Maombi ni upotevu wa muda

Maombi ni upotevu wa muda

Kama maombi kweli kweli yatatatua matatizo, basi umaskini ungeisha, magonjwa yangeponywa, rushwa ingeisha, na majanga yangezuiliwa kwa kuomba tu kwa bidii.

Lakini uhalisia haupo hivyo.

Watu wanaomba kazi badala ya kujitengenezea fursa. Wanaomba uponyaji badala ya kutafuta matibabu. Wanaomba mabadiliko wakati hawafanyi chochote kuyaleta.

Maombi yanaweza kutoa faraja ya kiroho, lakini faraja si uthibitisho wa ufanisi.

Hatuhitaji kuomba suluhisho. Tunahitaji kufikiri kwa kina, sayansi, ushahidi, vitendo, na uwajibikaji.

Acha kusubiri msaada wa kimungu. Tatua matatizo ya kibinadamu kwa vitendo vya kibinadamu.

Taikuni la kuwastua wanaotapeliwa kiimani hasa wakristo Kubwa la Maadui
Ipo siku utayaitaji ayo maombi....
 
Watu tumekesha tukiomba Lissu aachiwe lakini wapi?
Wewe unasema hii?
Unawafahamu hawa

1. Askofu Kakobe
2. Askofu Jacob
3.Askofu Dickson Kabigumila
4. Mch Mbarikiwa.
5. Askofu Mwamakula
6. Pastor Rolinger
7. Nabii Denis Samweli
MImi BushDokta nilichukua muda wangu na commitment kuungana nao kwa kutangaza Ukuu wa Mungu, Rehema na baraka zake. Niliungana nao kuanzia Jan 2024. Tuliombea uchaguzi uwe wa Amani na Mungu akubariki kwa ajili ya Taifa la Tanzania na Wananchi wake.
Kilichotokea ni ushahidi 100% Mungu Hasikilizi maombi
 
Back
Top Bottom