtanzania Mimi ni masikini

mjukuu wangu hili ndio tatizo.nyumba zishauzwa halafu unamuona bwana mdogo kibonde anatuhamasisha eti tununue nyumba!kweli tanzania kazi ipo.
 
ogah umeeleza vizuri.najiuliza NHC walifanya utafiti wa kipato cha mtanzania na kuona hizo bei zinaendana na mapato yetu wafanyakazi au wafanyabiashara wa wa kitanzania?najipa matumaini watatukumbuka na sisi lakini swali langu kwa nini priority iwe kwa mapapaa?tafakarini jamani mimi umri wangu umeenda sihitaji hizo nyumba nawahurumia wajukuu wangu!
 
lakini nchi yetu si ya kijamaa na kujitegemea?anyway kinadharaia ni hivyo lakini kiutendaji si hivyo.tuachane na hayo,hivi kwa nini tunafanya maamuzi ambayo yanawakandamiza wazawa?kumuambia mtanzania alipe milioni 175+ wakati unajua pato lake ni dogo,hii ni akili au ujuha?hivi hawa wanakaa chini na kuamua haya wanaishi nchi gani?

Sawa ni nchi ya ujamaa na kujitegemea, ubepari kimsingi haupingi hayo ukiangalia definition ya ujamaa kwenye katiba.
Kuna watanzania wana kipato halali cha kuweza kununua hizo nyumba, sio wengi ila unakuwa unalenga market tofauti kwenye biashara.

"Ujamaa" au "Ujamaa na Kujitegemea" maana yake ni misingiya maisha ya jamii ya kujenga Taifa linalozingatiademokrasia, kujitegemea, uhuru, haki, usawam udugu na​
umoja wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano;
 
Kwa taarifa yako Babu, kuna mtu yupo NHC hapa ananidokeza kuwa hizo nyumba tayari zimeshanunuliwa zote kwa bei hio ya zaidi ya Tsh 175,000,000/=. Na walionunua ni Watanzania.
Usiseme sisi Watanzania ni Masikini, sema Mtanzania Mimi ni masikini
Na madokta ni wangapi katika hiyo list? Tatizo la nyumba lipo kwa watu wa kipato cha kati na chini, kwa sababu hawawezi kuafford kujenga na ili shirika ndio lingetakiwa liwe linawatumikia.Hakuna umuhimu wa kuwa na shirika linaloendeshwa kwa pesa za wananchi kwa ajili ya kuwatumikia matajiri, private kampani itaweza kufill hiyo gap.
 
Sawa ni nchi ya ujamaa na kujitegemea, ubepari kimsingi haupingi hayo ukiangalia definition ya ujamaa kwenye katiba.
Kuna watanzania wana kipato halali cha kuweza kununua hizo nyumba, sio wengi ila unakuwa unalenga market tofauti kwenye biashara.
Hata kwenye nchi za kibepari hawafanyi hivyo, shirika la serikali linajenga nyumba kwa ajili ya matajiri na kuwaacha middle class wanateseka.
 
Milioni175 unanunua numba nchi yoyote nyumba siyo apartment. hapo chini inauzwa 69.000$
 
kwa hiyo ni wazi tumeingia kwenye capitalism?lakini tumebadilisha katiba yetu au tumewaandaje watanzania kuingia huko au ndo tunarudishana utumwani kidogokidogo?hata mimi sidhani kama watakosa wateja lakini sina uhakika kama wateja watakuwa ni watanzania.sana sana wazungu wenyewe au wazungu kupitia majina ya watanzania wenye tamaa.

Duh! mkuu unaishi nchi gani? Au ulkikuwa jela? Unauliza kama tumeingia kwenye capitalism leo in 2011?
 
Kwa taarifa yako Babu, kuna mtu yupo NHC hapa ananidokeza kuwa hizo nyumba tayari zimeshanunuliwa zote kwa bei hio ya zaidi ya Tsh 175,000,000/=. Na walionunua ni Watanzania.
Usiseme sisi Watanzania ni Masikini, sema Mtanzania Mimi ni masikini
Al Shabab na hela za utekaji meli, ndio soko letu, tumeona Kenya wanazifaidi saana
 
SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA
KUKARIBISHWA MAOMBIYA KUNUNUA NYUMBA 30 ZILIZOKO MJINI ARUSHA
Shirika la Nyumba la Taifa linawakaribisha watanzaniawakazi na wasio wakazi kuleta maombi yakununua nyumba zake zilizojengwa mjini Arusha. Nyumba hizo ambazo zinaitwa “MeruResidential Apartments” zinatarajiwa kukamilika ndani ya miezi mitatu (siku 90)kuanzia tarehe 1 Oktoba,2011.MRADI WENYEWE:Meru Residential Apartments zimejengwakwenye mandhari murua inayokupatia maisha bora katika jamii yenye usalama.Zimepewa jina hilo kama ishara ya kuuenzi Mlima wa Meru ambao ni mlima wenyeVolcano hai nchini Tanzania wenye urefu wa mita 4,566 (futi 14,980), ukiwa nimlima wa kumi kwa urefu barani Afrika.MAHALI ZILIPO:Meru Residential Apartments ziko mjiniArusha kwenye eneo la katikati kabisa, kwenye mtaa wa Wachaga, Kiwanja Na. 565/I. Eneo hilo likoumbali usiozidi kilomita mbili toka ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ukumbi wa mikutanowa Kimataifa wa Arusha (AICC), nyumba hizo zimepakana na hospitali ya Selian naChuo cha Ufundi, na kwa upande wa mashariki inakupatia muonekano mzuri wa MlimaMeru.MAELEZO YA NYUMBAHIZO.
Idadi ya Nyumba 30
Ukubwa eneo la nyumba 169.45
Idadi ya Majengo 2
Idadi ya ghorofa kwa kila jingo Ghorofa nne
Idadi ya vyumba kwa kila nyumba 3 (kimoja kinajitegemea)
Sifa nyingine za nyumba hizo Sebule kubwa, chumba cha kulia, jiko,stoo,bafu na choo [ Nyumba zinauzwa bila samani (furniture)]
Kila nyumba ina maegesho maalum ya gari, pamoja na tanki la maji la lita 1000.
BEI ZA NYUMBA HIZO:Bei ya chini kabisa ya kila nyumba nishilingi za Kitanzania 175,314,366.48 bilakujumlisha kodi ya ongezeko la thamani. Mwombaji atakayetoa bei ya juu zaidi nakutimiza masharti yote yaliyoelezwa hapo chini ana nafasi kubwa zaidi yakuuziwa.TARATIBU ZA KUOMBA:Waombaji wanatakiwakuzingatia utaratibu ufuatao:1. Wanaopenda kununua nyumbawachukue fomu za maombi kutoka Makao Makuu ya Shirika, kwenye ofisi za Shirikazilizopo Arusha, au kwenye ofisi yoyote iliyo karibu nao. Fomu zinapatikana piakwenye tovuti wa Shirika (www.nhctz.com). 2. Fomu za kuomba kununua zijazwe nakuwekwa saini na kurejeshwa kwenye ofisi za Shirika pamoja na barua yakuonyesha kiasi ambacho mwombaji yuko tayari kulipa. Shirika litahitaji pia ushahidiwa malipo ya shilingi 10,000/=(Malipo yasiyorejeshwa) kama ada ya maombi namalipo ya asilimia kumi (10%) ya awali zilizolipwa kupitia benki kulingana nathamani ya nyumba uliyochagua. 3. Waombaji wote waliofanikiwawataandikiwa barua kujulishwa hivyo. Watapewa siku 90 toka tarehe ya barua hiyokukamilisha malipo ya asilimia tisini (90%) iliyosalia kulipia nyumba husika.Utaratibu wa kulipa unaweza kuthibitishwa kwa kulipa pesa kwenye akaunti yamradi au kuonyesha hati ya mkopo toka benki. 4. Kama uthibitisho wa malipohautawasilishwandani ya siku 90, mnunuzi atanyang’anywa na nyumba hiyo kuuziwamtu mwingine toka kwenye orodha ya waombaji. Mnunuzi aliyeshindwa kulipa hiyoasilimia tisini (90%) ataruhusiwa kutumia asilimia kumi (10%) ya awali kulipianyumba kwenye mradi mwingine. Aweza pia kurejeshewa fedha zake kwa kukatwaasilimia mbili (2%) ya kiasi hicho. 5. Mwisho wa kuwasilisha maombi niJumatano tarehe 4 November, 2011 saa4:00 asubuhi. 6. Maombi yapelekwe ndani ya bahashayenye rangi ya hudhurungi/kahawia iliyoandikwa juu;”Maombi ya Kununua Nyumba za Meru-Arusha”. 7. Maombi yote yapelekwe kwa: Meneja wa Mkoa, Shirika la Nyumba la Taifa,S. L. P 883, ARUSHA
 
Milioni175 unanunua numba nchi yoyote nyumba siyo apartment. hapo chini inauzwa 69.000$

Mkuu sasa huku ndiyo kuchanganya "apples" na "oranges", kuna factors nyingi kwenuye suala zima la uuzaji na ununuzi wa nyumba, lakini kuu kuliko yote ni demand and supply. Lakini pia mji, kitongoji,eneo. Nyumba yenyewe imejengwaje? Umri wake Sasa kama unayoinyesha hapo usikute imejengwa in 1920's ni ya mbao na inaonekana mahali hapo -40 deg. wakati wa winter in kitu cha kawaida tu.

Leo hii ukiangalia mfanno bei za nyumba Australia katika miji say yenye watu 100,000 mpaka 150,000 avg price for a 3 bed room house kwenye suburb nzuri, 10 yrs old, brick work ni around $350,000.00 (AUD) lakini ukienda Marekani nyumba kama hizo hizo na miji ya namna hiyo hiyo ni around $100,000 (USD). kUMBUKA 1AUD ni sawa na 1.15USD..

Sasa tukija hizo apts za Arusha, kwanza lazima ufahamu kwamba demand ipo na wateja wa kununua hizo nyumba kwa bei hiyo wapo. Lakini ukizibeba kama zilivyo ukazimwage Musoma hata kwa nusu ya bei unaweza usipate wateja. Cha msingi ni kwamba je shirika la umma halistahili kufanya biashara? Na kama linastahili basi je lina mikakati gani kuhakikisha linajenga nyumba za bei nafuu kwa ajili ya watanzania wa kawaida???

Na pia ikumbukwe anaweza kutokea tajiri mmoja akazinunua zote hizo, je shirika la nyumba linaruhusu huo utaratibu?????
 
Mkuu sasa huku ndiyo kuchanganya "apples" na "oranges", kuna factors nyingi kwenuye suala zima la uuzaji na ununuzi wa nyumba, lakini kuu kuliko yote ni demand and supply. Lakini pia mji, kitongoji,eneo. Nyumba yenyewe imejengwaje? Umri wake Sasa kama unayoinyesha hapo usikute imejengwa in 1920's ni ya mbao na inaonekana mahali hapo -40 deg. wakati wa winter in kitu cha kawaida tu.

Leo hii ukiangalia mfanno bei za nyumba Australia katika miji say yenye watu 100,000 mpaka 150,000 avg price for a 3 bed room house kwenye suburb nzuri, 10 yrs old, brick work ni around $350,000.00 (AUD) lakini ukienda Marekani nyumba kama hizo hizo na miji ya namna hiyo hiyo ni around $100,000 (USD). kUMBUKA 1AUD ni sawa na 1.15USD..

Sasa tukija hizo apts za Arusha, kwanza lazima ufahamu kwamba demand ipo na wateja wa kununua hizo nyumba kwa bei hiyo wapo. Lakini ukizibeba kama zilivyo ukazimwage Musoma hata kwa nusu ya bei unaweza usipate wateja. Cha msingi ni kwamba je shirika la umma halistahili kufanya biashara? Na kama linastahili basi je lina mikakati gani kuhakikisha linajenga nyumba za bei nafuu kwa ajili ya watanzania wa kawaida???

Na pia ikumbukwe anaweza kutokea tajiri mmoja akazinunua zote hizo, je shirika la nyumba linaruhusu huo utaratibu?????

Samahani mkuu kwa kutotoa informations zote. Najua demand imekuwa met huko Arusha. Nyumba hiyo ipo Toledo, OH ambapo sio kijjini sana ila siyo rahisi kuipangisha.Pamoja na hayo nini hakika kuwa huu mji upo industrialized kuliko Arusha, umbasli wa social services,etc, kuhusu winter, sijui sehemu nyingine duniani, ila US snow huwa effects zake kwa mwananchi wa kawaida ni negligibly small.

Barabara zinasafishwa nyumba zina a/c etc. Ila kama ulivyosema, demand inaruhusu bei hiyo. Kama demand inaruhusu bei hiyo, kwanbini unafikiri watu binafsi hawainvest heavily in housing? Kwenye mji kama Arusha?

Nadhani NHC wamepunguziwa regulatory constrains( I'm not sure) ili kuwajengea wananchi kama waalim, mapolisi, manesi etc waweze ku afford.
The point I was trying to make was, those apartments were expensive and they look like some projects. Hiyo ni biashara na wengi wataonunua watazipangisha kwa $.
 
Back
Top Bottom