Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hivi Man U tuna scouting department kweli?
Mtu kama Camavinga, Diaz why are we missing them na mchuzi tunao?

Man U inaamini kwenye Majina na sio Vipaji ndiyomana imeacha Fabinho ikasajili Fred, ikaacha VVD ikasajili Maguire, ikaacha Diaz ikasajili Sanch.

Sasahivi kupigwa kwa Haaland is loading....
 
Boss Rangnick amekuwa akisema mara kwa amara anapoona kuwa ndio tatioz la United mbele ya vyombo vya habari. Aitha kwa utashi wake au kama moja ya majukumu yake pale United,amekuwa mtu wa msaada sana kwetu msimu huu bila kujali matokeo ya uwanjani.
Baada ya matamshi yake tumeona jinsi wakubwa wanavyomwaga manyanga na kutuachia timu. Naweza kusema Rangnick ndio usajili wetu bora kwa msimu wa 2021/22 maana ametufanya tutafute chanzo cha tatizo letu la msingi.

Nimesikia taarifa kuwa Matt Judge yule mshikaji wa mikataba ya 10% naye anang'atuka kwenye nafasi yake.
 
Nakumbuka Manchester United ndo tulikua na possibility kubwa ya kumsaini Camavinga, ila hata Fabrizio Romano anakwambia anashangaa deal lilivyopinduka. Scouts wa Man United wakasema Cama sio type ya mchezaji wamtakae
Scouts Wa Man United Hawamjui Hata Christopher Nkunku...Ralf Mwenyewe Alibaki Kustaajabu Tu, Scouts Wa United Waambie Kuhusu Harry Kane, Decline Rice Au Kalvin Phillips Apo Ndo Wanaelewa.
 
Anaondoka summer.

Maandalizi ya Glazers kutimka.

Msimu ujao hauishi, glazers wanaweza tema ndoano.
 
Kashasepa jamaa, hii rebuild isipofanikiwa kitakachobaki Man U ni ishuke daraja tu sasa
 
Scouts Wa Man United Hawamjui Hata Christopher Nkunku...Ralf Mwenyewe Alibaki Kustaajabu Tu, Scouts Wa United Waambie Kuhusu Harry Kane, Decline Rice Au Kalvin Phillips Apo Ndo Wanaelewa.
Wale wazee wapo toka enzi za Fergie mf. Chief scout Jim Lawlor alikuwa na Man United kwa miaka 16 tunajifunza nini? Bora wameondoka aisee
 
Jombaa hakuna mchezaji anayeweza kukataa kuja kucheza United. Mfumo wa uendeshaji wa timu toka walipostaafu kwa pamoja Fergie na David Gill (boss mkuu) ulibadilika sana, ukaacha mamlaka kamili kwa bodi kuamua uelekeo wa timu.

Sajili nyingi za United ndani ya miaka 10 zinaongozwa na msukumo wa kibiashara na sio mikakati benchi la ufundi mara nyingi makocha wamekuwa wakiletewa wachezaji hata nje ya matakwa yao wenyewe Van Gaal na Mourinho waliongea wazi wazi juu ya hili.

Ole aliletewa Amad na Pellistri ila sio yeye moja kwa moja aliyewahitaji. Nafikiri walikuwa recommended na baadhi ya watu wenye ushawishi ktk bodi wakiamini wana potential kubwa sana kwa baadae ila in reality wanakuwa hawapo ktk mipango ya kocha.
 
Pia kitu kikubwa sana kinachowavuta wachezaji wadogo ni kocha husika anayewahitaji. Wengi hupenda sana kuja kocha ana mipango gani na wao kwa muda mrefu.

Hao wachezaji uliwataja hapo juu kwangu mimi sioni hata mmoja anafaa kuja kwetu. Haaland, Felix, Bellingham - <Muingereza #Clowns > ( wote hawa ni too expensive), Karim Adeyemi (Alijiunga na Dortmund toka mwaka jana June - makubaliano ya awali). Usiangalie habari za magaeti ya Uingereza yamejaa udaku ili kuuza nakala.
 
Kwa attitude ya wachezaji waliopo angekua polluted,Naamini tusiweza ku-expolore potential yake.
Kwa malezi ole aliyowapa wachezaji, aliwaharibu. Unawezaje mchezaji anafanya makosa unampetipeti. Moriinho hakutaka ujinga, Ferguson hajawahi kuishi na mchezaji Kwa kumsifiasifia. Ni wapuuzi Sana. Kibongobongo ni sawa na kupetpeti mwanao .. Baadae unashangaa akiwa panyaroad,akiwa chokoraa anakuwa nunda. Pogba anisamehe lkn ni kama nunda pale united.


Kama kweli hii msms ni yake anawafundisha nini wadog zake
 
Edited tu hiyo imetengenezwa na wahuni wa Twitter
 
Short and clear naomba wadau wa United kila mmoja ataje USAJILI wa watu wa nne ambao yeye km shabiki lkn akihusianisha na reality ya timu yetu....kila mmoja atoe short analysis kuhusu hizo sajili na kwann ahisi zitatusaidia.

1. Nunez km forward na umri wake nahic atatusaidia
2. Nkunku wa Leipzig jamaa anajua sn msimu huu ana goal 17 na assist 13 na gharama yake tunaiweza around £55 million
3. Anthony kutoka Ajax gharama ni £ 55 million. Atatusaidia wing ya kushoto na ni mzr wa chenga, pass na anacheza kitimu pia hataanguka coz anakuja na mwalimu wake ETH
4. TIMBER anacheza RB na CB gharama ni £30 million atafaa kuboresha ukuta wetu.
5. Touchamen kutoka ligue 1 jamaa ni pogba mwenye nidhamu na bidii .
naamini tukileta hawa watu lzm ttakuwa bora msimu ujao.

Karibu na ww upendekeze sajili zako 4 au 5 ambazo unaamini zitatuamarisha msimu ujao
 
Man City is praying that Spurs defeat liverpool so that they can secure the Epl

Arsenal is praying that Spurs lose to Liverpool so that they can be in top 4 and go for Champions league next year

Man U is praying for Russia to bomb England and the league becomes null
 
Kuna uwezekano Haaland akaja United. Hata binafsi nakubaliana na hilo.

Ni natural goal getter. Akikupa goli 30 kwa msimu na Ronaldo akikupa nae 25.

Mnakuwa kwenye nafasi nzuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…