Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kwenye Media anasema yeye Ni muumini wa total football



Nyuma ya pazia anamlazimisha Degea abaki

Dalot abaki

Varane miguu Kama banio abaki

 
Hiv rebuild ya man utd itaisha lini kama kila msimu tunanunua wachezaji 2-3 halafu mmoja ndio anafit kwenye mfumo?
Mbaya zaidi timu ikipata afadhali kwenye kiungo beki zinakuwa ovyo kuliko maelezo,ukipatia beki idara ya ushambuliaji inatetemeka kama imekatika sentabolti.

Jana Sevilla walijua udhaifu wa centerbacks wetu ndio maana wakaongeza presha kwa pressing ya kutosha na ikawalipa,hawakutoa mguu kwenye pressing hadi man utd ikaonekana timu ya championship.
 
Rebuild imeanza upya. Tatizo kubwa la United ni kwenye kusajili. Miaka iliyopita wako radhi watumie £80m kwa mchezaji mmoja wakati hiyo pesa ingeweza kutumika kuboresha eneo zaidi ya moja.

Mfano dirisha lililopita €100m kwa Antony ni kosa lingine timu ilifanya, ile pesa ingeweza kutumika kusajili RW na CB wa maana tu kutoka palepale EPL.

United shida kubwa ni kwenye uongozi, rejea ishu ya Ronaldo ilikuwa haina mantiki yoyote ktk kuboresha kikosi ilikuwa ni kama "statement signing" tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…