Wengi wao huwa ni wafuata mkumbo tu Antony ni typically Man utd player, anayo fighting spirit ambacho ndicho kigezo kikubwa cha wachezaji wa united kitu ambacho Rashford, Sancho na Martial hawana.
Ukifuatilia sajili zote za Ten hag amesajili watu fighter na wabishi wabishi yaani aggressive pale wabapokuwa na mpira, Anzia Mallacia, Antony, Casemiro, Matinez, Mount na sasa Hodjlund. Kinachomkwamisha kwa sasa ni kuwachanganya vijana aliyewasajili na hawa wavivu kina Rashford hapa atakwenda kuanguka, ni lazima aangalie namna ya kucheza bila hawa wavuvi ikiwezekana wawe wanatokea benchi wakati biashara imeshaisha.
Sasa wanakuja wachambuzi uchwara humu wanajaza server ukisoma uchambuzi wao unaishia kusikitika tu na kujiuliza hivi hawa wanaangaliaga mpira kwel?