christeve88
JF-Expert Member
- Aug 11, 2018
- 3,150
- 5,065
Mkuu hapo siwezi kukuelewa kirahisi, uwezo wa Chicharito, Rafaeli na Van Persi unaeleweka pale united. Swala la kutofanya vizuri huko walikoenda hii kwangu sio hoja.sababu hajapewa watu wake anaowataka, in real life mpira sio kama Fifa na Pes unachukua timu unacheza,
LVG alikuwa wazi kabisa anataka nini na hakupewa anachotaka so akachukua hao watoto. LVG ana UEFA ubingwa wa La liga, Bundesliga, Ligi yao uholanzi etc. katoa malegend kibao, hajaanza ukocha na UTD.
angalia wachezaji walioachwa na LVG kama Rafael, Nani na wengineo walifanya nini walivyoondoka UTD? si tu timu kubwa hazijawataka, hata hizo ndogo hawakucheza vizuri.
Yule mzee pamoja na kufanya vizuri huko kwingine ila utd alifail kama hao wakina Rafael walivyofail huko kwingine. Unasema kocha hakupewa anachotaka? Wewe ulitaka apewe nini wakati alimnunua Di maria na Falcao wakiwa onfire akashindwa watumia. Yaani mimi yule mzee hapana kwa kweli nilipitia kipindi kigumu sana wakati wake.