Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Another individual perfomance well done bruno
skysports-20200710-0001.jpg
 
mtzmweusi,
Nadhani Mason anatufuta machungu ya kumkosa halland


Mimi ni moja kati ya watu wachache ambaye niliupinga sana usajili wa Erling Haaland kujiunga nasi na hata tulipomkosa nilifurahi. Binafsi niliamini tusingeweza kuwa-accommodate wote wawili kwa wakati mmoja bila mmoja kuua kipaji chake.

Na haya ndiyo yaliyokuwa maoni yangu kabla hata hajajiunga na Borussia Dortmund:

Dec 17, 2019

Kuna jambo hapa kuna baadhi ya watu wananifurahisha sana, Erlin Haaland wanini wakati tuna Mason Greenwood? Tena kwangu mimi naona Erling anacheza mahala ambapo hana pressure na kapewa muda zaidi kuliko Mason. Kwangu mm kama ananunuliwa mshambuliaji basi anapaswa awe mzoefu kuja kumpa uzoefu mtu kama Mason calibre ya Harry Kane na sio kinda mwenzie tena ambaye anamzidi uwezo. Kama kuna kitu kitanifanya nilidharau bench letu la ufundi ni kumnunua huyu Erling. It's a total joke! And It will be very disrespectful kwa Mason.
 
Popular opinion....Watu wengi wanaichukia United kwa sababu ya mateso iliyowahi kuwapatia hasa kipindi cha Sir Alex Ferguson. Babu alipostaafu ikawa Neema na ndereko kwa hawa wapinzani. Mara hii kuiona tena United ikiwa na kila dalili za kurejesha zama zake, inawauma sana watu zaidi ya kisu cha ngariba. Tusiwanyanyapae,(hawana Covid-19)...ni ndugu zetu wenye majeraha mengi rohoni, deep down wanatamani lingekuwa chama lao ila ndo hivyo tena.

Manchester United ni zaidi ya FC, ni Imani katika Soccer, ni alama ya Ushujaa na ushindi iliyo kwenye DNA ya wafuasi wake.

Win or lose, we are forever UNITED.
 
Back
Top Bottom