Manchester United (Red Devils) | Special Thread

bado hatujawa na usawa wa kikosi licha ya kuondoka kwa hao wachezaji 6 uliowataja, changamoto kubwa tulionayo ni kuwa na kundi kubwa la wachezaji wenye taathira ndogo sana ya kiuchezaji jambo linalopelekea kuwa frustrated.

licha ya kuondoka kwa hao wachezaji walioishiwa mikataba yao lakini bado tunao wachezaji hawa wa kikosi cha kwanza waliotolewa mkopo, bahati mbaya sana hakuna mwenye uwezo wa kufikia matarajio yetu ndio maana tunawaza usajili.

facundo pellistri + amad + anthony martial + tuanzebe + james garner +tahit chong + teden mengi + levitt​
 
Tuna mabeki wa kati 7, Maguire, Varane, lindelof, Bailly, Jones, Tuanzebe na Mengi hapo Mpaka wauzwe watatu ama zaidi ndio tuanze kufikiria mengine.

Winga wa Kulia Tumenunua sana Sasa hivi elanga anacheza Kule, Amad, Pellistri na Sancho ukitoa Sancho wengine hawaeleweki eleweki ngoja Kocha awaangalie wengine watoke kwa Mkopo.

No 10 nayo kama Anakuja Eriksen ina maana wapo wengi pia, VDB, Bruno, Perreira na Eriksen inabidi auzwe Perreira hapo.

Sehemu pekee ambayo hakuna watu wa kutosha ni Striker.
 
Hivi Henderson anatolewa kisa nini?..

Hatoshi kuwa 2nd goalkeeper..au anataka game time ya kutosha?

Hii move sijaielewa kabisa.
Naona kocha kachagua De Gea awe no 1 msimu ujao. Dean anataka game time watoto wanaibuka tu pale England kila leo, anahofia kupotea kabisa nadhani
 
Hii timu hii sasa wachezaji wanatoka tu sasa wanatoa kipa kijana huyu mbona akili za hii timu sizielewi.View attachment 2270766
Henderson ni kipa mzuri na yeye kulazimisha kupewa mechi za kutosha ni suala linaeleweka kabisa. Kitu kizuri United hawajauza kabisa maana bado kama watu hawana uhakika pale Sheffield United (PL) ni one season wonder au vipi? Hii move nzuri sana kwake na kocha, mwisho wa msimu kocha atapata picha nzuri kipa yupi anamfaa kwenye timu yake maana rebuild ndiyo kwanza inaanza.
 
Hivi Henderson anatolewa kisa nini?..

Hatoshi kuwa 2nd goalkeeper..au anataka game time ya kutosha?

Hii move sijaielewa kabisa.
Henderson hawezi kukubali Kuwa choice no 2, ni kipa mzuri kwa Timu yoyote ile midtable epl pale. Aliwafikisha Shefield mpaka nafasi ya 6 kabla ya Corona.
 
Duh city na liver pamoja na ubora wa vikosi vyao ila wameongeza watu tusidanganyane shida sio kocha pekee hata uwezo binafsicwa mchezaji mmojammoja bado toko nyuma sana man kuna wachezaji city na liver na timu nyengine kikosi cha kwanza hawewezi kupata nafasi ! mfano dm wa rodri ila wameongeza philips we una Mctominay,fred,perreira na garner
 
Man. City mabingwa wa PL na bado wamesajili DM kabla yetu. [emoji58]

Next season nafasi 2 za top 4 tayari ni 100% Liverpool na City wana uhakika kuwepo, Spurs ya Conte haikosi pia hiyo moja inayobaki ndiyo ya wachovu waliobaki.
Arsenal,chelsea na westham man u labda 8 au 9 tusibiri
 
Uongozi mzima wa MUFC unamatatizo. Ukubwawa club, uwingi wa mashabiki na vyanzo vya mapato vinawaponza na kuwafumba macho na hivyo kushindwa kuona hali halisi na kuchukua hatua. Nasiki Cristiano Ronaldo anafikiria kuondoka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…