Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Acha kuteseka,TIMU ITAWAUA HIYO

 
Tatizo mnabetia timu mnazozipenda ndio mnaumia double double
 
Hujaongea point ata moja
 
Umepanik Sana ,ila hi Ni football tu, haina haja ya kutoa matusi

Ten hagg amepewa £250m dirisha moja ,lakin timu inarukaruka tu,

Ili muanze hata kucheza angalau hata kiwango alichofikia Ole Gunnar inambidi Ten hagg apate madirisha manne na kila dirisha apewe £250m , kifupi atumie £1Billions .

Naona mnatamba kipind Cha pili mlimkamata Pep 🤣🤣🤣

Mnashindwa kung'amua Pep tayari alishapata matokeo ambayo kwavyovyote alijua hamuwez kuyarudisha, ana mech ya UCL ,ana majeruhi ,

Mimi Kama mdau wa Epl nataka nione kwa mpira huu wa Ten hagg wa ujanja ujanja akiokota point ngapi hapa


Manchester United's next six fixtures:

Everton (A) - October 9

Newcastle (H) - October 16

Tottenham (H) - October 19

Chelsea (A) - October 22

West Ham (H) - October 30

Aston Villa (A) - November 6
 
Hizi game zote kwa manyumbu ni ngumu sana
 
Lakini waaaapiiiiiii


FA nao pia wajiangalie, sio kila mchezaji anapewa tu kibali cha kuchezea Premiere league, kuna wachezaji wengine wametumwa makusudi kuja kutuharibia ligi yetu pendwa baada ya kelele za "EPL ndio ligi ngumu zaidi duniani" kua nyingi.
 
Furaha ya mpira ni pamoja na kupoteza kama hivi.

Uimara wa timu unakuja kufatana na kupoteza game.
Kweli kabisa maisha bila changamoto hua yanakosa msisimko.
Mechi ya jana kulikua na mistakes za hapa na pale ila kipindi cha pili vijana walionyesha mabadiliko makubwa sana, nimeongea na Ten Hag amenihakikishia kua mapungufu yote yaliyojitokeza jana ameyaona na atayafanyia kazi na ile kauli yake ya "Eras come to an end" bado iko palepale.
 
awa city nao wasipotibu tatizo lao la kuluhusu migoli ovyo itawachukua muda mrefu sana kubeba ligi ya mabigwa barani ulaya
Mkuu...Sitaki kusema sana ila Historia inaonyesha Mabeki wengi wazuri...huwa wakipata injury tu basi wanaporudi viwango vyao huwa chini na huwa wanapoteza form zao.

Mfano: Van Djik wa Liver saiv ana kiwango cha chini tofauti na alivyozoeleka awali na hii ni tokea amerudi injury hayuko sawa kabisa. Tukiiangalia City vizuri unaona kabisa ata Dias tokea arudi kutoka majeruhi amepoteza ubora wake na vivyo hivyo ata kwa Larpote ambaye amerudi jana.

Kumbuka Stone naye yupo injury pamoja na walker jana pia, kwahiyo challenge kubwa ya wachezaji wazuri ni kupata majeruhi ambayo City yanawaandama sana kwa sasa, Na ukiangalia vizuri saiv Uhai wa ukuta wa City ni yule Akanji(waliemsajili majuzi kutoka Dortmund) na Ake ndo wanaafadhali pale nyuma...wengine wapewe muda watarudi kwenye ubora wao ila kwa umri wa walker(32yrs) tena katika EPL...hana kiwango kibaya ila naona kabisa mwisho wake unakaribia maana injury ni nyingi kwake.

Lakini ata kama kuna kuruhusu magoli...kikubwa pawe na forward kali zenye accuracy ya kufunga magoli mengi ili Kucompasate kwenye goals difference...na hiki ndicho kitakachowasaidia City uwepo wa haaland pale mbele, kikubwa awe fit asipate majeruhi nayeye.
 
Ndugu Mie City ila lile goli la Antony ni FAR-POST ya hatari, kijana ana kitu mpeni muda na nachokiona mkitaka mpate THE BEST OUT OF ANTHONY...acheni kupaki basi mcheze mpira wa kutandaza.

Na ili litawezekana kama mtampata beki mzuri mwenye kimo atakayeweza kucheza na Martinez(huyu yupo vizuri ila mfupi)...kwa varane bado na jana goli la haaland la pili ni kosa lake kabisa KIPA KAJITAHIDI KUBANA GOLI ALIVYOWEZA JAPO KUNA UPENYO ULIUACHA NA HII YOTE DE GEA ALIAMINI ULE MPIRA UTATOKA NJ'E...sasa ilitakiwa yeye Kama beki wa mwisho asiruhusu ule mpira kumpita yani angeuosha(swipe) kabla ya kwenda kukutana na Jini haaland pembezoni mwake na kupenyeza kwenye ule ule upenyo mdogo ulioachwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…