Bavaria,
Ujue bado ubovu sio benchi la ufundi bali ni wale watu wa juu wafanya maamuzi ndio wacheleweshaji wa mambo. Hata huyu Donny Van De Beek mtu anaweza kujiuliza mbona tumepeleka offer moja tu fasta ikakubali ukweli ni kwamba Edwin Van Der Sar kapokea offer yetu bila ku-negotiate na kama angeamua ku-negotiate basi Ronald Koeman alishaanza kuomba pesa ktk bodi ya Barcelona amnunue.
Mapungufu yapo lakini ukweli utabaki Ole ndani ya msimu wake wa kwanza kamili kama kocha mkuu kamaliza nafasi ya tatu. Bado naona kama akipewa mahitaji yake anaweza kufanya kitu. Ed yupo slow ku-match na bench la ufundi muda mwingi analeta wachezaji nje ya wakati sahihi.
Kwa mfano kwa sasa tunahitaji sana beki wa kati na mshambuliaji mmoja mbele. Siwezi kuhamaki kama tukisajili haya maeneo mpaka pressure za mashabiki zianze. In fact, Ed sio mtu sahihi kuendesha timu ya soka anapaswa akafanye kazi kama chief financial officer (CFO) ktk investment banks maeneo ya London huko.