Mandela Funeral: Live updates

Mandela Funeral: Live updates

Citizen wako juu, wanarusha wenyewe live toka Sauzi, sio kama maTBC yetu haya yanajikomba tu kwa SABC News. Kwa hali hii tutapona kauli ya Cameron kweli, yule waziri wa Uingereza.
 
JK, anapaswa achukue kitu hiki kwenye Hotuba ya Zuma, kuwa S.A inatumia elimu kama silaha yakupata maisha Bora. Na kuinua maisha ya wa Afrika kusini.

Yeye Bado analia na Kilimo Kwanza.
 
inaelekea wale wa dini nyingine hawakushiriki kuusaka uhuru wa sauzi...maana bwana zuma anataja majina hapa wote wanaonekana wa dini nyingine
 
Jamani rais wetu na wa Malawi ndio watu waliopewa nafasi ya kuongea mbona hamsemi. Amewajulisha namna tulivyomusaidia Mandela na Afrika ya kusini na vyama vingine kama FRELIMO , very excited! bright Prezoo.

JK katoa speech ya kitaifa kwa kweli. Safi sana!
 
Kuna jamaa hapa anaitwa Kolin Thumbadoo anafanya chanting kabla ya Zuma hajaongea. Huu utamaduni sijui maana yake nini? Kila watu na style yao!

Mwana utamaduni wa kizulu huyo, napendezwa nayo sana
 
Zile goli 6 (sita) Arsenal alizochapwa jana na Man. City sijui kama atazisahau ndani ya karne hii
 
Tumetoka kusikiliza dakika kumi tu zilizopita na hukumbuki alichoongea JK........

Au Thabo na Zuma kwako ni mtu mmoja...............hizi shule za kata zinatuzalishia nini jamani...
Ha ha haaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!
 
Duh, makofi kwa Zuma yanatafutwa kwa tochi! Jamaa sijui kama atarudi Magogoni ya Bondeni baada ya uchaguzi.

South Africa wanachaguwa chama boya wewe.

Kama hawamtaki hata leo wanamwondoa na chama kinateuwa mtu mwingine anaapishwa kuwa Rais. Msiwe mnakurupuka kwa msiyoyajuwa. Kuzomea ni kitu cha kawaida sana kwa nchi zenye demokrasia.
 
Aisee!!!

Kaunda anakaribishwa naye kutoa yake machache, anaelekea jukwaani kwa kukimbia.
 
Kumbe serikali hii ya Tanzaniandio iliyokuwa inafundisha watu kujilipua. wa South Africa wamekuja hapa wakapewa majina feki, wakaukana uraia wao na walipewa passports za kusafiria na mpaka leo hawajazirudisha.

HAYO SIYO MANENO YANGU

Bali ni maneno ya Mheshimiwa, Ndugu, Mwenyekiti, Rais, Dokta JAKAYA MRISHO KIKWEYE kwenye mazishi ya Mandela huko kijijini QUNU.

Jk amesema wazi kuwa huyu rais wa sasa wa South Africa bado hajarudisha passport aliyopewa ya Tanzania kusafiria

sasa cha kujiuliza je AMBOKILE na IMMIGRATION wanajua hawa wa South Africa wangapi wana passports za Tanzania na south Africa?

au tumeamua kusamehe?

kama ni kwenye intelligence bas JK amme mmade Zuma live dunia nzima imeona.

acha uongo wewe. Thabo mbeki
 
Back
Top Bottom