Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Raiola on Haaland and Pogba

Could Haaland produce the same economic returns as Pogba, for example?
I think it's different. I had a Ballon d'Or, Nedved who in terms of marketing was a zero. Whereas, imagine Balotelli with Messi's head, because he's got the quality. And Paul [Pogba] is the number one at this. If he'd played at Madrid or Barça, he'd be the player generating the most amount of money.
 
After Haaland, is Pogba one of Raiola's main concerns for this transfer window?

When a player asks you, what are we going to do?, it's an enormous responsibility. That's when you stay up all night thinking about what's best... My aim is to make it a process alongside the player to see what they really have in their heart. Ibrahimovic knew I was against him going to Barça, he wanted to go because it was an incredible Barça side. And although people might think differently, I think that [this failed move] was really important, not a major disaster. Because he learnt so much more in six months than in major stretches of his life.

With Pogba, what’s really important too is what Manchester United want, what project they are proposing for Pogba. Pogba has always been interested in one thing, winning the Champions League, titles, that’s his objective. And we’ll see if that’s possible at United or at other big European clubs.
 
Why is Pogba not already at Real Madrid?

It's a question for Madrid. At one time, Pogba felt a lot of love for, and trust in, United, and there are various other clubs... Afterwards, it's really hard for United and Madrid to reach an understanding on a massive transfer, because big clubs don't like selling great players to other big clubs. And I'm not going to kid you, for Pogba, playing at Madrid was always a really attractive option, because of Zidane too. He's Pogba's childhood hero.
 
matumaini na mawazo ya mashabiki
ujio wa paul pogba ndani ya manchester united ulileta matumaini makubwa sana ya kwamba tumeanza rasmi process ya kujenga timu bora itakayoleta ushindani kwa muda mrefu barani ulaya, wengi wetu pia tulijawa na imani ya kushuhudia maingizo bora ya wachezaji wengine baada yake hii ni kwa sababu tuliamini hakuna mchezaji mwengine yeyote tutakayeshindwa kumsajili kwa sababu ya dau lake (tumeweza kwa paul, kwa nini tushindwe kwa raul). Si hivyo tu bali pia ujio wake ulituaminisha ya kwamba kupitia paul ndio utakuwa msingi wa manchester united kiuchezaji

matumaini ya paul na wakala wake
Mino anatwambia ndoto kubwa ya paul ni kushinda michuano ya ulaya, Ina maana kitendo cha mteja wake kurudi tena manchester bila ya shaka kulitokanwa zaidi na mikakati bora waliyoelezwa na upande wa manchester united nyakati hizo wanafanya mazungumzo ya kibiashara kati ya pande mbili hizo. Sitaki kuamini ya kwamba paul amerudi tena kwetu kwa sababu ya mshahara pekee huku akitupilia mbali ndoto yake tajwa hapo juu.

chimbuko la kusambaratika kwa mahusiano
Bila ya shaka imani ya watu wawili hao ilianza kufifia baada ya kushuhudia kusuasua kutekelezwa huo mkakati bora wa kiuwekezaji walioelezwa nyakati hizo na upande wa mancheter united. Naamini mkakati lengwa hapa ni suala la usajili wa wachezaji bora watakaoungana na pogba kwa dhumuni la kujenga timu bora pamoja na kuondoa wachezaji wenye viwango visivyoendana na hadhi ya manchester united (sitaki kuzungumzia mzunguko wa usajili wetu)

ukiongezea na matokeo mabovu ya timu (sometime paul hakuwa muhusika mkuu), kushushiwa shutuma paul na kocha mkuu kwa kushindwa kuonyesha kiwango bora (mgogoro wake na jose), kelele za mashabiki, wachambuzi na legends kulizidi kuchochea moto kwa upande wa paul kutamani kuondoka lakini klabu iliendelea kusimamia msimamo wa kutokuruhusu paul aondoke licha ya mwalimu naye kuonyesha nia ya kutamani kumuondoa paul, hatimaye tulishuhudia kuondoka kwa mwalimu na kubaki kwa paul

Pogba na ugonjwa wake binafsi
majeruhi ya mara kwa mara yanayomfanya atumie muda mwingi kitandani, mshahara mkubwa usioendana na anachotupa tokea asajiliwe, kukosa mchezo bora (consistency) jambo linalopelekea asiwe na nafasi ya uhakika na nafasi maalum ndani ya kikosi, ukiongezea na matatizo ya wakala wake ya ubwatukaji na uchonganishi yanazidi kuchochea hasira za wanafamilia ya manchester united wanaotamani kuuona mwisho wa paul akiwa na jezi nyekundu, si hivyo tu bali pia tabia za wakala wake zinaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa sana vilabu vyenginevyo kusita kufanya biashara naye kwa hofu ya muendelezo wa matendo yake

man utd na ugonjwa wake
hatuna mchezaji mwengine anayelingana na paul kiuwezo kwenye nafasi yake hivyo basi inakuwa ni vigumu kwa united kuwaridhisha mashabiki wanaotamani paul aondoke na kuleta mchezaji mwengine, bado tuna matatizo mengi ya kiufundi tunayopaswa kuyatatua kama vile eneo la ushambuliaji, kiungo wa chini mwenye uwezo wa kutimiza majukumu kwa ukamilifu (aliyebora zaidi ya scott na fred), winga wa pembeni, mlinzi wa kati, mlinzi wa kulia mbadala wa wan bissaka,
Maafikiano ya pande mbili ndio suluhisho

sidhani kama upande wa raiola bado atakuwa na jeuri yenye kuambatana na upofu wa kuamini ya kwamba bado ana nguvu ya kuzishawishi timu kubwa kumsajili mteja wake kwa dau litakalowekwa na upande wa manchester united bila ya kusahau maslahi binafsi ya kwake (pesa ya wakala) na ya mteja wake. Juve wapo hali mbaya kifedha na kiuchezaji, Paris wanaweza kuvutiwa naye ila ishu ni FPP na dau litakalowekwa na man utd, real madrid wameshampa kandarasi luka modrik kwa maana ya kwamba eneo la kiungo halitakuwa kipaombele chao (ukiongezea na kipigo cha corona ndio zaidi haitokuwa rahisi kwa hivyo vilabu kumtafuta edwoodward)

pia sidhani kama klabu itakuwa tayari kujiingiza katika msako mwengine wa kutafuta mchezaji atakayerithi nafasi ya paul baada ya kuondoka kwake, tumekuwa wazito sana kukamilisha usajili wa mchezaji hatimaye tunajikuta tunatumia wiki kadhaa kufanya negotiation na pande hasimu, kumuondoa paul na kuleta hapo tunazalisha process nyengine ndefu na ya gharama.

Naamini klabu itatumia njia ya mazungumzo na upande wa paul ili asaini kandarasi mpya yenye maboresho ya maslahi na si vyenginevyo, klabu haitokubali kuuziwa uhuni na raiola kwa kumuachia pogba aondoke bure kama wanavyofanyiwa AC milan kwa donnarumma.
" kwa sasa Pogba, raiola na manchester united ni wakorofi wanaohitajiana"

pumba za daemusin
 
Mkuu kwann umeamua kutumia jina la huyo kocha wa wapinzani wetu wa jadi?
napenda nihukumiwe kwa ninachokiandika na si username ninayotumia ndio maana nabadili majina mara kwa mara. kuna tabia imezuka humu ndani ya JF kupeana credit ovyo kwa sababu tu ya nguvu ya username (ndio naipinga kampeni hiyo kwa njia hii)
teh teh teh
=============
nilimpima na nagelsmann pamoja na verified name ila nikaona bado mizani inaelekea kwenye jina la klopp,
tusisahau klopp ni muajiriwa tu wa liverpool na si mwanachama, hata mwanzoni sisi tulimtafuta klopp ila mikakati yetu hakuvutiwa nayo ndio akaenda liverpool mbeleni
 
Inapendeza sana kuona Man U inaenda kuamua tena ubingwa wa Man city Kama ambavyo iliamua msimu wa 2018/2019 guys kesho mkifungwa na Liverpool hata 1 itapendeza Sana kumbukeni tunatoka Jiji laManchester wote.
 
fred ni mchezaji bora mbele ya scott mctominay, kwa mara ya kwanza nilifanikiwa kuligundua juzi tulipocheza na As roma baada ya kumchunguza scott, licha ya kuwa na mechi mbovu siku za karibuni bado fred anabaki kuwa na mchango bora ndani ya kikosi (hapo ndipo unaposhangazwa na takwimu). Nimegundua kuna tabia ya upendeleo imezuka ndani ya mashabiki na hata benchi la ufundi juu ya wachezaji hao wawili, scott analindwa sana kuliko fred labda ni kwa sababu mmoja tumemsajili kwa dau kubwa hivyo basi tulijawa na matarajio makubwa zaidi ya haya anayotupa kila siku uwanjani.

hawa wajinga newcastle united ndio walitaka kutuuzia sean longstaff kwa paundi millioni 50 au kwa sababu ni muingereza?
1619875636337.png
 
fred ni mchezaji bora mbele ya scott mctominay, kwa mara ya kwanza nilifanikiwa kuligundua juzi tulipocheza na As roma baada ya kumchunguza scott, licha ya kuwa na mechi mbovu siku za karibuni bado fred anabaki kuwa na mchango bora ndani ya kikosi (hapo ndipo unaposhangazwa na takwimu). Nimegundua kuna tabia ya upendeleo imezuka ndani ya mashabiki na hata benchi la ufundi juu ya wachezaji hao wawili, scott analindwa sana kuliko fred labda ni kwa sababu mmoja tumemsajili kwa dau kubwa hivyo basi tulijawa na matarajio makubwa zaidi ya haya anayotupa kila siku uwanjani.

hawa wajinga newcastle united ndio walitaka kutuuzia sean longstaff kwa paundi millioni 50 au kwa sababu ni muingereza?
View attachment 1770143
Fred>>McTominay
 
Na mkifungwa na Liverpool, Rasmi mnamtangaza CITY bingwa EPL 2020/201.
Binafsi sina shida na City tukimpa ubingwa kesho. Japo nitafurahi zaidi kama tukimpoteza maboya L'pool ili asishiriki michuano ya Ulaya msimu ujao.

Msimu wa mwaka 2009/10, Chelsea alichukua ubingwa kwa points 86 wakati sisi United tulikuwa na points 85. City alitusaidia kumfunga Chelsea mechi zote mbili home & away.

L'pool wakatufanyia roho mbaya Steven Gerrard alitoa boko makusudi kwa kumpasia Didier Drogba ili Chelsea washinde wabebe ubingwa. Tulikuwa na utofauti wa point moja tu kama mechi ingeisha sare sisi tungebeba kombe.
 
Inapendeza sana kuona Man U inaenda kuamua tena ubingwa wa Man city Kama ambavyo iliamua msimu wa 2018/2019 guys kesho mkifungwa na Liverpool hata 1 itapendeza Sana kumbukeni tunatoka Jiji laManchester wote.
Jombaa, nyie mmeisha chukua kombe haijalishi matokeo ya kesho. Huwa sinaga kinyongo na City ila wale watu wenye roho mbaya L'pool tokea mwaka 2010 Steven Gerrard alipotufanyia ule uchoko sijawahi kuwasamehe mpaka leo.

L'pool sio wana michezo ni watu wenye wivu wa kike sana, waliona ni kheri wafungwe makusudi ila sio United kubeba ubingwa.
 
Binafsi sina shida na City tukimpa ubingwa kesho. Japo nitafurahi zaidi kama tukimpoteza maboya L'pool ili asishiriki michuano ya Ulaya msimu ujao.

Msimu wa mwaka 2009/10, Chelsea alichukua ubingwa kwa points 86 wakati sisi United tulikuwa na points 85. City alitusaidia kumfunga Chelsea mechi zote mbili home & away.

L'pool wakatufanyia roho mbaya Steven Gerrard alitoa boko makusudi kwa kumpasia Didier Drogba ili Chelsea washinde wabebe ubingwa. Tulikuwa na utofauti wa point moja tu kama mechi ingeisha sare sisi tungebeba kombe.
itakuwa bwana gerrard ana uhusiano wa karibu na chelsea, unakumbuka kituko chake dhidi ya demba ba msimu wa 2014
 
itakuwa bwana gerrard ana uhusiano wa karibu na chelsea, unakumbuka kituko chake dhidi ya demba ba msimu wa 2014
Steven Gerrard kama akiwa ktk situation ya Manchester United achukue ubingwa au L'pool wafungwe washuke daraja. Jamaa atachagua wafungwe na washuke daraja ila sio kinyume chake. L'pool wana ushindani wa kitoto.
 
Back
Top Bottom