Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hizi sasa zinaweza kuwa chuki binafsi kwa EtH. Ni sawa kutomkubali EtH kwa points zako ulizotoa.

Ila siamini kuwa anasajili wachezaji ilimradi tu. Kama unahisi hivyo utakuwa unakosea. Ni mtazamo wako tu, EtH anasajili kulingana na vile anavyotaka timu yake icheze.

Tatizo kubwa nililogundua kwa mashabiki wa United tumeshazoea sajili za majina makubwa. Hapa angekuja Bellingham ungeongea tofauti kwasababu ni mchezaji ambaye yupo kwenye spotlight ila usajili wa Mount unaona ni wa ilimradi tu bila kuangalia ni namna gani EtH anataka timu yake icheze.

Kingine siyo kitu rahisi kocha kuwaongelea vibaya wamiliki / waajiri wake. Hilo ni jambo ambalo ni ngumu sana kutokea. Solskjaer alivyokuja kuwasema Glazers baada ya kufukuzwa kazi watu walimtukana kuwa kipindi ameajiriwa alikuwa ni mzee wa "YES" ila ukiwauliza ni wangapi walio kwenye ajira wanaweza kuongea kauli zenye ukakasi kwa waajiri wao? Jibu baki nalo.
 
Naona umemtukana Luke Shaw. 😂

Nitajie top 5 ya left backs bora kwenye EPL.
 
Tatizo lako ushabiki unakutoa kwenye facts.

Rashford, Shaw, Bissaka, Lindelof hao wote hujaona walivyo-improve msimu huu!? Plus introduction ya Garnacho EPL ameweza ku-manage na kumfanya kijana mdogo tu kuwa na impact kwenye timu, yote hayo huoni.

Huoni kwasababu wewe ni "deluded fan" umeshaamini uwezo wa EtH ni mdogo so utatafuta namna yoyote ile ilimradi uamini EtH atafeli United.

Unavyoandika mambo ni kama vile Arteta hana sajili mbovu, kama vile alikuja tu then paaap in a blink of ana eye Arsenal mnagombea ubingwa.

Rebuild inahitaji muda, EtH alichukua kikosi ambacho siyo chake. 90% alitumia wachezaji ambao siyo wake.

Ronaldo ni fala tu na naungana na kocha kutimuliwa kwake. Weghorst alikuja kwasababu Glazers hawakutoa pesa ya striker.

Malacia hakuja kum-replace Shaw. Najua unajua kuna kitu kinaitwa "squad depth".

Antony ni raw talent na EtH anaamini anaweza kumsaidia kufika full potential, tatizo lipo wapi? Kwanini Arsenyani mnaogopa? Kwasababu mnajua United inaanza kurudi wakati ambao nyie bado hamueleweki. Yani United iliporomoka imekukuta kwenye shimo na wakati wewe unajaribu kuondoka na yenyewe inaondoka, hicho ndiyo kinachotokea. Miaka 7 hamjawahi kusikia UCL anthem pale Emirates lazima muogope.

Rashford alifunga 5 goals kabal ya EtH. Casemiro wala usim-judge, Arsenal hamtawahi kuwa na kaliba ya mchezaji kama yeye. Amerudia mara kadhaa kulibeba taji la UCL Arsenyani mtaishia kuota hata hilo moja tu.

Eriksen, what a player! Msimu huu ndiyo atatusaidia zaidi kwasababu most of the games ata-cover Money Mase, Mason Mount.

Arsenyani kaa kwa kutulia. Hii tunaita Scary Hours.

ANDRE ONANA, WHAT'S MY NAME???
 
Umeandika kwa hasira Sana

Nilijua utakuja na utetez wa Rashford,Garnacho , ila sababu umejitia upofu huwez ona kuwa Rashford alishakuwa Moto hata kwa ole alifananishwa had na kina mbappe ,

,Shaw,bisaka hata lindelof ni wale wale , bisaka aameongezeka kipi? Kama Kross bado hajui kupiga ,Zaid ni yule yule mfalme wa tackling

Garnacho mwenyewe ni mpaka atokee bench sio mchezaji wa kuanza ,kipi Sasa amemuongezea?


Ukweli Ole gunar ana uwezo mkubwa kuendeleza vipaji na ni Talent ID ,kuliko ETH

Eth alimsajili Malacia akiamini Shaw ni flop ,kitu ambacho tunajua sikweli ,mwisho malacia ndiye anaonekana flop tu
 
Umeandika kwa hasira Sana

Ila Rashford,Shaw,bisaka hata lindelof wapo hivo hivo toka kwa ole ,
Upo sahihi hawabadilikagi but kuna sehemu huko nyuma ulisema eti kocha kashindwa kuwapandisha viwango


Hao watu wamepita kwa makocha watatu kabla ila hawabadilikagi tusimpe mzigo mzito ETH

Hata mimi Rashford pamoja na Shaw ambaye aliwahi kuwekwa nje na Brandon Williams wote siwawekeagi expectations kubwa.

Shaw huwa anacheza vizuri akiona ana hatari na kupoteza namba kwa backup wake ilikuwa hivyohivyo kabla hajaletewa Telles alikuwa mzembe kupindukia but alivyoona kaletewa Telles akapambania nafasi alivyojihakikishia namba akarudi default settings.

Rashford pia anacheza kifaza kwa kuwa hana mtu threat kwa position yake so hanaga presha hata akicheza pumba kiasi gani bado ana uhakika wa kuanza.
 
Shaw sijawahi kuona shida yake kubwa huwa anahitaji competition tu ,maana katika LB Bora watano EPL ,Shaw humkosi ,

Yeye huwa anataka mletee mtu anayejifanya anaitaka namba yake

Rashford kwasasa ni umri wake wakuwa peak miaka 25-27 ,ni muda wachezaj wengi wanakuwa peak katika football
 
Unarudia kuandika yaleyale kwasababu huna facts za kuthibitisha unayoyasema.

Ni uongo kusema EtH haja-improve kiwango cha Rashford.

2022/23 Rashford Stats

EPL
22 G/A

UEL
8 G/A

EFL
8 G/A

FA
3 G/A

Total: 41 G/A
Credits kwa EtH na McCarthy

Leta proof kama kuna msimu Rashford aliwahi kufanya hivi.

Kama Arteta anajua sana kwanini haku-improve viwango vya wakina Mustafi?

Vieira, Lokonga, Willian, Soares wote si alisajili Arteta? 😂
 
Soma hapa chini ni makocha wawili, mmoja licha ya kubeba europa na kumaliza nafasi ya pili bado alihitaji at least wachezaji wapya watano, Huyu mwingine licha ya kupewa fuko la goli saba bila na looser fool, kapigwa sita na manshity still anakuambia ameridhika na kikosi chake

Imagine huyu ndio kocha tunategemea aturudishe kwenye glory days
 
Usiamini sana maneno ya kocha na kikosi chake.

Ninachokumbuka mara ya mwisho mtu kuongea ukweli kwenye media "Ralf Rangnick" alitimuliwa na Glazers.

EtH ni muajiriwa, pamoja na mapenzi yake na football anatafuta pesa. Usitegemee atoke hadharani aanze kusema sitaki hawa wachezaji hawanifai au awaseme wamiliki hawatoi pesa, ukisema hivyo maana yake mwajiri atatafuta competent candidate kuendana na mazingira ya kazi maana wewe umeshindwa.

Wachezaji ni binadamu, kama kocha kazi ya kwanza ni kuhakikisha wana imani na wewe. Sasa ukisema hawakufai inapaswa uwe umejiandaa kuwaondoa.

Chukulia mfano wewe ni mchezaji na una mkataba na timu halafu kocha anaenda kwenye media kusema hauna uwezo wa kufanya naye kazi. Wewe kama binadamu hiyo kauli utaipokeaje?
 
Ngoja nikuache tu maana hautaki kuelewa , Kuna wachezaj ni flop au hhawaingii katika mifumo , but sijawahi ona uwezo wa kutisha wa ETH hapo manjesta wakukuza au kumtoa mchezaji point A had tukashtuka , hatukatai Kuna wachezaj ni wabovu wanajulikana hata Arteta aliwakuta na wengine aaliwasajili kwa pesa ndogo tu ,

Ila ninapozungumzia Talent ID ,ETH ni wakawaida Sana hata kwa Ole gunar ,kuanzia sajili alizokuwa ana point, kuanzia wachezaj aliowapa nafasi

Leo Sancho, mctominay,Fred , n.k tunaambiwa wote ni wameshindikana kufundishika , lakin Kuna aliowasajili Kama Weghost, Anthony,malacia , hatuoni upgrade yoyote ,


Pale Arsenal ,Arteta alimkuta Saka ni beki, Martinelli yupo U21 ,hafikiriwi kuja senior team kupenya , alimsajili regelated GK, na a lots of players ambao hawajulikan now wamepanda viwango , hata factor ya Rice kuja Arsenal anasema anaamini atatoka point A kwenda B,
 
Ni vizuri kusubiri msimu wake wa pili kum-judge. Hata Arteta alipewa muda na makocha wote hawawezi kufanana namna watakavyofanya kazi.

Ila stats hazidanganyi makocha wote post SAF wamezidiwa na EtH kwenye msimu wao wa kwanza.
 
Ni vizuri kusubiri msimu wake wa pili kum-judge. Hata Arteta alipewa muda na makocha wote hawawezi kufanana namna watakavyofanya kazi.

Ila stats hazidanganyi makocha wote post SAF wamezidiwa na EtH kwenye msimu wao wa kwanza.
Mm nakubaliana na wewe kuzidiwa msimu wa kwanza ,ila lazima Kuna key points tuziangalie ,ambazo zitasaidia kujua mbelen atafika mbali zaidi,

Kwangu mm Ole gunar anabaki moja ya watu wenye talent ID kubwa ni vile hakupewa Uhuru,huyu ndiye aliwataka kina halland, Bellingham,Sancho,n.k wakiwa hawaeleweki, huyu ndiye alimuamin Greenwood had leo mnamkumbuka

Niliwahi fanya mijadala huu na ambangile anaamini ETH kwenye Talent ID bado kwa Ole ,ila anaweza kuwa na mbinu nzuri za ukocha kuliko ole Gunar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…