Solskjær: "I’m not here to explain every single detail of how I want my team to play. We want a central midfielder who can play. Today’s football is about he’s a good 6, 8, 10."
Sijui watu huwa wanatoaga wapi ujasiri wa kumtetea Ole.
Tuna kikosi kizuri sana kuliko timu yoyote ile pale ulaya ila inaongozwa na bogus.
Tutaishia kusema hivi hivi kila msimu sijui DM alihitajika sijui nani tulimhitaji. Ukweli ni kwamba tunapoteza muda na Ole.
Mapungufu ya Ole ni Game management skills - kama huna hii kitu huwezi kubeba mataji hata siku moja.
Sipendi kujilinganisha na wenzetu ila timu kama Chelsea, Man City na L'pool hawana ubora wa kikosi tulichonacho lakini wana ubora mkubwa sana ktk safu ya ufundi.
Mf. Mtu kama Tuchel sio kocha wa juu sana kama Pep ila ana game management skills ya hali ya juu sana. Jaribu ku-review mchezo wake dhidi ya L'pool (sare) na ule dhidi ya Villareal UEFA super cup.