Al Watani
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 21,869
- 32,774
Ukiondoa Simba na Kaizer Chiefs Man United ndiyo timu inaendeshwa hovyo zaidi duniani kwa vilabu vikubwa.INEOS wasipofanya operesheni ya moyo hawatofika mbali.
Ni mchakato unaoweza kuchukua madirisha mawili makubwa ya usajili.
- Eriksen mwili wake hautaki tena kugombania mpira.
- Tukubali makosa ya kusajiliwa wan bissaka, level yake ni crystal palace.
- Varane bado ana kitu mguuni lakini mwili hautaki tena, majeruhi yasiokwisha huku akiramba mshahara mkubwa.
- Kulipa millioni 60 paundi kwa casemiro mwenye miaka 30 kwenye dunia yenye ruben neves, palhinha ni kosa jengine la kutoipa umuhimu future.
- Kwanini tulimsajili Onana ikiwa mfumo wetu wa uchezaji ni ule ule, tujiulize amekuja kuongeza nini, hapa kipara awajibike.
- Tuache tabia ya kupapatikia wachezaji kwa hoja mfu, tuliwahi kukataa kumuuza lingard kwenda newcastle kwa hoja ya kumuimarisha adui, msimu huu klabu imekataa 30 millioni kwa scott mctominay, ni kichekesho.
- Klabu ya mpira si hisani, luke shaw aonyeshwe mlango wa kutokea, amekosa mechi nyingi sana kwa hoja ya majeruhi na pia hana consistency.
- Nguvu aliotumia kipara kumgombania amrabat hailingani na anachomfanyia, hapa tumelipa paundi millioni 10 kwa mkataba wa mwaka mmoja, kosa jengine la kipara.
- Victor lindelof hawezi kuwa na miujiza na hatokuwa na miujiza.
Wachezaji walioko United hawawezi kuwa sehemu ya kikosi chochote cha vilabu vikubwa Uingereza,Spain au Bundesliga.
Tuna idadi kubwa ya wachezaji wanaopaswa kuhamia Serie A.


