Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Dogo Amad anaonekana sio mbinafsi kabisa..Jana katoa assist tatu na ni assist za upendo kabisa..
 
Sijajua sosha katumia vigezo gan kumchezesha huko under 23 wakat huyo dogo kacheza atalanta timu ya wakubwa
Mkuu kucheza U23 ni kawaida. Ni kama kautaratibu fulani hata hawa wachezaji wakubwa wakiwa wameumia muda mrefu, wakipona kabla hawajarudi kwenye nafasi zao wanapiga at least mechi moja ya U23.
Sijajua kwa timu nyingine but kwa Manchester united ni kawaida hata kina Baily wanachezaga U23
 
Huyu akija timu ya taifa huku lazima wamroge
 
Hivi Ole aligawaje points kwa Gunners,dah sitakuja kumsamehe labda UTD uchukue EPL au ndoo yoyote this season
Tatizo kwenye hizi big matches tumeingia sana kiuoga uoga..Arsenal sio timu ya kushindwa kuchukua japo point tatu.

Tunakuwa hatutengenezi nafasi nyingi kwenye hizi mechi(apart from Arsenal away) na zikitengenezwa chache fowards wetu wamekuwa butubutu..yaani mpaka wapate chansi nyingi ndo washinde..Hili limetucost sana,tungekuwa tunaongoza ligi kwa gap zuri tu.
 
Wakuu Leo Sina access na TV kabisa
Naomba app itakayoonesha mechi yetu au website ambayo haina magumashi
#GGMU
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…