frankshops
JF-Expert Member
- Jul 28, 2015
- 212
- 180
Watoto wa walala hoi wanalia ajira,watoto wa vigogo wanazidi kutesa kila leo, Kweli nimeamini nchi hii ina wenyewe ni mali ya familia za watu,Hta aibu hakuna,wanajazana kwenye nafasi,kwa upendeleo,kwani wengine hatuna elimu.Si mlidhike na ubunge?Vyeo vitatu vitatu wakati wasomi wengine Hawana ajira.Nimeona mkeka wa baraza jipya la Mawaziri, unajiuliza uchaguzi umeisha au bado tupo Kwenye kampeni? Watu waliopo Kwenye baraza la Mawaziri ni watoto wa familia zilezile zinazoelekea kustaafu au zilizostaafu.
Hakuna ufanisi, ubunifu wala mikakati ndani ya baraza bali wamewekwa watu wakumsaidia Mhe. Rais kupiga kampeni kuelekea uchaguzi ujao.
Baraza la Mawaziri kwa kipindi hiki halipaswi kujazwa watu wa propaganda, inahitaji watu wakufikiri kuhusu maendeleo ya nchi yetu.
Baraza la sasa limerejesha fadhila Kwa timu Jk baada ya miaka mitano ya mateso. Naiona Tanzania maskini huko tuendako