Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kwa mtizamo wangu.
Tatizo la Ole hajawahi kuwa muwazi linapokuja suala la mapungufu ya timu yake kama alivyokuwa Mourinho bali hutoa jibu la pamoja tu kuwa timu imefanya vizuri bila kusemea uwezo wa wachezaji katika nafasi zao. Hivyo inakuwa ngumu kujua kama anaridhika na alichonacho kulingana na mbinu zake au la.
Lakini tumefundishwa kitu tangu ujio wa Bruno kuwa wachezaji wenye kiwango na kiu ya mafaniko ndio wanambeba Ole,hivyo basi kutokana na kundi alilonalo inawezekana akafeli kwa sababu zile zile zilizomfelisha mwaka jana.
.Mbavu ya kulia haipandishi timu
.Kuchezesha Mc Fred Inampunguzia nguvu na idadi kwenye eneo la ushambuliaji.
 
Yaani kwenye usajili sijui tunakwama wapi. Wachezaji wa kawaida ndiyo tuko sokoni wa nguvu tunasepa. Tunaonekana hatuna malengo ya kushinda kikombe chochote musimu huu tena View attachment 1882960
Huyu Ole naye ni kama analetewa wachezaji tu. Sasa kama amemaliza target zake huo mlango kauacha wazi wa kufanya nini?
Ina maana mashabiki na wachambuzi wote hawako sahihi kuhusu nafasi ya DM?
 
Si rahisi bado kikosi chepesi. Kwenye nafasi ya namba 9 bado panapwaya mana kuna Cavan tu ndio uhakika ila naye umri si rafiki sana. Pia kuwategemea Rashford, Martial na Greenwood ni kama kucheza kamali tu. Ukijumlisha na uwezo Wa Kocha ndio balaa!
 
Leo umeongea point
 
Cantwell juzi katoa assist moja ya kinyama sana huko kwenye pre-season..ni mchezaji mzuri..

Kiungo tu akishaweza kukuota mipira na kuwa na jicho la pasi basi huyo tayari ni fundi..This is lacking kwa kijana wetu Van de Beek.
Van De Beek siyo mkokota mpira ila huwa anautembeza mpira kwa kasi kubwa kuliko kawaida kwa njia ya quick passes.

Tatizo linaijia pale unayetakiwa kumpa pass hafanyi runs sahihi na akipewa pass anapiga back pass.

Kinachomtesa Donny ni intensity ya ligi yetu na ufalme wa Bruno na Pogba.

Nafikiri anajipima kupitia hao viumbe hivyo unapoteza confidence.
 
Laissez faire attitude
 
Barcelona walipitia situation kama ya kwetu tu kufanya signing kwa panic bila kuzingatia mahitaji muhimu ya timu.

Baada ya Neymar kuondoka walihitaji sana msaidizi wa Messi wakajitosa kwa Griezman lakini akageuka Ditram Nchimbi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…