Manchester United (Red Devils) | Special Thread

mgogoro wa mourinho dhidi ya paul pogba ndio ulimfaidisha scott mctominay, jose alimpandisha kutoka academy. uwezo wa mctominay ni wa kuchezea vilabu kama burnley na si kuwa regular starter wa manchester united. Tumerudi nyuma sana.
Chelsea wana kikosi kizuri sana na wanatoa wachezaji wengi sana kwenye timu za taifa.

Ilihali Manchester hata kwenye Olympics tu kwenye timu ya taifa walikuwa na mchezaji mmoja tu ambaye hakucheza hata mechi moja.
 
Unamnunua Harry Kane unamuacha Patrick Schick ?
 
mnaonaje wadau jamaa atakuwa msaada kwenye tatizo la kiungo ? inasemekana deal done
 
Lakini pia ni wachezaji wachache sana nje na waingereza ambao wamekua wakitupa mafanikio all the way.. With exception ya Ronaldo, Berba (atleast) na RVP ni mchezaji gani non English aliyekuja na kufanikiwa?
Ungetaja waingereza waliotupa mafanikio with exception of class 92 ,ferdinand na rooney ndo ujue jinsi walivyo vimeo pamoja na wingi wao pale utd
 
Huyu dogo Garnacho msimu ujao awe first 11.. Mali hii aisee, dogo anaujua
 
Lakini pia ni wachezaji wachache sana nje na waingereza ambao wamekua wakitupa mafanikio all the way.. With exception ya Ronaldo, Berba (atleast) na RVP ni mchezaji gani non English aliyekuja na kufanikiwa?
Reecruitment yeyote inakupa kile unachostahili.

Ukifanya vibaya lazima upate magarasa.

Bissaka, Maguire ni costful signings za hovyo United ilizifanya.

Huwezi toa £100M kwa Rice wakati kuna maelfu ya cheaper options.

Proper recruitment itatupa watu sahihi kama wakati wa SAF.

Kuliko kumnunua huyo Kane bora tubaki na Ronaldo.
 
Msimu uliopita pia mlisema msimu huu mtaupiga mwingi mpaka kumwagika, naona mnaelekea kuumwaga carabao hukooooooo
United siyo kwamba ina kikosi kibovu kuna vitu tu havipo sawa na kwa ujio wa EtH kuna matumaini kidogo tunayo pia kuna wachezaji baadhi wanaturudisha nyuma: uwezo mdogo kuliko matarajio, viwango kushuka, mbinu za kocha hazifanyi kazi pamoja na uvivu.

Just imagine midfield yetu kama tukimpata de Jong na DM mwingine atakayependekezwa na kocha.

BRUNO
de JONG
FRED
(Any possible DM)

Hao wote niliowataja Bruno kiwango kimeshuka ila ni mchezaji anayejituma tofauti na mchezaji kama POGBA (lazima aondoke) FRED ni mchezaji mzuri na anajituma sana uwanjani na kuna position akicheza anafanya vizuri sana tofauti na McTominay.

Kitu pekee ninachoomba United dirisha la usajili waepukane na hawa overpriced English players na wageukie cheap options ambazo kocha atapendekeza. Naamini ujio wa de Jong hautafuta usajili wa DM, CB, ST na Winger ambaye kwa tetesi ni Antony.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…