Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Timu yetu ya utd bado ina average players wengi sana leo tumefunga magoli yote manne. Ila bado nasema ya kuwa pamoja na kwamba Antony watu wanamdharau ila timu yetu inapata tabu sana pale anapotoka.
Bruno na Antony ni muhimili mkubwa sana wa timu kwa sasa.
Sijui kulikua na umuhimu gani wa kufanya sub za hawa watu kwa pamoja?
Sub ya muhimu ilikua ni ya Sancho tu, hata huyo Martial leo hakustahiki kutoka.
Draw ya leo lawama zote tunambebesha kocha maana sio mara ya kwanza wala ya pili kufanya sub zinazotucost.
 
Mi nimeliongelea hilo ..sub zilikuwa mapema sana na kwa watu muhimu mno...
Tunahitaji kuwalinda wachezaji ni sawa ila kwa hii timu yetu tia maji ndo tatizo.
Magoli 2 yalifungwa mapema sana ila wachezaji wakarelax na kocha akajiamini akafanya sub.
 
Le captain Maguire ndio Man of the Match, pamoja na kusugua bench kwa muda mrefu ila bado ana uwezo wa hali ya juu wa kufumania nyavu

Le Captain wetu atake asitake apewe mkataba wa maisha hapo Old Trafford na akistaafu kucheza soka apewe timu awe kocha.
10 Hag kama kweli ni muungwana leo anapaswa kusimama nje ya geti la OT na kuruhusu kila shabiki anaetoka uwanjani amtie kwezi kwenye hio solar panel yake.
 
Kitu na uhakika nacho ni kwamba
2nd leg Shaw,Rashford,Varane,AWB watakuwepo na Case,Fred,MCtominay wote watakua Fit sidhani kama Sevilla atatufanya kama alivyotufanya kipindi kile itakua FEDHEHA SANA aisee
 
Ni kweli ila kocha mimi simlaumu kiufundi alipokuja hakuwa hivyo ila kwa sasa kutokana na majeruhi yanayoiandama timu yetu mara kwa mara nahisi kocha naye ni kama kavurugwa anahofia kupata majeruhi hivyo wakati mwingine analazimika kujilipua. Fikiria timu inapigania pig 4 bado kombe la FA na EUROPE kwa average player tulionao kisha ukapata majeruhi ua wachezaji muhimu kama Rashford ni lazima kocha uchanganyikiwe coz unaweza poteza vyote kumbuka ligi bado ngumu. Arsenal mwenyewe na ubora wake anapambania ligi tu na anaweza asipate hilo kombe.

Hawa Sevila leo tuliwazidi kila kitu naamini hata kwao tutawafunga tu coz sikuona walichotuzidi kiufundi, ETH hajapoteza mechi yeyote Espian msimu huu naamini na hii hawezi ipoteza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…