Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Na Nyie mlitufunga tukiwaje, ule mchezo tuliteleza tu, Kwa Arsenal kwa sasa the real test ni Man City tu...wengine labda wabahatishe.
 
Kwa mashabiki waliopo Afrika, upinzani wa Arsenal dhidi ya Manchester united sijui utaishi lini.

Nyakati zile timu mbili hizi zilipokuwa kwenye kiwango bora tulishuhudia upinzani wa maneno usiokwisha.

kushuka kwa viwango kwa timu zote mbili nilitegemea upinzani wao utafishwa na ujio wa timu kama chelsea na manchester city ila hali bado imebaki kuwa vile vile.

Ni makelele yasiokwisha.
Mashabiki wa timu mbili hizi wanahitaji tuzo maalumu.
 
Rudia tena game ya united vs Arsenal alafu uje kuandika upya ,najua itakusaidia kujiamdaa kisaikolojia namna utakavyopigika hapo Emirate,najua kuwa wajua ila nataka ufanye reinforcement.....tuliwapigia soka la uhakika....

Emirates stadium ni KABULI LA WAGAGAGIGIKOKO KAMA NYINYI

ATMOSPHERE YA PALE HAMUWEZI KUIKABILI
MTAPIGIKA MCHAKAE
 
Lini united aliwahi dominate game na aseno

Toka enzi ya wenger nyie ndio mnaokamata game ila ubao sasa unasomaje mi sijui
Aisee kama kuna ukweli hivi maana hata ile mechi ambayo United anashinda goli 8-2 Arsenal aliongoza ball possession. Nakumbuka hata mechi ya mwaka 2001 ambayo United alishinda goli 6-1 pia Arsenal aliongoza kwa kumiliki mpira.
 
Arsenal ya kawaida sana na jana defense yenu imekuwa exposed na Brighton.

Brighton ndiyo timu pekee ukiacha United imeonyesha udhaifu wenu ni vile tu na wao walikuwa na makosa mengi ya kiulinzi na udakaji.
Kwamba????🦻🦻 Ongeza volume kidooooogooo....
 
Full fit Rashford na Martial, City anafungika.
Mkuu Chief mie huwa unanivutia sana kwa namna ulivyo optimistic na timu yetu hata iwe ovyo kiasi gani.
Vile vile sijawahi kuona ukimkosoa mchezaji yeyote wa united hata awe out of form kiasi gani,utapata positive 2/3 utamsemea tu.

Mfano mzuri ni kuhusu Anthony,kijana ameanza kuwakatisha tamaa mashabiki nami nikiwa mmoja wao lakini umemtetea kwenye angle ya defensive contribution yake kama vile alikuja mahsusi kwa ajili ya hili.

Wewe ni mfia timu kwakweli mkuu,big up.
 
Tuuze anthony pale tumepigwa,sehemu ya kutoa pasi yeye anapiga danadana[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Timu yetu imeanza kuimarika sana kwenye maeneo mengi.

Tunacheza vizuri kwenye phase zote za uwanja japo bado yapo mapungufu madogo madogo ambayo ni ya mchezaji mmoja mmoja.

Sasa hivi timu yetu ikiwa inacheza unakuwa unajua kuwa at any time tutafunga goli lakini pia unakuwa huna wasi wasi wa kufungwa easy goals.

Kama Erik Ten Hag ataendelea kupewa support kwenye madirisha ya usajili ni vyema kuimarisha kwenye eneo la full backs zetu pamoja na kusajili striker mmoja mwenye kaliba ya Cavan, Zlatan Robin Van Persie au Kane changamoto ni kwamba ni ngumu kupata striker wa kaliba hiyo sokoni.

Mwalimu amefanya vizuri kwenye kudistribute magoli kwa wachezaji mbalimbali hivyo timu inakuwa siyo predictable sana wakati wa kushambulia na kwa kiasi fulani tunakuwa dangerous.

Bado kuna mapungufu fulani upande wa kulia hasa kwa Anthony bila shaka bado hajakomaa au hataki kubadilisha art yake ya uchezaji eneo la kulia bado siyo threat sana kwenye kutengeneza magoli tunatakiwa kubadili sana eneo hilo, Anthony siyo mchezaji mbaya sana japo tangu mwanzo sikuwa nakubali uchezaji wake lakini naona ameongeza kitu defensively ana track back vizuri na mikimbio yake ina faida changamoto ni end product yake.

Kuna tetesi za usajili kwa wachezaji kadhaa hasa Joao Felix kwangu mimi naona tulichelewa sana kumpata Joao napenda resilience yake, fighting spirit na technical ability yake lakini uwezo wa kucheza maeneo tofauti tofauti uwanjani.


Kwenye eneo la ushambuliaji mtu pekee anayeweza kuturudisha kwenye reli ni Harry Kane, japo wapo wengine kama option Benjamin Sesko, Lautaro Martinez pamoja na Patrick Schick.


Kifupi msimu huu kama mechi zetu tatu zijazo hatutapoteza point nyingi huenda tukarudi kwenye mbio za ubingwa rasmi ifikapo February.
 
Kama tunapata short term striker january kwa mkopo, dirisha kubwa la Usajili Harry Kane ni rahisi kupatikana.
 
Kivip! Mkuu
Anaingia mwaka wake wa Mwisho wa mkataba, asipouzwa anaondoka bure, so ni Either aongeze mkataba ama auzwe dirisha lijalo.

Timu iliokuwa inamtaka Kane ni City na wameshamnunua Haaland, Liverpool wana Nunez, so inabaki Sisi na Chelsea labda na timu za Nje ya Uingereza.

Kama tupo serious anapatikana.
 
Sasa mkuu kane atakubali kweli kuja kwetu!,, maana hawa wachezaji ambao bado wapo kwenye fomu nzuri. Na wana uhaba wa vikombe maranyingi huwa wana option za kwenda vilabu wavitakavyo.

Vyenye uwezo wa kubeba kombe la ligi,uefa e.tc ili kutengeneza rekodi zao vizuri katika maisha yao ya soka, nasio mda wote wanatanguliza sana pesa mbele. Unazungumziaje kuhusu hili chief.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…