Bramo nini India nenda Kenya katuonyeshe Mtanzania ambaye ni Diwani wa kule. Huu ni Ubaguzi wa kiwango kile kile cha wale wanaowabagua wenzao kutokana na dini zao. Kama Kenya Mtanzania hawezi kuwa Kiongozi ni kwa nini mtake Mtanzania akawe kiongozi India? Manji ni Mtanzania na ndiyo maana amechaguliwa kuwa Diwani wa Mbagala Kuu, ila yeye Kabila lake ni Mhindi kama Magufuli alivyo Msukuma!!
Ubaguzi ni kama ugonjwa, humpata mtu yeyote yule. Waulize watu wanaosoma masomo ya Jamii kuhusu saikolojia ya watu wachache (Minority) dhidi ya watu walio wengi kwenye eneo husika.
London watanganyika husema Wazanzibar wanawabagua, Dar es salaam wazanzibar wanadaia wanagandamizwa na watanganyika. Hisia za kubaguliwa na ubaguzi ni vitu viwili tofauti. Mzee Mohamed Said anadai kuwa Waislamu wanabaguliwa katika mfumo wa uongozi na Elimu. Ni kweli?
Mwambieni kuwa Yanga ni club tu ka Simba na Azam hata Toto Afr. Kuukwaa uongozi yanga si fagio la kuwafanya Watanzania wamthamini.
Wapo wanaotoa misaada mingi tu kwa ajili ya wenye shida mbali mbali, na bado hawajaomba hata ujumbe wa nyumba kumi. Yeye kuwa mfadhili wa Yanga tu ndo nchi yake imthamini?
Maji, jiulize umeifanyia nini nchi yako, si watu wamekufanyia nini. Mwaga misaada kila mkoa, Wekeza kwenye vyama vya kuondoa umasikini hata tubilioni tuwili hivi, kwani utafilisika? Mbona umeenda kuwabania wenzako kwenye udiwani hutaki watoto wa wengine wende chooni?? Manji, weye si wa kugombea udiwani tafadhali. Ungeomba Urais au ukishuka kidogo, uwe mbunge ka wenzaki kina Abood.
Ukitaka tukuthamini, kwanza jithaminishe kwetu
Mkuu,Mkuu
Nadhan wewe utakuwa Mhindi, sio bure
Dhulma na ufisadi alioufanya kwa Taifa hili halafu bado anakula pilipili za kihindi uraiani anahisi taifa lote ni jinsia ya kike kasoro yeye ndio sababu ana kebehi eti Taifa halimthamini. Kwanza yeye si Mtanzania aseme tu ana hati ya kusafiria ya Tanzania. HATA BAba yake Marehemu Mzee Ghulum alikuwa na pesa maarifa mengi ya kibiashara lakin hakuwa Mshenzi kama Mwanae. Kamdhulumu mpaka Dada yake wa Pekee mirathi ya Baba yake itakuwa Hohe hahe wa Mitaani!!
Bila shaka hapo wanaonekana kama wana kwao mwingine zaidi ya tz. Lkn vipi Mrugulu au Mgogo, ana mwingine. Sorry, but that is I see it. Back in 1995, wahindi wengi walihamisha familia zao wakisubiri haki ya Uchaguzi. Lkn akina Dionizi Na akina Mengi unadhani walifanya hivyo??
@Elli ndiyo Tanzania ni nchi yake kwani ana uraia wa nchi nyingine? Kuna tatizo la watu kuwaza kwamba wahindi siyo watanzania. Ni bahati mbaya sana!!
Yanga hata uwanja wa mazoezi hawana.ni kombe gani la maana yanga wamechukua.yanga imemsaidia manji.alikua hajulikani pamoja na mihela yakemagufuli anamchukia sana Manji, sijui alimfanyia nini...manji amesaidia watu wengi sana mpaka club yetu ya Yanga
Goodrich,
Nasikia harufu ya Ubaguzi.Mimi siyo Mhindi lakini kitendo cha kuanza kumlaumu Manji na kulalamika ati sehemu kubwa ya utajiri meshikiliwa na Wahindi naona ni upuuzi mtupu! Kwa maana hiyo hata kina Mo Dewji na Wahindi wote wafanyibiashara wakubwa hawatakiwi Tz?
Watz acheni wivu wa kijinga wa kuwaonea ghere jamii ya Waasia ambao ni wachakarikaji na watafutaji wa maisha walio makini kabisa na dunia inajua hilo.
Nenda USA,Canada,Uingereza,n.k utawakuta hawa jamii ya Wahindi wakimiliki biashara za uhakika!
Kama kuna mtu ana ushahidi wa Manji kuhusika na Ufisadi wa aina yoyote kama EPA,TEGETA ESCROW,CONTAINERGATE(TRA&TPA),DEEPGREEN,n.k atuwekee hapa ili tuanze kumchana live!
Hakika Kwa Mawazo Duni Waliyonayo Wachangiaji Wengi Humu Kama Taifa Tunasafari Ndefu Sana Kufika Huko Tunakotaka Tufike
Uhindi wala weusi si Utanzania. Mimi nitaendelea kuamini kuwa Manji ni mtanzania kama nilivyo mimi!! Huo ubaguzi wenu wa rangi wengine hatuwezi hata kwa bahati mbaya kuuvumilia. Huo ni UKABURU na ni lazima tutapigana kuutokomeza!!