Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

MATOKEO HAYAKUPI PICHA HALISI

Mtu akiona matokeo anaweza kuhisi mechi ilikuwa tight sana lakini ni Bayern ambao wakiamua kufunga basi unaona goli lileeee linakuja . United wakifunga basi Bayern kama vile wanasema " tunakuja kufunga goli letu tena " BANG .!

United walianza mchezo vizuri jinsi walivyokuwa wana press na kuwalazimisha Bayern kupoteza mipira hasa pale walipokuwa wanataka kutoka nyuma

1: Bayern walikuwa wanafanya build up na 2-3 ( Upamecano na Kim ) nyuma na mstari wa Laimer Kimmich na Davies

2: Lakini United walikuwa wanafanya pressing kwa 4-1-4-1 Hojlund anafunga njia ya pasi kwa Kimmich huku Rashy na Pellistri kwa Fullbacks wote wa Bayern : Bruno na Eriksen wanafunga njia za pasi zinazopita kwenye halfspaces zote mbili kwasababu ya Musiala na Goretzka .

Bayern baada ya kutulia na kuanza kupasia mpira vizuri , ndio shida ilipoanza kwa United

1: Musiala anakuwa maeneo ambayo anajua Casemiro na Eriksen hawawezi kufika na anajua akishapata mpira ni rahisi kupita katikati yao

2: Kane anashuka chini kidogo ili kufanya kazi ya Lisandro na Lindelof kuwa ngumu , kwasababu wakimfuata wanaacha space nyuma yao kwa Sane na Gnabry kuishambulia , wasipomfuata anapokea mpira na kupiga pasi kwa wingers wake

Aina ya magoli ambayo United wanaruhusu yanafanana sana msimu huu

1: Goli la pili dhidi ya Spurs
2: Goli la Martin Odegaard
3: Magoli yote ya Brighton
4: Goli la Gnabry

Yanafanana nini ? United wanashida sana ya kukimbia na runners wa timu pinzani ( tracking runners ) , cutbacks zinawafunga sana United msimu huu na timu zinajua hilo . Casemiro na Eriksen pamoja kwenye kiungo bila mpira ?

NOTE

1: Jamal Musiala kawapika sana viungo wa United

2: Kimmich muda wote anapicha kichwani kwake nini kinaendelea na nini afanye

3: Bayern bila mpira wanaacha space nyingi sana ni wewe tu kuwapa adhabu kama unataka

4: Goli la nne la Bayern , pasi , movement na finishing

5: Andre Onana wakati anaopitia sasa hivi

6: Man United katika mechi 5 zilizopita wameruhusu magoli 14

7: Kufunga magoli 3 ugenini na bado hujashinda mechi

FT: Bayern 4-3 Man United

#Ambangile

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
Ujuaji as usual
 
Bayern vs man u, game ilikua tofauti sana na watu walivyofikiria
Dakika 15-20 za mwanzo man u aliishika vizuri kabisa game.
Ata Bayern walipopata rhymes yao, still man u walikua bado wapo mchezoni

4-3
Ina maana Bayern alikua anafungika vizuri tu
Rashford anakosa sifa za kuitwa mchezaji mkubwa kwasababu ana mapepe Sana, na anachosahau kwa Sasa yeye ndio wakuibeba timu katika mechi Kama hizi

Kiungo ya man u, inakata Moto mapema sana, sababu ni umri

Mentality ya wachezaji ipo chini, hii inawafanya team kuwa underdog mchezoni

Pundits wangekuwa wanaenda mazoezini kutoa hamasa na sio kuishambulia timu kwenye media ingekua vizuri sana

Ten hag angemaliza tofauti zake na Sancho, asimame Kama baba, mtoto akinyea mkono hatuukati

Kuna uwezekano mkubwa Antony, amrabat, Sancho, mount, maino wangekuwepo Jana Mambo yangekua tofauti
Ndio maana shabiki wa man u aliesema Hawa wakija OT hawatoki, nilimuelewa Sana

Man u wamekosa nafasi nyingi, na wameshindwa kuzitumia nafasi nyingi kuliko hayo makosa ya Onana

Timu yenu inahitaji vitu viatau: utulivu, morali iwe juu, strong mentality
Kama unafatilia mpira vizuri, ni rahisi man u ku-bounce back kuliko chelaea

Bayern anakikosi kizuri wanakosa chemistry nzuri
Au wanakikosi Cha kawawaida lakini wanacheza kwa amsha-amsha tu
Au mentality ya kuwa timu kubwa bado wanaitumia vizuri

Ile Bayern akicheza na Brighton, anakufa vizuri tu
Rashford akiamua kutafta goli lawama ,akiamua atoe Pasi lawama , wachambuzi wa mchongo mnazingua sana
 
Bayern vs man u, game ilikua tofauti sana na watu walivyofikiria
Dakika 15-20 za mwanzo man u aliishika vizuri kabisa game.
Ata Bayern walipopata rhymes yao, still man u walikua bado wapo mchezoni

4-3
Ina maana Bayern alikua anafungika vizuri tu
Rashford anakosa sifa za kuitwa mchezaji mkubwa kwasababu ana mapepe Sana, na anachosahau kwa Sasa yeye ndio wakuibeba timu katika mechi Kama hizi

Kiungo ya man u, inakata Moto mapema sana, sababu ni umri

Mentality ya wachezaji ipo chini, hii inawafanya team kuwa underdog mchezoni

Pundits wangekuwa wanaenda mazoezini kutoa hamasa na sio kuishambulia timu kwenye media ingekua vizuri sana

Ten hag angemaliza tofauti zake na Sancho, asimame Kama baba, mtoto akinyea mkono hatuukati

Kuna uwezekano mkubwa Antony, amrabat, Sancho, mount, maino wangekuwepo Jana Mambo yangekua tofauti
Ndio maana shabiki wa man u aliesema Hawa wakija OT hawatoki, nilimuelewa Sana

Man u wamekosa nafasi nyingi, na wameshindwa kuzitumia nafasi nyingi kuliko hayo makosa ya Onana

Timu yenu inahitaji vitu viatau: utulivu, morali iwe juu, strong mentality
Kama unafatilia mpira vizuri, ni rahisi man u ku-bounce back kuliko chelaea

Bayern anakikosi kizuri wanakosa chemistry nzuri
Au wanakikosi Cha kawawaida lakini wanacheza kwa amsha-amsha tu
Au mentality ya kuwa timu kubwa bado wanaitumia vizuri

Ile Bayern akicheza na Brighton, anakufa vizuri tu
Huyu ndio mkorea yuleyule ninaemjua mimi?
Hii chambuzi kama ya 3 hivi naiona kutoka kwako ukiongelea Man Utd positive pamoja na matokeo yetu kua mabovu.
Hongera sana Mkuu naona akili yako imeanza kupevuka, chambuzi kama hizi kutoka kwa mtani wako wa jadi hua zinaongeza matumaini ya kuishi kwa watu waliojikatia tamaa pia inasaidia kupunguza suicide rates in sports
Nimependa zaidi hapo uliposhauri kua Pundits wangekuwa wanaenda mazoezini kutoa hamasa na sio kuishambulia timu kwenye media.
 
20230921_002545.jpg
 
Bayern vs man u, game ilikua tofauti sana na watu walivyofikiria
Dakika 15-20 za mwanzo man u aliishika vizuri kabisa game.
Ata Bayern walipopata rhymes yao, still man u walikua bado wapo mchezoni

4-3
Ina maana Bayern alikua anafungika vizuri tu
Rashford anakosa sifa za kuitwa mchezaji mkubwa kwasababu ana mapepe Sana, na anachosahau kwa Sasa yeye ndio wakuibeba timu katika mechi Kama hizi

Kiungo ya man u, inakata Moto mapema sana, sababu ni umri

Mentality ya wachezaji ipo chini, hii inawafanya team kuwa underdog mchezoni

Pundits wangekuwa wanaenda mazoezini kutoa hamasa na sio kuishambulia timu kwenye media ingekua vizuri sana

Ten hag angemaliza tofauti zake na Sancho, asimame Kama baba, mtoto akinyea mkono hatuukati

Kuna uwezekano mkubwa Antony, amrabat, Sancho, mount, maino wangekuwepo Jana Mambo yangekua tofauti
Ndio maana shabiki wa man u aliesema Hawa wakija OT hawatoki, nilimuelewa Sana

Man u wamekosa nafasi nyingi, na wameshindwa kuzitumia nafasi nyingi kuliko hayo makosa ya Onana

Timu yenu inahitaji vitu viatau: utulivu, morali iwe juu, strong mentality
Kama unafatilia mpira vizuri, ni rahisi man u ku-bounce back kuliko chelsea

Bayern anakikosi kizuri wanakosa chemistry nzuri
Au wanakikosi Cha kawawaida lakini wanacheza kwa amsha-amsha tu
Au mentality ya kuwa timu kubwa bado wanaitumia vizuri

Ile Bayern akicheza na Brighton, anakufa vizuri tu
Leo kwa mara ya kwanza nimeona umeshusha nondo za kweli big up sana mkorea.
 
Huyu ndio mkorea yuleyule ninaemjua mimi?
Hii chambuzi kama ya 3 hivi naiona kutoka kwako ukiongelea Man Utd positive pamoja na matokeo yetu kua mabovu.
Hongera sana Mkuu naona akili yako imeanza kupevuka, chambuzi kama hizi kutoka kwa mtani wako wa jadi hua zinaongeza matumaini ya kuishi kwa watu waliojikatia tamaa kupunguza suicide rates in sports
Nimependa zaidi hapo uliposhauri kua Pundits wangekuwa wanaenda mazoezini kutoa hamasa na sio kuishambulia timu kwenye media.
Jamaa kashusha nondo za ukweli sana.
 
Huyu ndio mkorea yuleyule ninaemjua mimi?
Hii chambuzi kama ya 3 hivi naiona kutoka kwako ukiongelea Man Utd positive pamoja na matokeo yetu kua mabovu.
Hongera sana Mkuu naona akili yako imeanza kupevuka, chambuzi kama hizi kutoka kwa mtani wako wa jadi hua zinaongeza matumaini ya kuishi kwa watu waliojikatia tamaa pia inasaidia kupunguza suicide rates in sports
Nimependa zaidi hapo uliposhauri kua Pundits wangekuwa wanaenda mazoezini kutoa hamasa na sio kuishambulia timu kwenye media.
Ushabiki katika kuchangamshana tu
Sometimes ushabiki tunauweka pembeni, tunaongea uhalisia
 
Nawashangaa ,hawajui baryen ya Sasa Ni ovyo Sana ,juzi hapa wamekimbizwa na kina Xhaka ,

Narudia Tena baryen,Madrid sio Timu tishio kwasasa

Wanaoendelea kuamini katika majina waendelee

Madrid sio kila siku Jude atawaokoa dk za mwisho
Madrid wamedumazwa na Upuuzi wa Kumfatilia Mbappe kipindi chote cha usajili, Mpk usajili umefungwa na Sasa Wameingia kwenye msimu Bila Namba 9,

Aisee nawaonea huruma wakikutana na Timu kama Man city UEFA maan watatandikwa goli Si chini ya 3 kuanzia Home & Away
 
Bissaka,mount,varane,Shaw,malacia,amrabat,antony,kobbie maino,sancho sina
Wachezaji angalau wengi hapa wakirudi na waliopo na matokeo yakiwa hv basi ndo ntasema kocha mbovu
 
Ushabiki katika kuchangamshana tu
Sometimes ushabiki tunauweka pembeni, tunaongea uhalisia
Kabisa mkuu, Masingeli yeye anajiita mchambuzi lakini chambuzi zake zimejaa ushabiki mwanzo mwisho hataki kabisa kuzungumzia uhalisia wa mambo anakua hana tofatauti yoyote na kina Flano
Ethics za uchambuzi unatakiwa usiwe biased, hivyo vitu ndio vinamfanya Geoge Ambangile akubalike na mashabiki wa timu zote katika chambuzi zake sio kama kina Edo Kumwembe ambao kweli mpira wanaujua ila wameamua tu kwa makusudi kujifanya ni comedians.
 
Back
Top Bottom