Mandela Funeral: Live updates

Mandela Funeral: Live updates

JK kaongea vizuri sana japo alchomekea na kautani kidogo
 
Citezen television ya kenya wamesitistisha kurusha live baada ya kumwona Jk,jamani hawa wa kenya uwivu utawamaliza
 
Pale alipo ad-lib kuhusu Maria Nyerere kachemka kwenye grammar.

Kaongezea maneno yasiyokuwa kwenye hotuba....

Ila Nkwingwa, nadhani hii ni nafasi pekee kwa ulimwengu kufahamu mchango wa Tanzania katika Uhuru wa RSA na Africa kwa ujumla...
na Rais JK anaitumia ipasavyo...
 
'GoVT of TZ had build a radio station for liberation movement'
 
Waandaaji wa speech za rais wetu ni dhaifu. hotuba inaonesha zaidi matukio kuliko kuuleza undani wa matukio hayo na uhusiano na tukio la leo katika nyanja za diplomasia na uchumi.
 
JK anacheka hajui yuko kwenye msiba.

Ni kutokana na aina ya hotuba anayosoma..Ina visa vya kusisimua na wakati mwingine kuchekesha...Ndio maana unaona hata wasikilizaji wanacheka na kushangilia....
 
Serikali ya Tanzania ilikuwa ina redio maalumu ikitangazwa kutokea dar es Salaam ikitangaza kwa lugha za kusini mwa afrika...Viatu alivyoviacha Mandelaa kwa Mzee Nsiro Swai kabla ya kufungwa... alivikabidhi kwa Mandela alipotoka jela... Mama Swai yuko kwenye mazishi
 
Bila shaka Watz kwa leo tutaingia South Afrika wth warm welcome. Katangaza vizuri ukarimu wetu. Ila mnaopitisha unga mtatuharibia dili. Acheni washikaji, Kapuya et al.
 
Waandaaji wa speech za rais wetu ni dhaifu. hotuba inaonesha zaidi matukio kuliko kuuleza undani wa matukio hayo na uhusiano na tukio la leo katika nyanja za diplomasia na uchumi.

He is trying to make the connection............kuwa TZ waliplay kwenye contribution ya Independence..........
 
Kutokua na elimu kubaya sana, mama wa taifa nyerere angekua anajiweza hata kwa lugha tu angepewa nafasi ya kuhutubia leo

Kwa hiyo kujua Kiingereza ndo kuwa na elimu?

Na kwani angeongea Kiswahili halafu wakatafsiri kungekuwepo ubaya?

Mbona Dilma Rousseff pale FNB aliongea Kireno....
 
Oooh, Kikwete kanigusa na hotuba yake kuhusu uhusiano kati ya South Africa na Tanzania na kuhusu Tata Nkulu Madiba, Kikwete oyee!!!
 
Kikwete mwongo sana...anadanganya live...alimdanganya Obama kwamba umati uliojitokeza haujawahi kutokea...hapa andanganya kuwa umati uliojitokeza kumpokea mandela haujawahi kutokea na rekodi haijavunjwa........Uongo wa MaCCM mbaya sana
 
JK alivyotaja Mazimbu ameshangiliwa sana.
Pia,kakumbusha viatu vya Mandela alivyovisahau kwa Mama Swai,naye (Mama Swai) kapaishwa kuwa naye amehudhuria.Kashangiliwa pia.
 
Back
Top Bottom