Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Akifa leo tutasema alikuwa na miaka 31 Mkuu
..AW, soko la DMs ni gumu kidogo, tunam-nurture Mactominay awe mrithi wake asiboharibikiwa.....With due respect, Matic deserves the contract aki-flop tunamuuza sio kuondoka bure
simple like that Mkuu
 
Nemanja hadi 2023


Mkataba mrefu sana kwa umri wake
ingelipendeza kama wangelimpa mkataba wa miaka 2 wenye kipengele cha kumuongezea mwaka 1 kama walivyofanya kwa juan mata...
========================

kupewa kwake mkataba wa muda mrefu haimaanishi ya kwamba atakuwa ni mchezaji wa uhakika wa kikosi cha kwanza bali performance yake ndiyo itakayoamua mustakabali wake kama ilivyo hivi sasa (mwanzoni mwa msimu muda mwingi aliutumia benchi), ina maana ikiwa klabu itachoshwa na uwepo wake wana uwezo wa kumruhusu aondoke huku klabu ikitengeneza faida ya mauzo yake kama ilivyokuwa kwa ashley young tofauti na kuondoka mwishoni mwa msimu huu.

Management imezungumzia ishu ya experience aliyonayo na heshima kwa young players​
kwa tafsiri ya haraka ni kwamba klabu haipo tayari kwa sasa kuingia sokoni kwa lengo la kutafuta midfield mwenye sifa yake (tetesi za ndidi, partey na wengineo zimezimwa rasmi) ila wataendelea kuwatumia hawa waliopo (fred na scott) huku wakiendelea kuyafuatilia maendeleo ya kisoka kwa wachezaji vijana waliopo klabuni (garner na levitt).

cha umuhimu ni kuomba mzee matic aendelee kucheza kwa nidhamu hii aionyeshayo majira haya ya 2020, huenda atakuwa ndiye michael carrick wetu.
=================

halafu hii ishu ya kuextends mkataba mpya kwa mchezaji asiye na impact kubwa sana uwanjani nayo ni kama kamari, nakumbuka katikati ya msimu uongozi wa klabu ulimshinikiza ashley young asaini kandarasi mpya huku mashabiki wengi tukichukizwa na uamuzi huo bahati nzuri sana ashley young alisoma alama za nyakati na hatimaye akaamua kuondoka mwezi January.

rejea ishu ya fellaini, alipewa kandarasi mpya kwa sababu ya shinikizo la mwalimu lakini tulipofanya mabadiliko ya benchi la ufundi tukapata bahati ya kumuuza kwa hela nzuri...

kwa sasa tumecheza kamari kwa marcos rojo na phil jones, wote hawa tumewapa mkataba wa muda mrefu huku mustakabali wao ukiwa haujulikani (mpaka sasa hakuna timu zilizoonyesha nia za kuwahitaji)

nadhani ndio maana baadhi ya mashabiki wana wasiwasi na hii dhana ya kutoa mkataba wa muda mrefu kwa wachezaji waliovuka peak ya ubora wao
 
Mkuu unadhani mimi napiga kupewa mkataba? Anastajili sana tu, anatubeba sana tu... But 3 years


Kweli ni wachache sana DM ni wachache sana

Mimi namuona Garner na Levit kama more DM watarajiwa kuliko Scoty, Scoty is more Box to Box
 
Mkuu unadhani mimi napiga kupewa mkataba? Anastajili sana tu, anatubeba sana tu... But 3 years


Kweli ni wachache sana DM ni wachache sana

Mimi namuona Garner na Levit kama more DM watarajiwa kuliko Scoty, Scoty is more Box to Box
nimekupata vyema Mkuu.....Tuliombee mema chama letu walau nasie tuanze tembea tena vifua mbele ka bata mzinga
 
Mkuu umeeleza vizuri


Logic behind ya huu mkataba ni hicho ulichosema

Obvious hapa nampa heko wakala wa Matic, kafanya kazi yake vizuri sana

Hapa hatusajili tena DM na hicho ndio kinanipa hofu sana, huwa kuna wakati Matic anapoteana kabisa mpaka watu mnatamani aondoke hata bure


Tusingepata mid field crisis kipindi kile cha Desember na January kuna uwezekano Matic tusingekuwa naye tena, maana hakuwa na kiwango cha kuridhisha

Ngoja tuone nini kinakuja mbeleni, sisi huku chini wapigania uhuru tunaishia kujadili tu


 
Ngoja tuone nini kinakuja mbeleni, sisi huku chini wapigania uhuru tunaishia kujadili tu
yes, hiyo ndio kazi yetu inayotukutananisha humu ndani japokuwa wapo wengineo huchukizwa na kazi hii kama alivyofanya mmoja wapo hapo juu....

sijui leo amepatwa na jambo gani bwana fortaleza, hii si kawaida yake (ni mpenzi mzuri sana wa mijadala ya soka)

panapo majadiliano ndipo pazaliwapo uhuru na heshima
 
Exactly, ndio maana nikaendelea kujadili na wale wenye lengo hilo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…