Ole hana mbinu!!, anaongea hivyo myu ambaye hata team ya darasa hakuwahi fundisha.
Tushakuwa na makocha wa mbinu zote, Van gaal( kumiliki mpira), mpaka kuzuia ( Mou) hakuna cha maana tulichoambulia.
Ole hana mbinu? anawezaje kushinda mechi kubwa bila mbinu.
Niambie Ole hana mbinu zinazonifurahisha, au Ole hana mbinu za kufanya team icheze kama navyotamani, hapo utaeleweka.
Mpira anaojaribu kuufundisha Ole ( kama ukifanikiwa) ndio uliotufanya wote tuipende Man U ( tokea enzi za fergie man U ina style yake ya kiuchezaji) .
Ukitaka mpira kama wa Man city kamwe hutoupata Man U narudia kamwe, ko ni bora ukakubaliana na hali tu.